Natafuta ajira Nina degree ya mechanical engineering

Natafuta ajira Nina degree ya mechanical engineering

mechanical engineering kama hauna GPA kuanzia ya 4,nenda kwenye viwanda vya wahindi,kama inaanzia 4 tembelea migodini hasa shinyanga utapata mshahara Wa kufuru
Usimtishe dogo ndio maana nyiny mnao jifanya mna GPA kubwa huwa nagonga practical vyet pemben

Huwa hatuangalii vyet siku hz tuna angalia uwezo wa kivitendo tu cha kumshaur akomae na practical tu.

Na hzo GPA zenu Kuna jamaa alilia kaja kavimba kapewa ka practical kadogo tu kamchemsha mzungu akamuweka kando akakosa 3.5m kwa mwez na marurupu ya sigara na bia
 
Usimvunje moyo mwenzako.
GPA na kazi ni vitu viwili tofauti.
GPA kubwa umuhim wake labda Kama unataka ukawe mwalimu.
Kwenye manufacturing industries wanachohitaji ni practical works na wala hawataki theories zako ulizomeza kwenye vitini ili upate GPA kubwa.
Kuna mawili eitjer huna GPA kubwa au unawaonea wivu wenye GPA kubwa.

Ivi injinia anaweza ku design bila kujua theory?
 
Kwa wewe unaweza ukaanzia kwenye gereji za mitaani uku ukiangalia na sehemu nyingine
 
Nenda migodini unaweza ukabahatika sema uwe na refa au utoe kitu upate kitu jaribu kahama,Geita,kakola mungu atakusaidia naamini ukipata Kazi mgodini utasahau shida wanatoa mishahara minono.

Nimesikia ule mgodi wa kahama uliofungwa wanakaribia kuanza kuajiri hivi karibuni kuna jamaa alikuwa dereva wa mgodi ndio katupea hii taarifa.
Mkuu, mishahara minono ni kuanzia pesa ngapi??
Jambo lingine nemegundua watu wengi hudanganyana sana kuhusu mishahara ya migodini kwamba ni mikubwa sana. Huu ni uongo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku za nyuma kulikuwa na tangazo la kazi kwenye kampuni inayojenga SGR kituo cha Dodoma.
Zipo njia nyingi za kupata kazi:-
1.Nenda ulipofanyia field omba kama volunteer uku ukiendelea kupata uzoefu wa kazi.
2.Nenda kwenye Garage hata za mtaani kwa kuanzia ili walau upate A,B,C..za namna ya kuanzisha Garage yako Siku za usoni.
3.Nenda kawaone mafundi wa Temesa ili upate uzoefu kwa upande karakana za Kiserikali.
4.Waone Mantrac/CAT hapo pugu road ili uanze kama mwanafunzi.
5.Tembelea Bodi ya usajili ya wahandisi ili ujisajili kama Graduate Engineer, then uingie kwenye SEAP program.
6.Unawaze kuwaona SIDO kwa ushauri au kusaidia kuandaa design mbalimbali/michoro e.t.c
 
Usimvunje moyo mwenzako.
GPA na kazi ni vitu viwili tofauti.
GPA kubwa umuhim wake labda Kama unataka ukawe mwalimu.
Kwenye manufacturing industries wanachohitaji ni practical works na wala hawataki theories zako ulizomeza kwenye vitini ili upate GPA kubwa.
Kakudanganya nani ww! Theory ni precursor ya practical , hujui theory , hujui practical!

Hii mambo ya kujaribu kudis connect theory na practical inatokea sana huku kwetu ambako engineer amabaye originally alipaswa kuwa designer na developer anaishia kuwa technician!
 
Kakudanganya nani ww! Theory ni precursor ya practical , hujui theory , hujui practical!

Hii mambo ya kujaribu kudis connect theory na practical inatokea sana huku kwetu ambako engineer amabaye originally alipaswa kuwa designer na developer anaishia kuwa technician!
Kumbe wewe unawaza Ulaya sisi tunaongelea nchini kwetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom