Nasema kwaheri CHADEMA iwapo....

Nasema kwaheri CHADEMA iwapo....

Je, ni matumizi mazuri ya ubongo kuwa au kutokuwa mwanachama wa CHADEMA kwasababu ya mtu mmoja?

baadhi ya wanachadema makini tunachotaka ni haki na usawa kwa wanachama wote - hatutaki ubaguzi, mbona lema alitapika hapa na uongozi umekaa kimya?!! zzk kama kuna ushahidi akiaadhibiwa ni sawa lakini na lema je, hakukuhitaji hata uchunguzi!!!!
 
Siko tayari kulala na Nyoka mmoja ndani, kisa tupo wengi ndani ya nyumba.

huna lolote wewe, chadema family...................lazma ukichunguzwa utakuwa 'mkaskazini' tuu!! kumtetea mbowe kichwa maji kisa tu damu nzito kuliko maji!!! tuletee ushahidi wa usaliti wa zzk kama sio porojo.
 
HOJA ZA CHUKI DHIDI YA WATU WA KASKAZINI, WACHAGA, NA SUALA LA DINI HAVITAMWACHA ZITTO WALA CCM IMARA KISIASA!... PIGENI DEBE SAANA ILI UDINI, UKANDA NA UKABILA UJENGEKE!... ZITTO aKIHAMIA CHAUMMA "UKIGOMA" NA UDINI WA CHAMA HIKI UTAONEKANA... AKIHAMIA CCM NI HIVYO HIVYO!... DHAMBI HII HAIACHI MTU!... CHAUMMA BAADA YA KUANZISHWA NA ZITTO SASA AMEMUWEKA MUHA MWENZIE NA MTU WA DINI YAKE HASHIM RUNGWE KUWA MWENYEKITI...

kwani uongo, lema na kilewo wamevunja katiba yetu ya mwaka 2006 ibara ya 10 - mbona hawajaguswa???!!! mwigamba aliiivunja akaadhibiwa fasta!!! yule mwenyekt wa chadema monduli nayeye aliivunja akaadhibiwa within 24 hours!!! wengine hatupendi undumilakuwili tunataka HAKI sawa ndani ya chama!!!!!
 
Wana JF, Mimi ni miongoni mwa vijana wengi ambao tunasubiri kwa hamu mustakabali wa siku 14 za maamuzi ya Kamati kuu ya CHADEMA kuhusiana na issue ya ZZK na wenzake.Siko peke yangu, tupo wengi. Siko tayari kuendelea kuwa mwanachama wa CDM iwapo Zitto atasamehewa na kuachiwa uanachama kwasbabu kuu 31. Alishindwa kututumikia katika nafasi ya Unaibu Katibu Mkuu wa Chama (Miezi 7 haingii Ofisini), eti kiongozi, kiongozi wa nani?2. CCM wanasikitika sana Zitto kusimamishwa uongozi, hii nalo ni janga, na nia ajabu. Karibu CCM wengi wanamtetea, kuna nini?3. Dharau;- Kabla hata ya siku 14 kuisha, anakimbilia kwa wanahabari huku akipata sapoti ya CCM, duu. Kali zaidi ni alipoenda redioni, ka. Yaani anaidharau Kamati kuu, kwanini asingekaa kimya.Najua inawezekana kukawa na sababu nyingi tu, ila kwa mimi NASEMA;- Kwa heri CDM iwapo Zitto ataendelea kuwa mwanachama wa CDM.

Sasa hizi ni sababu 31?? Viroba siyo maji!!!!
 
Zitto asipofukuzwa chadema mimi nitachukua maamuzi magumu katika siasa za Tanzania,

Siwezi kukitumikia chama ambacho kinaamua kumkumbatia baradhuri na mzandiki kama Zitto,

Heri nikajiunge na chama cha bwana Dovutwa,

he, yaani unadhani we ni mwanaCDM muhimu kuliko wengine, kutokuwepo kwako CDM kutatuathiri nn sisi tutakaobaki?! huu ubaguzi dhidi ya wengine ndo baadhi yetu tunaoupinga.....katiba inakupa uhuru kuchagua vyama vipo kibao ukiona CDM haifai chapa lapa nenda CCM, SAU, NCCR, CUF au kama pia na vyenyewe havifai anzisha chako, ndo demokrasia hiyo! Kwa akili yako zzk ndo kikwazo CDM, 'umeamua' kusahau mchango wake kwa chama hapo kilipo kisa tu umelishwa maneno ya usaliti bila kuwa na ushahidi na vielelezo vya kutosha. Wengine wetu wenye mawazo huru tunadhani hizi ni chuki tu kuelekea kwenye uchaguzi mkuu ndani ya chama vinginevyo chama kituletee ushahidi usio na shaka wa uhusika wa zzk ktk usaliti.
 
ZZK asipotolewa mimi naacha Siasa maana kuhama siwezi naipenda sana Chadema
 
Hawa vijana bana viroba na tindikali vinawatolesha sana akili,hivi katika ule waraka wa ushindi 2013,mbona matumizi mabaya ya fedha za ruzuku za chama na uendeshaji wake ambao unawahusisha watu watatu tu Mbona hawahoji?

Kama ndivyo,alishindwa nini kuhoji kwenye vikao halali wakati yeye ni mjumbe wa vikao vyote vya juu? anapoitwa msaliti na mnafiki hawakosei! rejea kazi/wajibu wa kamati kuu ni nini kwa chama? maoni yake au ushauri wake alitakiwa aupeleke kwenye vikao na si kufanya siasa za kuviziana dhidi ya viongozi wenzake.AFUKUZWE TU NA VIJANA WA MWANZA TUNAUNGA MKONO.
 
kama ndivyo,alishindwa nini kuhoji kwenye vikao halali wakati yeye ni mjumbe wa vikao vyote vya juu? Anapoitwa msaliti na mnafiki hawakosei! Rejea kazi/wajibu wa kamati kuu ni nini kwa chama? Maoni yake au ushauri wake alitakiwa aupeleke kwenye vikao na si kufanya siasa za kuviziana dhidi ya viongozi wenzake.afukuzwe tu na vijana wa mwanza tunaunga mkono.
naendelea tena mkuu unielewe.kutoka waraka wa ushindi 2013,na quote "inapofika ajenda ya masuala ya matumizi ya fedha huwa inarushwa na kusema tutaijadili kikao kijacho"kama hujanielewe nenda ukasome tena ule waraka
 
Je ni CCM ,CUF au ni vibaraka ndani ya CDM wakiwemo wakuu wao kwa kuivunja kila nyota inayotishia uhai wa CCM au inayotishia wakuu wenyewe ?

Kila utakaemsikia kafukuzwa au kasimamishwa uwanachama ndani ya CDM ,sababu za undani utaziona ni kuwa ananyemelea kugombea nafasi nyeti na hivyo huwahiwa mapema asije akawaangusha wazee wa Chama.

Ukiangalia Chama kama CUF wale waliofukuzwa wote hakuna alietishia uhai wa viongozi wakuu nikimaanisha kuwaangusha katika uchaguzi ,wengi wameonekana kujiengua wenyewe haswa pale wanaposhindwa kiuchaguzi na wengine kwa maslahi yao binafsi.

Kuna akina Lwakatare huyu nae amehamia CDM yanayomkuta huko kila mmoja anayajua ,Tambwe huyu mchumia tumbo CCM wesha mtupa ,mwengine ni Shaibu Akwilombe hajulikani amepotelea wapi na wengine wengi ambao walikiacha chama cha CUF ,lakini umakini na umahiri wa CUF umeonekana ,hakukutokea mtafaruku wala chama kuyumba kama inavyoonekana kwa CDM ,CDM inakufa ila inajikaza kisabuni ,ukweli ni kuwa CDM imechafua ile sura ambayo ilikuwa wameivaa ya kuwa chama makini na chenye muelekeo wa kuongoza Nchi hii .lakini imekuwa kama iliyovamiwa na viwavi jeshi ,imesambaratika na joto la kuzidi kusambaratika linaendelea.

Aidha viongozi wakuu wa CDM wanatumika na CCM kuuwa umoja wa WaTanzania ndio ukaona hawang'atuki au wameng'ang'ania ukubwa ,sio kosa ila ung'ang'aniaji wao haukubaliki ndani ya Chama wanachodai ni cha WaTz wote

Leo CDM inakufa vibaya sana ,kifo cha ajabu japo hakuna kifo kizuri. Beggars cant be choosers walala hoi hawana haki ya kugombea nafasi za juu.:A S 103:

Good comment, vipofu hawaoni kama CDM imeshakufa.!
 
Bado kwa vain reasons mnazozitoa hatutaimarisha upinzani nchini na kuchukua dola. Mbowe hataki kukubali kupingwa wakati wa chaguzi za chama. na mimi nasema, mpaka mbowe akubali kuacha kiti ndipo ntaelewa uhalisia wa demokrasia tunayoihubiri mitandaoni kila siku. mara ngapi Lipumba amepondwa humu kwa kungangania madaraka? mbona mko kimya kwa Mbowe?
 
ebo, umekuwa msemaji wa vijana wote chadema au Tanzania nzima?! na mie nasema ni kijana ila simsemei mtu - napenda kuona demokrasia halisi chadema tofauti na ya maccm! nataka kuona maelezo na vielelezo vya kutosha nijiridhishe usaliti wa zzk kabla sijamhukumu - kama kijana mwenye fikra huru nataka nijiridhishe pasipo na shaka bila ushabiki!!!!

Waambie hao wanafiki wenye chuki binafsi, fitina na wafata siasa za mkumbo wasiojielewa. Kuna aliyeusoma huo waraka akajua usaliti unaozungumzwa? Au ndo siasa za mkumbo na hisia? zzk anasema waraka haujui wakati huo huo aliyeuandaa huo waraka anasema zzk alikua haujui ww kama hakimu utamhukumu zzk kwa hisia zako au facts? Stupid
 
Back
Top Bottom