Gwappo Mwakatobe
JF-Expert Member
- Nov 22, 2019
- 1,486
- 1,861
Kuna wanandoa wengi hawaungani kindoa ili kuwa mwili mmoja, yaani umoja au ushirikiano wa kimaisha katika familia, bali huunganishwa na sifa au vitu alivyonavyo mtu.
Unaoa au kuolewa na fulani kwa kuwa ana elimu nzuri, mali nyingi, umbile zuri au cheo fulani. Mungu hakuunganishi na elimu, cheo, umbile au mali ya mtu. Unasahau kuwa utaishi na mtu, si vitu vyake!
Kwenye ndoa hatupaswi kufuata vitu alivyonavyo mtu, bali utu alionao mtu na tabia yake njema. Mungu anaunganisha upendo wa moyoni wa wawili bila kujali mali au vyeo vyao. Hivyo ni ziada tu, si kipaumbele!
Hao ndiyo ambao ndoa zao hudumu kwa kuvumiliana, kuchukuliana udhaifu na kupendana mioyoni - pawepo mali au pasina mali. Naonya: usioe au kuolewa na mali, elimu, umbile au cheo cha mtu. Oa au olewa na yeye alivyo - tabia yake njema.
Pia tukumbuke kinasemwa "anachounganisha" Mungu, si "wanachounganisha" watu wa makanisani, kimila au misikitini. Hao hawaoni mioyo ya watu bali huona sura ya nje yenye hila nyingi. Mungu huangalia yaliyoko moyoni (1 Samweli 16:7), ndiposa huunganisha hao wawili ikiwa mioyo haina hila. Ndoa nyingi Mungu hajawahi kuziunganisha!
Aidha, nirudie kusema: Mungu haunganishi vitu na watu, bali watu wenyewe na mioyo yao safi na upendo wa dhati! La sivyo talaka inakuwa inasubiri tu siku, maana ndani ya ndoa tunapaswa kuishi na mtu na utu wake, na si mtu na vitu vyake!!!
Unaoa au kuolewa na fulani kwa kuwa ana elimu nzuri, mali nyingi, umbile zuri au cheo fulani. Mungu hakuunganishi na elimu, cheo, umbile au mali ya mtu. Unasahau kuwa utaishi na mtu, si vitu vyake!
Kwenye ndoa hatupaswi kufuata vitu alivyonavyo mtu, bali utu alionao mtu na tabia yake njema. Mungu anaunganisha upendo wa moyoni wa wawili bila kujali mali au vyeo vyao. Hivyo ni ziada tu, si kipaumbele!
Hao ndiyo ambao ndoa zao hudumu kwa kuvumiliana, kuchukuliana udhaifu na kupendana mioyoni - pawepo mali au pasina mali. Naonya: usioe au kuolewa na mali, elimu, umbile au cheo cha mtu. Oa au olewa na yeye alivyo - tabia yake njema.
Pia tukumbuke kinasemwa "anachounganisha" Mungu, si "wanachounganisha" watu wa makanisani, kimila au misikitini. Hao hawaoni mioyo ya watu bali huona sura ya nje yenye hila nyingi. Mungu huangalia yaliyoko moyoni (1 Samweli 16:7), ndiposa huunganisha hao wawili ikiwa mioyo haina hila. Ndoa nyingi Mungu hajawahi kuziunganisha!
Aidha, nirudie kusema: Mungu haunganishi vitu na watu, bali watu wenyewe na mioyo yao safi na upendo wa dhati! La sivyo talaka inakuwa inasubiri tu siku, maana ndani ya ndoa tunapaswa kuishi na mtu na utu wake, na si mtu na vitu vyake!!!