Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Wakuu!
Kwa muda sasa nimefuatilia mwenendo wa wasanii wetu hasa kipindi hiki ambacho joto la uchaguzi Mkuu limepamba moto.
Sina shida na msanii yeyote kuonesha mlengo wake wa kisiasa huo ni uhuru wa mtu binafsi. Ila kinachokera na kuumiza ni pale msanii anapogeuka kuwa CHAWA wa Kisiasa, anapotumika kupamba sura ya Watawala, kuwa propaganda machine licha ya ukweli wa hali ya maisha ya wananchi, na kutetea mfumo.
Soma: Wasanii kujiingiza kwenye siasa na kuwa machawa ipi faida yao kama nao wanashiriki kuingiza wananchi shimoni?
Wasanii hawa hawafanyi hivyo kwa bahati mbaya. Wamejijengea kiburi kwa kuamini kuwa nguvu waliyonayo ya ushawishi ni silaha ya kupindisha ukweli. Na tusisahau, hiyo nguvu waliipata kupitia sisi mashabiki.
Ni sisi tuliowapa views, subscribers, likes, downloads na kutokea kwenye matamasha yao. Sasa basi, sisi pia tuna uwezo wa kuwatupa. Tuwakatae bila shari bali kwa msimamo. Tusisapoti kazi zao, biashara zao pia na kila kitu kinachowahusu.
Wakipoteza mashabiki, watakosa ushawishi na Kiburi kitaisha. Na hapo watatambua kuwa sanaa si chombo cha kutumikia mabwana, bali ni sauti ya watu.
Kama vipi Tuungane. Tuseme hapana kwa uchawa wa kisiasa wa wasanii huku Maisha ya Wananchi yakiwa Magumu.
Kwa muda sasa nimefuatilia mwenendo wa wasanii wetu hasa kipindi hiki ambacho joto la uchaguzi Mkuu limepamba moto.
Sina shida na msanii yeyote kuonesha mlengo wake wa kisiasa huo ni uhuru wa mtu binafsi. Ila kinachokera na kuumiza ni pale msanii anapogeuka kuwa CHAWA wa Kisiasa, anapotumika kupamba sura ya Watawala, kuwa propaganda machine licha ya ukweli wa hali ya maisha ya wananchi, na kutetea mfumo.
Soma: Wasanii kujiingiza kwenye siasa na kuwa machawa ipi faida yao kama nao wanashiriki kuingiza wananchi shimoni?
Wasanii hawa hawafanyi hivyo kwa bahati mbaya. Wamejijengea kiburi kwa kuamini kuwa nguvu waliyonayo ya ushawishi ni silaha ya kupindisha ukweli. Na tusisahau, hiyo nguvu waliipata kupitia sisi mashabiki.
Ni sisi tuliowapa views, subscribers, likes, downloads na kutokea kwenye matamasha yao. Sasa basi, sisi pia tuna uwezo wa kuwatupa. Tuwakatae bila shari bali kwa msimamo. Tusisapoti kazi zao, biashara zao pia na kila kitu kinachowahusu.
Wakipoteza mashabiki, watakosa ushawishi na Kiburi kitaisha. Na hapo watatambua kuwa sanaa si chombo cha kutumikia mabwana, bali ni sauti ya watu.
Kama vipi Tuungane. Tuseme hapana kwa uchawa wa kisiasa wa wasanii huku Maisha ya Wananchi yakiwa Magumu.