Mimi ni kijana wa miaka 27. katika michakato ya kimaisha nilijiwekea utaratibu kua sitaoa mwanamke ambae ana mtoto kwa sabaabu zangu mwenyewe tu (sio logic sana).
Mwaka 2009 nilikutana na msichana mmoja ambae nilimpenda sana lakini huyo msichana alizaa mtoto wa kiume tangu 2004 na mimi nililifahamu hilo. Kwa wakati huo sikua tayari kuoa na sikutaka kufanya maamuzi ya kumchagua mwanamke wa kuishi nae ila mwili una mahitaji na matamanio yake, hayo matamanio yakanisukuma kutengeneza ukaribu na huyo binti nayeye akaingia kwenye line. siku ilipofika nikamwita nikamwambia kua nampenda ila habari ya ndoa sio warrant, yule binti alikubali kwa shingo upande tukaingia kwenye mahusiano japo changamoto zimekuwepo lakini tumeweza kumaintain.
Sasa muda wangu wa kuoa umefika na bado I can see the lady is beutiful, ni msichana anaenijali na kunisupport lakini ninashindwa kumwoa eti kwa sababu ya mtoto wake. Kwa kweli tatizo kubwa ninaloliona mimi ni hilo la mtoto. Yeye mwenyewe alishaniambia kua hana kipingamizi kuhusu kuoa kwangu endapo nitaoa mwanamke mwingine yuko tayari au km nikimtaka yeye mwenyewe yuko tayari ila anasema km nikioa mwanamke mwingine bado uhusiano wetu utaendelea japo kimya kimya
Sasa ndugu zangu nimeleta mada hii kwenu mnisaidie kwa kunipa ushauri ni jambo lipi la kufanya.
Tafadhali ushauri wako ni muhimu
Asante
Mwaka 2009 nilikutana na msichana mmoja ambae nilimpenda sana lakini huyo msichana alizaa mtoto wa kiume tangu 2004 na mimi nililifahamu hilo. Kwa wakati huo sikua tayari kuoa na sikutaka kufanya maamuzi ya kumchagua mwanamke wa kuishi nae ila mwili una mahitaji na matamanio yake, hayo matamanio yakanisukuma kutengeneza ukaribu na huyo binti nayeye akaingia kwenye line. siku ilipofika nikamwita nikamwambia kua nampenda ila habari ya ndoa sio warrant, yule binti alikubali kwa shingo upande tukaingia kwenye mahusiano japo changamoto zimekuwepo lakini tumeweza kumaintain.
Sasa muda wangu wa kuoa umefika na bado I can see the lady is beutiful, ni msichana anaenijali na kunisupport lakini ninashindwa kumwoa eti kwa sababu ya mtoto wake. Kwa kweli tatizo kubwa ninaloliona mimi ni hilo la mtoto. Yeye mwenyewe alishaniambia kua hana kipingamizi kuhusu kuoa kwangu endapo nitaoa mwanamke mwingine yuko tayari au km nikimtaka yeye mwenyewe yuko tayari ila anasema km nikioa mwanamke mwingine bado uhusiano wetu utaendelea japo kimya kimya
Sasa ndugu zangu nimeleta mada hii kwenu mnisaidie kwa kunipa ushauri ni jambo lipi la kufanya.
Tafadhali ushauri wako ni muhimu
Asante