Nashindwa kuelewa utajiri wa Software developers

Ili kupata jawabu la swali lako unatakiwa ujiulize kwanini....unalazimika kununua kifurushi cha intaneti ili wewe uweze kuperuzi kwenye hiyo mitandao.....??!!!

Ukishajua sababu ya wewe kulipia hiyo huduma ya mtandao ndio....alafu ujiulize ni watu wangapii wanafungua hyo mitandao kwa siku moja na kwa pesa.....
Hapo ndipo utakapopata kujua kuwa hao jamaa wanapataje utajiri kwa wewe kuchungulia kwenye mitandao yao.....!!!??
 
sababu kubwa ni kwamba software inawafikia watu wengi zaidi.

chukulia mfano app za google na Htc 10.
-htc akiuza simu 1 inamfikia mtu mmoja analipa mara moja mumemalizana akiuza sana ni simu milioni 1 na kila simu dola 600 mwisho wa siku ana mapato dola milioni 600
-app ya google inakuja na simu ya android zinauzika simu kama bilioni moja kwa mwaka, nenda playstore utaona app za google nyingi zimedownloadiwa zaidi ya mara bilioni 1 akiwa na app 20 na akipata kila app dola 1 tu basi ana dola bilioni 20 kwa mwaka. ili apate dola 1 kwa mwaka anahitaji umuingizie shilingi 6 tu kwa siku, hivyo ukiclick tangazo moja akapata shilingi 20 ujue hapo tayari umempa hela nyngi sanaa.

kuhusu bill gate yule jamaa mapato yake si microsoft tu ana hisa hadi cocacola na makampuni kibao. zaidi ya nusu ya utajiri wa bill gates hautokani na microsoft soma zaidi hii kampuni yake ya uwekezaji
Cascade Investment - Wikipedia, the free encyclopedia
 
Umefafanua vizuri sana
 
Suala ni kwamba, mwanzilishi/mmiliki wa Facebook, Mark Zukerberg, kuwa tajiri zaidi ya mmiliki/mwanzilishi wa Toyota haina maana kwamba Facebook ina thamani kubwa (au inaingiza pesa nyingi) zaidi ya Toyota.

Fikiria hii: Mwanzilishi na rais wa kampuni ya Huawei Technologies Co., Ltd., Ren Zhengfei, anamiliki chini ya 2% ya Huawei Technologies Co., Ltd.

Kwa hiyo inawezekana Toyota inaingiza pesa nyingi zaidi ya Facebook, ila ukija kwenye utajiri wa waanzilishi/wamiliki wake ikawa tofauti kutegemea na hao waanzilishi/wamiliki wanamiliki asilimia ngapi ya mapato ya kampuni zao.

Nadhani nitakuwa nimekujibu swali lako.
 
Alafu dukani wanatuambia ina "windows ya bure" daaah!!!
 
utajiri wa hawa jamaa kwa kiasi kikubwa sana ni matangazo.
huko ulaya wanauza mbaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…