Natafuta kazi za viwandani

Natafuta kazi za viwandani

Pole sana naona unatoa povu, usipanic ndugu. Kama mambo ya chuo hayakwenda vizuri unaweza tu kuwa mkweli.

Wote tunapambana kutafuta wala usijali,ukipata deal nishtue tu
Mimi sijapanic Ila wewe sijakuelewa unasema hivyo ili iweje...
Nasoma chuo ndio Sina Ada Sina pesa ya kujikimu.... Nimeamua kuomba connection unasema naogopa for what purpose????
 
Mwisho kabisa. Mwenzio anaposimama na shida usiwe Sehemu ya kumkatisha tamaa, kwasababu Leo kwako kesho kwangu..

Unakumbuka ulivyokuwa una haha kutafuta kazi????

Fanya Mambo YakoView attachment 2091246
uyo jamaa alie coment apo aliekua anasema anataka kutoa kazi ya ulinzi yeye mwenyewe juzi alikua anatafuta kazi umu ahaha umu watu waongo sana
 
Pale uhakika wa kazi upo, , andaa hiyo barua kutoka selikali za mtaa ila unatakiwa kuwahi asubuhi saa kumi na mbili na nusu uwepo pale getini.

Kazi za mule ni za kawaidatu. Section ya kwanza kupanga viloba vyenye unga wa ngano vinavyotoka juu kwa winchi vya kilo5 kilo25 mpaka kilo50, Section ya pili nikupakia viloba vyenye unga wa ngano kwenye magari madogo na makubwa yanayoenda nje ya nchi na ndanj ya tanzania na ndani dar es salaam.

Nitaelezea Section yangu niliyowahi kufanya na lazima na wewe ndo mara yako ya kwanza lazima uanze na hiyo , , , nikupanga viloba vyenye unga wa unga wa ngano vinavyotoka juu kwa kutumia winchi

Malipo kwa shift ya mchana huwa inatoka pesa kima cha chini haipungui elf7 na kuendelea haizidi elf12 kula kwako ukumbuke, kazi inaanza saa mbili mpaka saa kumi na mbili ama saa kumi na moja kama sikosei za jioni . Na ikitoka elf7 ujue sku hiyo kazi ilikuwa hakuna

Malipo kwa shift ya usku huwa inatoka kima cha chini elf9 nakuendelea mpaka elf13 ama 14 kazi kuanzia saa moja na nusu mpaka saa kumi mbili za jioni kumbuka kula kwako

NB kazi zake sio za kitoto unabeba kilo 25 ama 50 huku unatimua mbio na kurudi kwenda kuchukua mzigo unarudi kwa mchakamcha Pale tuna jina la utani wabeba mizigo wote tunaitwa "Makuli" na mule hakuna watoto waliozaliwa Dar es salaam wote nikutoka mikoani

Kuna unga huwa unakosewa kuchanganywa maana huwa hakuna winchi ya kupandisha mpaka ghorofa ya tano ama sita na zinazokosewa kuchanganywa mara nyingi huwa kilo50 yaan siku ndo unaanza kazi bahati mbaya ukutane na hali hiyo ya kupandisha kilo50 kwenda ghorofa ya sita hata uwe na nguvu lazima uombe poo labda saivi iwe ishawekwa winchi ya kupandisha juu.... Asanteh sana ndugu zangu
Duh sio poa
 
Mimi sijapanic Ila wewe sijakuelewa unasema hivyo ili iweje...
Nasoma chuo ndio Sina Ada Sina pesa ya kujikimu.... Nimeamua kuomba connection unasema naogopa for what purpose????
Mungu akuongeze mkuu, kila la heri, Maisha ya chuo bila financial support huwa yanakuwaga magumu Sana, Niliyaishi hayo maisha, Namshukuru Mungu kwa Neema yake nilimaliza, nipo mtaani napambana na hali yangu, Mungu akawe upande wako kwenye harakati zako za kusongesha gurudumu la maisha
 
Nenda pale buguruni.kwenye kiwanda cha bakhressa cha ngano.asubuh na mapema unagaiwa kadi unaandikisha jina tayari kwa kupangiwa kazi.
Note.msingi nguvu.
Pale uhuni mwingi kazi ni ngum kupita maelezo na wale vijana wanaosimamia wkt wa kazi ubinadam ht chembe hkn. We unazunguka na viroba vya unga kutwa nzima bila kujua utalipwa kiasi gani, mara hamaki unaambiwa imepatikana elfu nne, mara ukatwe elfu mbili ya form na wale vijana wanaokupokea ukitoa na buku ya msosi unakabidhiwa buku ndo ujira wako. Vijana tupambn tujiajiri aisee, hawa wahindi sio watu kbs!
 
Kwaiyo ulitaka niseme Mimi Ni mwanafunzi wa chuo Nina tafuta kazi za viwandani ili iweje??

Kifupi sitaki kuhusisha Jambo lolote na elimu yangu, Mambo mengine unatakiwa kusimama bila ya kuangalia una Nini.. Thus why sijasema Mimi Ni Nani.

Kwa upande mwingine unadhani naongopea watu ili iweje????

Mwisho Jitahidi Sana kufuatilia Mambo yako.. Lengo lilikuwa kuwa kutoa connection kwa Faida yangu na wengine..

Inshort Acha kiherehere maua Mtoto wa kiume.
Hili ni moja kati ya majibu konki humu jf kwa watu wasiojielewa na wasiojua mfumo wa maisha upoje,

Kwa hyo mtu akiwa na elimu ndo hapaswi kupambana kutafuta hela??
 
Back
Top Bottom