Nashindwa nimjibu vipi dada yangu

Nashindwa nimjibu vipi dada yangu

Display Name

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2014
Posts
423
Reaction score
451
Jamani naombeni ushauri kwenye hili.

Mimi kwa sasa naishi nyumbani kwa dada yangu ambapo ameolewa na ana watoto wawili wa kwanza ana miaka 9 na mwingine 6. Dada yangu hakufunga ndoa na huyu mwanaume (kanisani wala msikitini). Walianza tu kuishi kuisha huko zamani na baada ya miezi michache dadangu akawa mjamzito(mtoto mwenye miaka 9) ndo ukawa mwanzo wa maishi yao ya pamoja mpaka leo.

Sasa shida ipo hapa, huyu shemeji akawa na tabia za kuchepuka chepuka, watu walianza kusema wa hapo mahali tunapoishi kwa upande wangu nikawa siamini kabisa maneno yao hadi mambo yakawa mambo(kiasi kwamba hadi dadangu akawa anajua kuwa shem huyo anamcheat). Wakati mwingine hao wasichana wakawa wanampigia simu dadangu na mtukana maneno makali na kumwambia awapishe hapo nyumbani wenyewe waje waolewe(coz dadangu hajaolewa kiimani).

Hayo maneno aliyokuwa akitukanwa dadangu na hao wasichana yalikua hayamshughulishi shem wangu kwani hata hivo alionyesha wazi kuwa anachepuka na wala alikua haogopi na hakuwa anasikiliza ushuri wa mtu. Vikao vilifanyanywa vikihishisha ndugu zetu na ndugu wa mwanaume lakini haikusaidia. Haya yote wakati yanatokea dadangu alikua tayari ana watoto wawili na yalikua yakiendelea kwa mda wa miaka isopungua mitano. Muda wote huo tukawa tunamshauri(dadangu) afanye utaratibu wa kuachana na huyu mwanaume but yeye alitoa sababu nyingi za kuendelea kubaki pale hiyo hakuondoka.

Mimi nilikua nasoma chuo flani hivo nilikua wakati mwingine narudi hapo home kusalimia ila kutokana na hiyo nyumba kuwa haina amani wakati mwingine nilikua natamani hata nisiende pale ila nikawa naenda sababu nampenda sana dadangu na wale watoto afu nikwa namwonea huruma mno kwamba atakua mpweke, coz hapakua mbali sana na chuo wakati mwingine nilikaa hapo weekend na hata week days nikawa natokea hapo kwenda chuo.

Nilikua na rafiki yangu tunasoma pamoja ambaye kwao yeye ni mkoa mwingine so nikawa napenda kumualika anakuja nyumbani hapo siku za jumapili au jumamosi tunashinda pamoja hapo nyumbani afu anarudi hostel. Huyu rafikiangu akaanza mahusiano na shem wangu, mimi nikaja kujua kama baada ya mwezi hivi, niliambiwa na rafiki yangu mwingine. Nilipomwuliza akakubali, sikuwa na cha kumfanya zaidi nilimwambia nilivyoumizwa na kitende hicho na hata hivo hatukuweza kuendelea na urafiki. Dadangu alishangaa ana aliniuliza kwani haji tena nyumbani nkasema amepata marafiki wengine hua anaenda huko. sikumwambia dadangu yaliyotokea coz angeumia sana afu mi nilikua najilaumu coz mi ndo nimemtambulisha yule dada hapo nyumbani(hiyo ilikua mwaka jana km wa 7). Tukamaliza chuo kila mtu akaende upande wake.

Juzi dadangu amepata habari kwa mtu ambaye alifahamu kuwa shem alitembea na yule rafiki angu , alafu huyo mtu akamwambia kuwa hata mdogo wako anafahamu(yani mimi), dadangu alisikia uchungu sana na aliita(maana nilikua nimeenda kumsalimia mama mkubwa), nilipokuja nyumbani nilimkuta dadangu amelia kiasi kwamba hadi macho yamevimba, akaniuliza kama shem alitembea na yule dada na kama mi niliua najua. Kiukweli nilistuka kuona amepata hizo habari afu nguvu ikanijia nikakataa katakata kuwa sifahamu wala sijasikia coz alikua ananilaumu kwa nini sikumwambia. Nilikataa hadi nikalia coz wakati nakataa lakini roho ilikua inaniuma mno kuwa namdanganya zaidi na zaidi.

Leo nimeamka roho inanituma nimwambie ukweli but naogopa kuanzisha hiyo mada hivo sina raha mie mwenzenu, napata maumivu makali nikimwona shem na zaidi napata maumivu makali nikimwangalia dadangu mana kuna watu wanasema hadi leo rafikiangu na huyu shem wanaendelea na uhusiano.

NAOMBENI USHAURI WENU NIFANYEJE. NIMWAMBIE DADA ILI NIPATE AMANI AU NIBAKIE HIVI HIVI HUKU NAJUA UKWELI NA PIA WATU WANASEMA BADO WANAUHUSIANO?

Nifanyeje jamani, naombeni msaada wenu.
 
Mweleze tu ukweli na kwamba ulikuwa unaogopa ataumia sana na Mungu atakusaidia ili muwe na amani na dada yako."..

.....tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote.........."
 
Mwambie tu dada yako. Mwambie nilijisikia vibaya endapo ukijua na nikampiga marufuku kufika hapa nyumbani tena huyo rafiki yangu kwa mambo ya ajabu aliyofanya ndo maana umuoni tena. Atakusamehe.:thinking:
 
Duh jamani inasikitisha

mie nimewmelewa dada ako sia analia kwa nini hujamwambia
ni analia matendo ya huyo mumewe yanamuumiza talk to her
mwambie situation ilivyokuwa na kwanini ulifanya ulivyofanya

Mwambie dada yako aachane na huyo mwanaume sio mtu ni shetani.

Mweleze tu ukweli na kwamba ulikuwa unaogopa ataumia sana na Mungu atakusaidia ili muwe na amani na dada yako."..

.....tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote.........."

^^
Aisee kuna binadamu wanajua kupenda!
Pole kwa moyo wa hatia mleta mada.
^^


Mwambie tu dada yako. Mwambie nilijisikia vibaya endapo ukijua na nikampiga marufuku kufika hapa nyumbani tena huyo rafiki yangu kwa mambo ya ajabu aliyofanya ndo maana umuoni tena. Atakusamehe.:thinking:

Asanteni kwa ushauri ndugu zangu,,, naomba msiache kuniombea kwa Mungu anitie nguvu.
 
Mwambie ukweli lakini siku nyingine jambo la uongo usitoe machozi umeonesha unafiki wa hali ya juu kiasi cha ata utakapomwambia atapata shida aamini lipo lile la kulia kuwa hufaham au hili la sasahivi kuwa unafaham, ni Vema ungemkatalia lakini usingetoa machozi ungeacha yeye alie leo hii ingekuwa rahisi kumwambia na akakuelewa zaidi, siku nyingine ZUIA machozi ya uwongo, all in all mwambie dada ukweli na huyo shemeji kwanini hakwenda na Malaysian airline tena peke yake tu wa pili pilot sababu shemeji yako hawezi kurusha ndege
 
Mwambie ukweli lakini siku nyingine jambo la uongo usitoe machozi umeonesha unafiki wa hali ya juu kiasi cha ata utakapomwambia atapata shida aamini lipo lile la kulia kuwa hufaham au hili la sasahivi kuwa unafaham, ni Vema ungemkatalia lakini usingetoa machozi ungeacha yeye alie leo hii ingekuwa rahisi kumwambia na akakuelewa zaidi, siku nyingine ZUIA machozi ya uwongo, all in all mwambie dada ukweli na huyo shemeji kwanini hakwenda na Malaysian airline tena peke yake tu wa pili pilot sababu shemeji yako hawezi kurusha ndege

Nililia kwa sababu alikua aniuliza kitu ambacho nilikua nafahamu ukweli afu sikua tayari kumwambia so nilikua naumia sana sana kuona kwamba nashindwa kumwambia ukweli ndio maana machozi yalimitoka.

Asante kwa ushauri pia.
 
Pole, pole pia kwa dada. Yani ndoa zina mambo kwa kweli, ongea na dada mfariji, mwambie kuanza upya sio ujinga.
 
Mmmmmmh! Kweli kuna majanga ulimwengu huu jamani.
Watu wengine wanawatesa watoto wa wazazi wengine kama nini jamani.
 
pole dadangu...utakapokuwa tayari mwambie...
 
Duh jamani inasikitisha

mie nimewmelewa dada ako sia analia kwa nini hujamwambia
ni analia matendo ya huyo mumewe yanamuumiza talk to her
mwambie situation ilivyokuwa na kwanini ulifanya ulivyofanya

Yaani Heaven on Earth kuna Mambo yanasikitisha sana!
Sipati picha hali anayopitia huyo dada ukizingatia jamaa ameshazaa naye watoto wawili!
 
Last edited by a moderator:
ulimjua kabisa shemejio samaki hapishi chambo halafu unapeleka mashoga zako kwake?anyway mpe pole dadayako na wewe kuwa mkweli mana ukweli utakuweka huru. sipati picha najua shost wangu anamvurugia ndoa dadayangu!!eti nimfichie siri shosti!NEVER! ningehakikisha shosti anaachana na shen
 
Mwambie dada yako aachane na huyo mwanaume sio mtu ni shetani.

sawa lakini mapenzi hayaingiliwi lakini vipi akimwambia then kesho amwone dada yake kafikishwa kunako si atamuona mdogo wake mbaya?
 
kuna story nyingine mtu anaandika angalau unaona kuna ukweli na anahitaji msaada. kusema ukweli siku zote sio kuwa mkweli! wakati mwingine uongo huepusha mambo mengi kuliko kusema ukweli. Ibrahimu alipokwenda Misri alimwambia mke wake kuwa wakikuuliza kuwa wewe ni mke wangu kata sema wewe ni dada yangu. alifanya hivyo akijua akisema ni mke wake falao atamuua na kumchukua mke wake. ninachokushauri wewe kaa kimya hadi kufa na unaweza ona jinsi ambavyo dada yako ameumia kwa jambo hilo hivyo ukimwambia utaongeza balaa. mimi najua ulifanya hivyo kwa maana nzuri tu ili usilete mfarakano katika ndoa ya dadako. kuachana ndio jibu lakini li katika uwezo wa dadako na si mtu mwingineyo.
 
Duh jamani inasikitisha

mie nimewmelewa dada ako sia analia kwa nini hujamwambia
ni analia matendo ya huyo mumewe yanamuumiza talk to her
mwambie situation ilivyokuwa na kwanini ulifanya ulivyofanya
sioni sababu ya kumwambia kwani dada yake anaonyesha pale kafika kwa kuwa alishakataa aonyeshe msimamo wake kesho atasikia na yeye anatembea na shemeji yake akiulizwa atakataa lkn dada yake atamini tu kama hivi alivyoamini.
 
Back
Top Bottom