Nashauri waziri Magufuli ashtakiwe

Watz tuwe tunashirikisha bongo zetu vizuri. Tunatakiwa kuhoji ni sababu gani zilizopelekea serikali kufuta kesi kwa hati ya nole. Iweje after years leo isiwe na interest ya kuendelea na kesi? Hapo ndio kuna suala la msingi la kuhoji na kupatiwa majibu kutoka ofisi ya DPP.
Sasa badala ya kuangalia hayo watu mnakurupuka na kutaka Magufuli ashtakiwe! Ashtakiwe kwa kosa gani?! Embu tuwe wachunguzi wa vijimambo kidogo badala ya kukurupuka tuu kuandika
 
Seriously huyo hakimu/jaji aliyetoa uamuzi huo anapaswa kunyongwa
 

Naomba tukumbushane, Magufuli kipindi akiwa Waiziri wa Ujenzi mwaka 2000 - 2005 alibomoa kituo cha mafuta kule Mwanza na Serikali ilisimamia vizuri kabisa kesi hiyo, Magufuli alipotaka tu Serikali ikashindwa kesi hata kituo hicho cha mafuta pamoja na kushinda kesi kilipotakwa kujengwa tena walizuiwa kuwa mahala hapo haparuhusiwi kama yalivyo madai ya msingi ya Serikali , na ni ukweli usiopingika mpaka leo sehemu hiyo ipo wazi.

Mwaka 2009 serikali ikakamata Wavuvi haramu Serikali ikashinda kesi ya msingi, Magufuli katoka pale kibao kimegeuka.

Sasa nikuulize wewe ni mtoto mdogo, fanya simple research angalia Serikali inavyohujumiwa kesi zake na mawakili wake wabovu na hasa pale viongozi wazalendo wanapoondoka ktk kusimamia ile haki.

Ofisi ya mwanasheria mkuu ni majanga majanga!!!!
 

We jamaa unapenda sana kuandika habari huku ukiwa na mihemko.
 
Sheria ipo,ila mawakili wapo ili wajenge hoja kwenye shitaka husika ili mteja wao ashinde kesi ila kibaya zaidi nikuwa Rushwa iliyopo mahakamani ndo tatizo kubwa la nchi hii!Ingekuwa kwa watu wanaotii serikali iliyowapa mamlaka wangekuwa wanafanya kazi kwa kufata misingi ya sheria!
 
Malisa Ndugu YANGU,tukifika mahala tukawa mashabiki wa SIASA kwa KILA jambo Kama taifa basi tutakuwa tumeharibikiwa sana Kama sii kupotea,kwamba Kitendo cha waziri kuongoza Doria wakakamata MELI iliyokuwa ikifanya shughuli ZAKE ukanda wetu wa bahari kimakosa ionekane ni jinai??what a shame,Yaani Magufuri kakosea wapi,je,tunabariki uvuvi haramu bahari kuu??kwamba huko baharini libaki shamba la bibi,MELI za mataifa mengine zije zivune samaki na kuondoka?? Ni mwaka Juzi tu,mahakama ilitoa ushindi kwa serikali dhidhi ya MELI hiyo,sasa Kama kuna kushindwa tena KATIKA rufaa,sioni mantiki ya ku-brand Eti MELI ya Magufuri ,samaki wa Magufuri ,KESI ya Magufuri hata Kama Big name ndo hu-make news,nayaona magazeti yanalichukulia jambo Hilo zaidi na Politiks na hasa SIASA za URAIS jambo ambalo sioni TIJA yake,kwamba Leo akikamatwa mtu na dawa za kulevya,kesho akashinda KESI,basi sisi wananchi tunmpongeza muuza dawa za kulevya Kisa KASHINDA KESI,maana hata hayo mataifa wanayotoka hao wenye MELI ,wanaposoma habari za KESI Yao kwa magazeti ya Tanzania WATAKUWA wanatucheka sana Kama sii kutudharau,jinsi tunavyowashangilia Wao kwa ushindi,naamini nchini KWAO hata Kama ni utofauti wa kisiasa ni MGUMU wakuunge MKONO KWENYE jambo LENYE maslahi ya taifa Lao.
 
Msichokijua ni kuwa Taifa hili la Tanzania halijawahi kuingia hasara............

Ni mipango na mbinu mbinu tu..
 
Uongozi wa sasa wa Sirikali ya Tanzania unastahili kuingizwa kwenye maajabu ya Dunia;
(a) Waziri Mwanasiasa kakamata wavuvi haramu, hapa tunafahamu kila Wizara kuna Wanasheria je walimshauri vibaya?
(b) Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambayo ina wajibu wa kuishauri Serikali nayo ili jishauri kinyeji sio Kisheria?
(c) Ofisi ya Mwendesha Mashatka ya Jinai wa Tanzania nayo ili shauriwa vibaya?
(d) Mawakili wa Serikali walio andaa Hati ya/za Mashtaka nao ni mbumbubu wa Sheria?
(e) Wezi wa Samaki wanashinda Kesi kwa " Nolle prosequi" nchi inapata hasara ya Mabilioni/Matrilion RAHISI ana mpa zawadi DPP kwa kazi nzuri ya kushindwa Kesi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu?
(f) Sina uhakika kama Katiba Mpya tarajiwa ina IBARA ambazo zinatupa wananchi mamlaka kufukuza Kazi na kuwashtaki Viongozi Wezi, Wababaishaji, Wahuni, Mafisadi na wachumia tumbo?
(g) Huu WIZI, USHENZI NA UPUUZI ufikie mwisho ili wanaofanya haya mambo walipe wenyewe. Ebooooo nyambafu woote mlio husika katika mchongo wa kijinga kiasi hiki
 
Sensitive issue hapa ni hasara kwa taifa kulipa bilion 27. kwa hivi ni lazima serikali nzima na watanzainia wajihoji chanzo cha hasara hii ni nini. mtoa mada kaona kuwa Magufuli anahusika na wengine wanasema mahakama ina tatizo. kama ni hivo je, tuyaache hivi hivi? Hoja ina mshiko mkubwa sana. mimi naona kwa wahusika wote walzubaa tangu siku ya kwanza kwa kumshabikia mtu mmoja! Ilitakiwa ushauri utoke pale pale kupitia ofisi ya mwanasheria mkuu na watanzania weledi wa sheria. kwa hivo ingawa Magufuli alikaa mbele wakubwa walikuwa na nafasi ya kusema neno kama wakati fulani alipopigwa stop ya bomoa bomoa. hitimisho ni kuwa serikali inahusika naa hasara hii na kwa kweli ni fedheha!
 
Hiyo ndiyo mantiki kwa ujumla mahakama yote imeoza kwa rushwa ni bure kabisa.

Mahakama iko chini ya serikali inayoongozwa na nani?

Ile taasisi ya kupamba rushwa nayo inafanya nn?

Nyangau wakubwa
 
Mnapoenda mahakaman haina maana yule uliempeleka ndio akasilibwe kesi tu, kuna matokeo mawili na yana faida na hasara zake

wachina wameshinda, walipwe ni haki yao na lait kama Wangeachwa wavue tu bila kukamatwa leo mngepiga kelele tena
 
Kama Waziri alifanya maamuzi kutokana na washauri wa hayo maswala then anaweza akapima na kuamua kujiuzulu, upande mwingine hao waliomshauri Waziri, then wanatakiwa watoe maelezo....Bilion 27 kama ndo pesa ya kulipa ni nyingi mno na hailipi CCM, bali watanzania....so lazima Serikali ya CCM itoe ufafanuzi na kuwajibisha wahusika...
 
Hebu weka jina media hizo kama natujakutana na Tanzania Daima au Nipashe
Wewe pimbi ulichoandika hapo nilipobold ndo nini?Ila kwa taarifa yako soma pia mwanachi,wewe badala ya kuchangia hoja kwa point unakuja na makinyesi yako hapa.Nchi inazidi kufilisika,umaskini ukija kwa kasi na maradhi yanayosababishwa na CCM na nyie vibaraka wake ww unaleta mchezo!Nyambaf
 

Mkuu hapo nilipokoleza hiyo ofisi haina kitu kwani likubwa lenyewe ndo lile linatishia kuwapiga watu na kuwachinja kila linapozidiwa na hoja kama ilivyotokea majuzi huko Dom!
 
Jamani mbona mimi cku sio nyingi nilisoma habari kwamba tz imeshinda kesi inalipwa fidia ya sh billioni sita na kumiliki ile meli ya kichina??? Ss vipi kesi imerudiwa?......
 
Mkuu hapo nilipokoleza hiyo ofisi haina kitu kwani likubwa lenyewe ndo lile linatishia kuwapiga watu na kuwachinja kila linapozidiwa na hoja kama ilivyotokea majuzi huko Dom!

Ni kweli kabisa, manake kwa nafasi yake hakutakiwa kuhamaki kiasi kile halikadhalika kwa umri wake na taaluma (sijui kama inamsaidia chohote zaidi ya mshahara na allowances plus dubious deals) alitakiwa kuonyesha ukomavu.

Haya yote ni matokeo ya kuchagua Kiongozi eti " simply ni handsome" ataonekana vizuri kwenye pesa zetu? Huu ni uhayawani ambao hauwajawahi kutokea Duniani, pamoja na HASARA ZA MAKUSUDI bado kuna watu hawaoni wala hawafikirii kuwa sisi wananchi ndo tutakao lipa hizo pesa?
 
acha pumba fa.la wewe. yaana magufuli na kujitahidi kote hivi kulitumikia taifa na kwa uzembe uliopindukia wa mahakimu/majaji wetu unataka tena afanyweje? you are not serious.

Hata hao mahakimu/majaji wanapokea maagizo tu kwa hiyo usiwalaumu. Ni mapungufu ya system yetu ambayo mihimili yote mitatu anaisimamia mtu mmoja anayeitwa raisi. Kumbuka katika washtakiwa wamo wachina na unakumbuka yale ya prince wetu kule China? ungetarajia nini na usisahau pia kuna mikataba imesainiwa:A S wink:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…