Nashindwa kuchagua....!

Nashindwa kuchagua....!

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,393
Habari waungwana,
Nimeanza kazi moro nina kam miezi 9 na nimeanzisha uhusiano na binti mmoja alie jaaliwa uzuri miezi 3 iliyopita. Yeye yupo UDSM mwaka wa 2. Kwa bahati nimeamishiwa kikazi DSM. Mimi ni mpenzi sana wa mpira na analijua hili. Kutokana na kazi siku za kawaida nipo bize sana na yeye bize na masomo, weekend nipo free na yeye pia
Tatizo: Huwa anakuja kunitembelea weekend jioni muda ambao mechi nyingi zinachezwa na mimi bila kucheki mpira nakosa raha kabisa na anafahamu. Muda mwingine mechi zikianza jioni ni mpaka usiku, na nikisema nisiende kuangalia mpira nikae nae muda mwingi nacheki update za matokeo ya mechi kwenye simu. Hali hii imekuwa ikimkera na kukasirika mpaka imefikia hatua ameniambia nichague moja yeye ama mpira. wote wanakamilisha furaha yangu.sijui chafanya hadi sasa
msaada waungwana
 
Jichange fasta funga Smart Tv geto plus DSTV premium package,,, 129,000 kwa mwezi si haba kwa mtu mwenye mapenzi ya mpira kutoka moyoni... Ili uangalie mpira home ukiwa naye maana bar kuna matusi na mabishano yasiyo na maana kuenda na your loved ones haipendezi...

Duh lakini kaka umetisha mi mwenyewe mpenzi wa Soka but when it comes to Sweetheart Soka linanisamehe kidogo...

Wanawake wa kizazi hichi kazi mnayo yaani Dume linapenda Manchester kuliko Wife..
 
uwwiiiiiiiiiii jamani pangilia ratiba zako ili naye apate nafasi ya kuinjoy na wewe
 
Da hapo ni pagumu inabidi ufanye maamuzi magumu wewe mwenyewe iwe ni mpira au yeye
 
Jichange fasta funga Smart Tv geto plus DSTV premium package,,, 129,000 kwa mwezi si haba kwa mtu mwenye mapenzi ya mpira kutoka moyoni... Ili uangalie mpira home ukiwa naye maana bar kuna matusi na mabishano yasiyo na maana kuenda na your loved ones haipendezi...

Duh lakini kaka umetisha mi mwenyewe mpenzi wa Soka but when it comes to Sweetheart Soka linanisamehe kidogo...

Wanawake wa kizazi hichi kazi mnayo yaani Dume linapenda Manchester kuliko Wife..

thanx bro nimekusoma ngoja nizichange
 
Utoto una mateso lakini? Afu shida nyingi za kujitakia
Piga chini wote ubaki alone
 
Bado hujapenda....lazima uwe na ratiba ya rafiki, mpenzi, mpira na etc. Huwezi gonganisha kila kitu @ same time, utaachwa, maana hauonyeshi kujali, hizo mechi usipoangalia unapungua nini.....
 
Hahahah! Hivi utakufa ukikosa updates za mpira? Ukishaoa na kuwa baba kwenye familia yako utakuwa unashinda unaangalia mpira kuliko kutumia muda wako kujenga familia yako. Hujakomaa. You need to grow up. Utapigwa chini unashabikia Ronaldo who doesn't even know you exist.
 
Bado hujapenda....lazima uwe na ratiba ya rafiki, mpenzi, mpira na etc. Huwezi gonganisha kila kitu @ same time, utaachwa, maana hauonyeshi kujali, hizo mechi usipoangalia unapungua nini.....

nampenda sana 2,nikimwambia aje anasema asbh ana discusion, assgmnt zakufanya
 
Hahahah! Hivi utakufa ukikosa updates za mpira? Ukishaoa na kuwa baba kwenye familia yako utakuwa unashinda unaangalia mpira kuliko kutumia muda wako kujenga familia yako. Hujakomaa. You need to grow up. Utapigwa chini unashabikia Ronaldo who doesn't even know you exist.

ukishakuwa kwenye ndoa majukumu ni tofauti na sasa, alaf najua ninachokifanya,nimekueleza situation we unanihukumu.
 
Dating ni preparation ya ndoa. Yaani ni kama test ya kuona priorities zako ziko wapi. Kama muda wa kuonana ni weekend tu halafu wewe unataka kuangalia mpira tu, utalalamika akikubwaga?

Sijakuhukumu, nilitaka tu ufungue macho yako na ujaribu kuona mbali. Mpira unaouangalia jumamosi, by jumatatu umeshausahau unakumbuka highlights tu. Ukiukosa kwani utaisha? Mechi zingine hazitachezwa?

ukishakuwa kwenye ndoa majukumu ni tofauti na sasa, alaf najua ninachokifanya,nimekueleza situation we unanihukumu.
 
Back
Top Bottom