Aise,mjanja kitambo exposure pia
Ova
Mrangi,
Vizazi vitatu vyote vimetumikia jeshi katika, "armed combat," yaani mapigano ya silaha.
Alianza Sykes Mbuwane aliyeingia Germany Ostafrika 1800 akitokea Mozambique akiwa askari mamluki chini ya Hermann Von Wissman kuja kupigana na Bushiri bin Salim Al Harith na Mtwa Mkwawa.
Akafuatia mwanae Kleist Abdallah Sykes aliyepigana WW I katika jeshi la Wajerumani dhidi ya Waingereza chini ya Von Letton Vorbeck 1914 - 1918.
Wakaja wajukuu Abdulwahid na Ally Kleist Sykes waliopigana WW II katika jeshi la Muingereza King's African Rifles (KAR) Burma Infantry (1939 - 1945) wakapigana dhidi ya Waingereza.
Baba yao ndiyo alihamasisha Waafrika na Waislam mjini Dar-es-Salaam kuwa na umoja wa chini ya African Association kwa ujumla wa wananchi na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika)kati ya 1929 na 1933.
Kleist alifanya biashara na wanae Abdul na Ally walifuata nyayo zake katika biashara na katika jumuia hizi zote mbili zilizoasisiwa na baba yao wakashika nafasi za uongozi wa kutumikia jamii.
Kleist Sykes ndiye alifungua mlango kwa Waafrika kuwapeleka watoto wao kuwasomesha nje ya mipaka ya Tanganyika ya kikoloni.
Kleist alimpeleka mwanae wa mwisho Abbas, King's College Budo, Uganda kusoma.
Abbas Sykes alisoma darasa moja na Fred Mutesa aliyekuja kuwa Rais wa Uganda na Kabaka wa Wabaganda.
Familia ya Sykes imeacha nyaraka muhimu sana zinazoeleza historia ya mji wa Dar-es-Salaam na yote yaliyopitika katika kukabiliana na ukoloni kuanzia 1900 hadi uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961.