Nasumbuliwa na tumbo naombeni msahada wenu

THE ONETATUS

Member
Oct 2, 2012
29
9
Tumbo linanisumbua sana nilijarb kwenda hosp nikachukua vipimo nikahambiwa choo ndio kinasumbua nikapewa dawa hila dawa haijanisaidia chochote pia naweza nisipate aja kubwa kwa muda wa siku 4 hadi 5 na nikila muda kidogo njaa nisaidieni jamani
 
Mkuu.@THE ONETATUS Una Matatizo ya UKOSEFU WA KUTOPATA CHOO KIURAHISI : Soma tiba rahisi

UKOSEFU wa choo ni tatizo sugu miongoni mwa watu wengi. Bila kujua kuwa ni tatizo ambalo linahitaji tiba ya haraka, watu wengi hupuuzia na kuona siyo tatizo kubwa na ni hali ya kawaida. Ukosefu wa choo wa muda mrefu, huwa ndiyo chanzo cha magonjwa mengine hatari.

Mtu anapokosa choo kikubwa kwa siku kadhaa, uchafu hujikusanya tumboni na unapokosa sehemu ya kutokea hukimbilia kwenye damu na kuingia kwenye mfumo mzima wa damu. Uchafu huo unapoingia kwenye mfumo wa damu huwa sumu na chanzo cha maradhi mengine ambayo hujitokeza baadae na kuanza kumuathiri mtu, bila kujua chanzo chake.

Kwa kawaida mtu unapaswa kupata choo cha uhakika japo mara moja kwa siku, kutegemeana na mlo wake wa kila siku, unapokosa choo kwa siku nzima ili hali una kula milo yote kwa siku, elewa una tatizo katika mfumo wako wa kusaga chakula hivyo unapaswa kuchukua hatua haraka.

MTU MWENYE TATIZO HILI ANA DALILI GANI?
Mtu mwenye tatizo la ukosefu wa choo huwa na dalili kadhaa, ikiwemo kutumia nguvu na muda mwingi wakati wa kujisadia haja kubwa. Pili ulimi wake huwa na utandu mweupe na hutoa harufu mbaya mdomoni. Mtu huyu pia hukosa hamu ya chakula na wakati wote tumbo huwa limejaa.

NINI HUSABABISHA TATIZO?
Tatizo la ukosefu wa choo husababishwa zaidi na ulaji mbaya wa vyakula, kuacha kula matunda na mboga na staili mbaya ya maisha ikiwa ni pamoja na kutokunywa maji ya kutosha kwa siku.

NINI KIFANYIKE?
Ili kuondoa tatizo kabla halijawa sugu, fanya moja miongoni

mwa haya yafuatayo: Kunywa maji ya uvuguvugu asubuhi

mapema, kisha tembea tembea, baada ya muda utasikia haja

ya kwenda chooni. Ili usifanye haraka na upate muda wa

kutosha kujiandaa kwenda kazini, amka mapema zaidi. Kula

kiasi cha kutosha cha salad ya mboga mboga na juisi ya

matunda halisi asubuhi kabla ya kula chochote.

Kila siku kabla ya kwenda kulala, kunywa maji ya uvugu

yaliyochanganywa na kijiko kimoja cha asali. Kunywa maji ya

uvugu yaliyochanganywa na limau asubuhi na mapema kabla

hujala kitu chochote. Kunywa ‘castor Oil’ muda mfupi kabla ya

kwenda kulala. Ili kujiepusha kabisa na tatizo la ukosefu wa

choo, jenga mazoea ya kunywa maji mengi, kula mboga na

matunda kwa wingi kila siku na kuacha kabisa ulaji wa vyakula

vilivyoondolewa virutubisho kama vile mikate myeupe, ugali wa

unga mweupe, keki vyakula vyenye sukari nyingi na vyakula vingine vitamu.

Ninakushauri Nenda tena kamuone Dakatari.
 
Mkuu.@THE ONETATUS Una Matatizo ya UKOSEFU WA KUTOPATA CHOO KIURAHISI : Soma tiba rahisi

UKOSEFU wa choo ni tatizo sugu miongoni mwa watu wengi. Bila kujua kuwa ni tatizo ambalo linahitaji tiba ya haraka, watu wengi hupuuzia na kuona siyo tatizo kubwa na ni hali ya kawaida. Ukosefu wa choo wa muda mrefu, huwa ndiyo chanzo cha magonjwa mengine hatari.

Mtu anapokosa choo kikubwa kwa siku kadhaa, uchafu hujikusanya tumboni na unapokosa sehemu ya kutokea hukimbilia kwenye damu na kuingia kwenye mfumo mzima wa damu. Uchafu huo unapoingia kwenye mfumo wa damu huwa sumu na chanzo cha maradhi mengine ambayo hujitokeza baadae na kuanza kumuathiri mtu, bila kujua chanzo chake.

Kwa kawaida mtu unapaswa kupata choo cha uhakika japo mara moja kwa siku, kutegemeana na mlo wake wa kila siku, unapokosa choo kwa siku nzima ili hali una kula milo yote kwa siku, elewa una tatizo katika mfumo wako wa kusaga chakula hivyo unapaswa kuchukua hatua haraka.

MTU MWENYE TATIZO HILI ANA DALILI GANI?
Mtu mwenye tatizo la ukosefu wa choo huwa na dalili kadhaa, ikiwemo kutumia nguvu na muda mwingi wakati wa kujisadia haja kubwa. Pili ulimi wake huwa na utandu mweupe na hutoa harufu mbaya mdomoni. Mtu huyu pia hukosa hamu ya chakula na wakati wote tumbo huwa limejaa.

NINI HUSABABISHA TATIZO?
Tatizo la ukosefu wa choo husababishwa zaidi na ulaji mbaya wa vyakula, kuacha kula matunda na mboga na staili mbaya ya maisha ikiwa ni pamoja na kutokunywa maji ya kutosha kwa siku.

NINI KIFANYIKE?
Ili kuondoa tatizo kabla halijawa sugu, fanya moja miongoni

mwa haya yafuatayo: Kunywa maji ya uvuguvugu asubuhi

mapema, kisha tembea tembea, baada ya muda utasikia haja

ya kwenda chooni. Ili usifanye haraka na upate muda wa

kutosha kujiandaa kwenda kazini, amka mapema zaidi. Kula

kiasi cha kutosha cha salad ya mboga mboga na juisi ya

matunda halisi asubuhi kabla ya kula chochote.

Kila siku kabla ya kwenda kulala, kunywa maji ya uvugu

yaliyochanganywa na kijiko kimoja cha asali. Kunywa maji ya

uvugu yaliyochanganywa na limau asubuhi na mapema kabla

hujala kitu chochote. Kunywa ‘castor Oil' muda mfupi kabla ya

kwenda kulala. Ili kujiepusha kabisa na tatizo la ukosefu wa

choo, jenga mazoea ya kunywa maji mengi, kula mboga na

matunda kwa wingi kila siku na kuacha kabisa ulaji wa vyakula

vilivyoondolewa virutubisho kama vile mikate myeupe, ugali wa

unga mweupe, keki vyakula vyenye sukari nyingi na vyakula vingine vitamu.

Ninakushauri Nenda tena kamuone Dakatari.

nashhuru sana mkubwa ngoja kwanza niyafanyie kazi ulonambia ikishindikana niende tena kwa dactari.
 
Tumbo linanisumbua sana nilijarb kwenda hosp nikachukua vipimo nikahambiwa choo ndio kinasumbua nikapewa dawa hila dawa haijanisaidia chochote pia naweza nisipate aja kubwa kwa muda wa siku 4 hadi 5 na nikila muda kidogo njaa nisaidieni jamani

Dawa gani umepata ulipokwenda hospitali. Dawa unayohitaji ni edema. Huo ndio msahada unaohitaji.
 
Back
Top Bottom