Napokaribia kufika kileleni naanza kuunguruma

Napokaribia kufika kileleni naanza kuunguruma

yutu

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2013
Posts
1,778
Reaction score
1,223
HABARI GANI MARAFIKI HUMU NDANI NI MATUMAINI MU WAZIMA WA AFYA NJEMA.

Nakuja mbele yenu ili niweze kupata ushauri juu ya hili tatizo linalonikabili la ninapokaribia kufika kileleni (mshindo) naanza kuunguruma na miungurumo hiyo si ya kawaida ni ile inayofanana na wanyama kama simba, chui, mbuzi beberu, paka au mbwa na wakati mwingine hugugumia kama njiwa nk.

Tatizo hili lilianza kipindi cha nyuma kidogo na ex-girlfriend alinipigia sana kelele kuhusu tatizo hilo lakini sikumwelewa sasa huyu wa sasa hivi amenishikia bango na kudai nisipobadilika basi nijue sina mda mrefu nae kwani huko kuunguruma kuna mkera sana na kwa kunithibitishia hilo juzi kati tukiwa kwenye malavi davi alichukua kilonga longa chake akakiseti kwenye record ile tunaanza akabofya button ya kurekodia nisijue nini kinaendelea.

Baada mchezo wenye ushindi wa magoli matatu ndipo aliponiambia kwamba leo alikuwa na zoezi moja tu la kunirekodi huku nikimpuuza kwa hayo aliyoniambia kwani ni kweli huwa naunguruma lakini si kama anavodai, baada ya zoezi hilo aliifungulia simu na kuweka sauti juu kabisa kwakweli sikuweza kuamini kilichotokea yaani katika magoli yote niliweza kubadili miungurumo mitatu ya wanyama tofauti tofauti yaani iliogofya sana nikaone hapana niende jamvini nikatoe lililonisibu huenda nikapata pa kuanzia kwani mpaka sasa sijui nianze kwa vigagula au hospital.
 
^^
Unaikamia sana.
Unahitaji kuweka huru mwili wako (relaxed) na uone ni jambo la kawaida.
^^
 
Matatizo kama haya huwapata sana vijana wa machungani hasa mnapojikuta kwenye mahusiano na watoto wa mjini...hebu jaribu kubadili girlfriend,tafuta mtoto mmoja wa kienyeji (wa mfugaji) nenda naye machungani,omba 'ile kitu nammesaga mwenzie' kisha uone kama utatoa tena milio ya kondoo!...
 
Back
Top Bottom