Pale uhakika wa kazi upo, , andaa hiyo barua kutoka selikali za mtaa ila unatakiwa kuwahi asubuhi saa kumi na mbili na nusu uwepo pale getini.
Kazi za mule ni za kawaidatu. Section ya kwanza kupanga viloba vyenye unga wa ngano vinavyotoka juu kwa winchi vya kilo5 kilo25 mpaka kilo50, Section ya pili nikupakia viloba vyenye unga wa ngano kwenye magari madogo na makubwa yanayoenda nje ya nchi na ndanj ya tanzania na ndani dar es salaam.
Nitaelezea Section yangu niliyowahi kufanya na lazima na wewe ndo mara yako ya kwanza lazima uanze na hiyo , , , nikupanga viloba vyenye unga wa unga wa ngano vinavyotoka juu kwa kutumia winchi
Malipo kwa shift ya mchana huwa inatoka pesa kima cha chini haipungui elf7 na kuendelea haizidi elf12 kula kwako ukumbuke, kazi inaanza saa mbili mpaka saa kumi na mbili ama saa kumi na moja kama sikosei za jioni . Na ikitoka elf7 ujue sku hiyo kazi ilikuwa hakuna
Malipo kwa shift ya usku huwa inatoka kima cha chini elf9 nakuendelea mpaka elf13 ama 14 kazi kuanzia saa moja na nusu mpaka saa kumi mbili za jioni kumbuka kula kwako
NB kazi zake sio za kitoto unabeba kilo 25 ama 50 huku unatimua mbio na kurudi kwenda kuchukua mzigo unarudi kwa mchakamcha Pale tuna jina la utani wabeba mizigo wote tunaitwa "Makuli

" na mule hakuna watoto waliozaliwa Dar es salaam wote nikutoka mikoani
Kuna unga huwa unakosewa kuchanganywa

maana huwa hakuna winchi ya kupandisha mpaka ghorofa ya tano ama sita na zinazokosewa kuchanganywa mara nyingi huwa kilo50 yaan siku ndo unaanza kazi bahati mbaya ukutane na hali hiyo ya kupandisha kilo50 kwenda ghorofa ya sita hata uwe na nguvu lazima uombe poo labda saivi iwe ishawekwa winchi ya kupandisha juu.... Asanteh sana ndugu zangu