Nashindwa kumwelewa Mwamposa kwa kauli yake ya kutaka Serikali ichuje maudhui ya Mitandao ya kijamii

Nashindwa kumwelewa Mwamposa kwa kauli yake ya kutaka Serikali ichuje maudhui ya Mitandao ya kijamii

Mr Why

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2019
Posts
2,992
Reaction score
5,660
Bado nashindwa kumwelewa Mwamposa kwa kauli yake ya kutaka Serikali ichuje maudhui ya Mitandao ya kijamii

Ni kazi gani hii ambayo haijawahi kuonekana tangu dunia iumbwe? Unawezaje kuchuja maudhui yote yanayochapishwa mitandaoni?

Ni binadamu wa aina gani ambao hawajawahi kuonekana duniani watakaokuwa na uwezo wa kusoma maudhui yote yanayochapishwa Facebook au Instagram na kuchagua yale mazuri tu huku mabaya yakifutwa?

Kampuni ya META ina mfumo wa algorithm wa kukagau maudhui lakini hauwezi kusoma maudhui yote unategemea kupokea report pia

Bajeti ya kuweka teknolojia ya algorithm ndani ya bidhaa za META haikuwa chini ya trilioni 100 lakini uwezo wa algorithm ya kuchuja maudhui ukomo wake ndiyo huo

Anachokitafuta Mwamposa ni kipi kama sio kuendelea kusababishia matatizo kampuni za mitandao ya kijamii mfano JF, META, X Corp na wengineyo?

Sijapata kujua ni mtu wa aina gani asiyeweza hata kuheshimu uwekezaji wa kampuni za mitandao ya kijamii

Mitandao ya kijamii inaendeshwa kwa mamilioni ya fedha na sio bure. Kuweka mtandao hewani kwa mwezi ni mamilioni ya fedha na usipoyalipa basi mtandao wako unakua off

Kauli kama hizi ndizo zilizoipelekea JF kupitia matatizo makubwa miaka ya nyuma zinafaa kukemewa kwa nguvu zote.

Soma Pia: Mwamposa ataka Mitandao ya Kijamii idhibitiwe. Adai inafanya watu kuwa wavivu

Jambo linalonisikitisha ni namna JF wanavyoteseka kuhariri maudhui hii ni kazi kubwa sijapata kuona na huwa nawaonea sana huruma, META nao wanateseka tangu zamani kwa kulipishwa fines kila mara

Miaka ya nyuma walitokea viongozi wapuuzi wakaanza kushambulia mitandao ya kijamii ikapeleka matatizo makubwa sana kama mitandao kufungiwa huduma na utitiri wa kesi Mahakamani. Fikiria mwanzilishi wa mtandao aliwekeza kiasi gani cha fedha kuuweka mtandao hewani, ni bills za million ngapi analipa kila mwezi ili uwe hewani?

Leo mtu anatoka huko anaanza kutapika ujinga. Badala ya kuishauri Serikali ipambane na wavunja Sheria za mitandao anaharibu mtandao mzima kana kwamba watumiaji wote mitandaoni wanafanya upuuzi. Wafanyabiashara wangapi wanatumia mitandao kuuza bidhaa zao je ni Wananchi wangapi wanapata huduma zao mitandaoni? Stupid mind

Alihangaika X ifungiwe wakati algorithm ya X inakuletea maudhui uliyoyachagua wewe, ni nani anayependelea kufuatilia maudhui ya michezo akaletewa picha za uchi? Picha za uchi zinakuja pale mtumiaji anapokuwa na tabia ya kuzitafuta.

Ni Trillion ngapi Elon Musk amewekeza X leo unaanza kuharibu uwekezaji wake kwasababu ya watumiaji wachache wanaofuatilia mambo ya hovyo.

Je ni mamilioni mangapi ya watumiaji wanafanya biashara katika mtandao huo? Kwahiyo mtandao mzima ufungwe kwasababu ya watumiaji wachache wanaofuatilia mambo ya hovyo? Je hawa wanaofanya mambo ya maana haki yao unaipeleka wapi?

Unahukumuje watu wote kwasababu ya makosa ya watu wachache?

 
Atakuwa ametumwa na viongozi wake ili wapime upepo.
Nadhani hiyo ndiyo maana, kauli za kipuuzi kabisa, unawezaje kuchuja maudhui yote ya Facebook nonsense and stupid mind
 
Bado nashindwa kumwelewa Mwamposa kwa kauli yake ya kutaka Serikali ichuje maudhui ya Mitandao ya kijamii

Ni kazi gani hii ambayo haijawahi kuonekana tangu dunia iumbwe? Unawezaje kuchuja maudhui yote yanayochapishwa mitandaoni?
Sijawahi kumuelewa
 
Kauli gani mkuu
Miaka ya nyuma walitokea viongozi wapuuzi wakaanza kushambulia mitandao ya kijamii ikapeleka CEO wa JF kupata matatizo makubwa sana kama kufungiwa huduma na utitiri wa kesi Mahakamani. Fikiria mwanzilishi wa mtandao aliwekeza kiasi gani cha fedha kuuweka mtandao hewani, ni bills za million ngapi analipa kila mwezi ili uwe hewani? Leo mtu anatoka huko anaanza kutapika ujinga. Badala ya kuishauri Serikali ipambane na wavunja Sheria za mitandao anaharibu mtandao mzima kana kwamba watumiaji wote mitandaoni wanafanya upuuzi. Wafanyabiashara wangapi wanatumia mitandao kuuza bidhaa zao je ni Wananchi wangapi wanapata huduma zao mitandaoni? Stupid mind
 
Huyu ni mjinga, huwezi kusoma maudhui yote ya Facebook au Instagram na ukayachuja yote. Jinga kabisa. Mara ngapi META imekuwa ikiwekeza trillion za fedha kuboresha algorithm
Bora aongeage kuhusu biblia tu👿 kuepuka aibu ndogondogo kama hizi!!
 
Miaka ya nyuma walitokea viongozi wapuuzi wakaanza kushambulia mitandao ya kijamii ikapeleka CEO wa JF kupata matatizo makubwa sana kama kufungiwa huduma na utitiri wa kesi Mahakamani. Fikiria mwanzilishi wa mtandao aliwekeza kiasi gani cha fedha kuuweka mtandao hewani, ni bills za million ngapi analipa kila mwezi ili uwe hewani? Leo mtu anatoka huko anaanza kutapika ujinga. Badala ya kuishauri Serikali ipambane na wavunja Sheria za mitandao anaharibu mtandao mzima kana kwamba watumiaji wote mitandaoni wanafanya upuuzi. Wafanyabiashara wangapi wanatumia mitandao kuuza bidhaa zao je ni Wananchi wangapi wanapata huduma zao mitandaoni? Stupid mind
Exactly 💯 mkuu hii ndio imefanya hadi yule mmiliki wa telegram anateseka sana huwa najisikia vibaya mno napoona pale wamiliki wa mtandao wakipata matatizo kama haya yule mchungaji hajui kitu aisee
 
Serikali yenyewe Ina matatizo chungu mzima ya kuyatatua, umaskini umezidi kukithiri, alafu anatokea mjinga mmoja badala ya kuishauri serikali kutatua changamoto zinazolikumba taifa anaanza kuishauri ikague nini watu Wana post Mtandaoni, huyu mtu ni wa kupuuzwa na kukemewa Kwa nguvu zote
 
Back
Top Bottom