Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Nimekuwa nikijiuliza ni kwa kiasi gani mawaziri, manaibu waziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wanavyoweza kufanya kazi zao kwa ufanisi na hatimaye kutoa tija kwa taifa. Kwa maoni yangu nimeona ni jambo hilo ni gumu kutokana na aina ya mfumo wa utumishi Tanzania, ambapo waziri ambaye mara nyingi huwa ni mbunge anayewakilisha wananchi wa jimbo lake hujikuta ameegemea zaidi katika kufanya kazi za serikali kama mmoja wa wasaidizi wa rais katika wizara husika. Hali hii hupelekea wengi wa mawaziri kujikuta wakishindwa hata kuwatumikia wapiga kura wao.Nakumbuka kuna waziri mmoja katika jimbo moja katika mkoa wa Tanga alipoenda kwenye kampeni watu walimuuliza mbona tangu tulipokuchagua hukuonekana tena mpaka miaka 5 imepita leo ndio umekuja kuomba kura zetu tena..akajitetea kuwa majukumu aliyopewa na raisi akimaanisha uwaziri yamekuwa yakimfanya akose muda wa kutembelea wapiga kura wake.....:lol:
Hili pia lipo kwa manaibu mawaziri na wakuu wa mikoa na hasa wale wenye kofia mbili ubunge na ukuu wa mkoa. Katika mchakato wa kura za maoni tumeona pia baadhi ya wakuu wa wilaya wakijitumbukiza katika mbio za kutaka ubunge mfano Bi Betty Machangu (kasulu), Said Bwanamdogo (kondoa) na wengine.
Nadhani badala ya viongozi hawa kuwa wa kuteuliwa na raisi wengi wamekuwa wameshindwa kufanya kazi kwa ufanisi kwa kukosa uwezo na sifa kwa kazi walizopewa. HIvyo basi napendekeza kuwa nafasi za mawaziri, naibu waziri, wakuu wa mikoa na wilaya ziwe zinatangazwa watu wanaomba, kusairiwa na baadaye kuajiriwa tena kwa mkataba. Na atakaposhindwa ku-deliver anatimuliwa kazi.
Kwa njia hii kuna uwezekano mkubwa sana wa kupata watu wenye sifa na uwezo na sio kusubiri raisi ateuwe majina ya wabunge kupewa uwaziri, ukuu wa mkoa na ukuu wa wilaya matokeo yake kutuwekea watu wa ajabu ajabu.....Hebu tulijadilili hili wadau .
Hili pia lipo kwa manaibu mawaziri na wakuu wa mikoa na hasa wale wenye kofia mbili ubunge na ukuu wa mkoa. Katika mchakato wa kura za maoni tumeona pia baadhi ya wakuu wa wilaya wakijitumbukiza katika mbio za kutaka ubunge mfano Bi Betty Machangu (kasulu), Said Bwanamdogo (kondoa) na wengine.
Nadhani badala ya viongozi hawa kuwa wa kuteuliwa na raisi wengi wamekuwa wameshindwa kufanya kazi kwa ufanisi kwa kukosa uwezo na sifa kwa kazi walizopewa. HIvyo basi napendekeza kuwa nafasi za mawaziri, naibu waziri, wakuu wa mikoa na wilaya ziwe zinatangazwa watu wanaomba, kusairiwa na baadaye kuajiriwa tena kwa mkataba. Na atakaposhindwa ku-deliver anatimuliwa kazi.
Kwa njia hii kuna uwezekano mkubwa sana wa kupata watu wenye sifa na uwezo na sio kusubiri raisi ateuwe majina ya wabunge kupewa uwaziri, ukuu wa mkoa na ukuu wa wilaya matokeo yake kutuwekea watu wa ajabu ajabu.....Hebu tulijadilili hili wadau .