Lipumba ametumwa kuanzisha huu mgogoro, sasa unataka Seif azungumze nae nini? Kuzungumza na Lipumba ni kuhalalisha hivi vituko anavyoendelea kuvifanya, na hiyo haikubaliki. Lipumba amekikosea sana chama kwa kukubali kutumika ili kukiangamiza. Mbaya zaidi, Lipumba amemkosea Mungu wake kwa kukubali kukisumbua chama ili kipoteze muda wake na yeye badala ya kupigania haki(ushindi) kilichoporwa kule Zanzibara kwenye uchaguzi wa October, 2015. Dhambi hizi hazitomuacha Lipumba salama kwani Mungu wa kweli ni mwema sana. Mh. Seif endelea na msimamo huohuo kwani upo sahihi. Kama ulivyokataa kishiriki uchaguzi wa maigizo wa March, 2016 kule Zanzibar ndio hivyohivyo unavyotakiwa kukataa kufanya mazungumzo na mtu ambaye ni dhahiri kabisa kwamba anatumika na maadui wa chama, ambao sina haja ya kuwataja.