kubwa_Lao
JF-Expert Member
- Dec 12, 2015
- 934
- 1,183
Habari za asubuhi wadau,
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, nahitaji funcargo ingawa bajeti yangu ya 5M ni ndogo lkn ndio nahitaji gari hiyo iwe kuanzia namba C iliyo karibu na D na kuendelea.
Wadau mie hiyo ndio itakua gari yangu ya kwanza, sijawahi kumiliki gari hivyo mwenye nalo tafadhali tuwasiliane, pamoja kuwa ndilo gari ninalohitaji pia nakaribisha maoni au msaada zaidi wa mawazo ya gari ipi ni nzuri kutokana na bajeti yangu hiyo.
Passo nilikua naipenda lkn kutokana na maoni ya kitaalamu niliyoyasoma humu naona passo haitanifaa kwa kazi zangu za humu mjini lkn pia na kwenda mikoani.
Pia nitashukuru sana kama nitapata uzuri na ubaya wa funcargo.
Natanguliza shukrani.