Napendekeza Mkuu wa majeshi Gambia apewe Tuzo ya Nobel (AMAN)

Askari Muoga

JF-Expert Member
Oct 22, 2015
6,113
4,652
Kufuatia Rais wa zamani wa Gambia Bwana Jammeh kung'ang'ania madaraka baada ya kushindwa kwenye Uchaguzi,MKUU WA majeshi Gambia ameonesha au amefanya jambo la kuigwa sana Afrika na Duniani baada ya kukataa kumpa suport Bwana jameh ili ni jambo la kuigwa sana kwani viongozi wengi wa Afrika wanategemea majeshi yao yawaunge mkono katika kubaki madarakani,nampongeza sana Kamanda uyu wa GAMBIA NA ANASTAHILI APEWE TUZO YA NOBEL kwa kuheshimu maamuzi ya Wananchi kwani Viongozi wengi wa Afrika wanatumia vyombo vya usalama ku deploy au kukandamiza Demokrasia
 
Huyu jama nae amesoma alama za nyakati kwani nae hakuwa salama, awali alishatangaza kumuunga mkono huyu dikteta kwa njia yoyote. Ameona majeshi ya ECOWAS yako kila pembe na wengine wapo ndani ya Gambia akaona bora amtose mwenzie.
 
Kufuatia Rais wa zamani wa Gambia Bwana Jammeh kung'ang'ania madaraka baada ya kushindwa kwenye Uchaguzi,MKUU WA majeshi Gambia ameonesha au amefanya jambo la kuigwa sana Afrika na Duniani baada ya kukataa kumpa suport Bwana jameh ili ni jambo la kuigwa sana kwani viongozi wengi wa Afrika wanategemea majeshi yao yawaunge mkono katika kubaki madarakani,nampongeza sana Kamanda uyu wa GAMBIA NA ANASTAHILI APEWE TUZO YA NOBEL kwa kuheshimu maamuzi ya Wananchi kwani Viongozi wengi wa Afrika wanatumia vyombo vya usalama ku deploy au kukandamiza Demokrasia
Amefanya nini? ndo kwanza asubuhi hatujafukunyua
 
Huyo ni mnafki mara baada ya kuona majeshi na vifaa mengi yanakuja ndio anajifanya kuretreat

Alitoa kiapo cha utii na kumkataa Barrow wazi
 
Pro utawala hapa kwetu utawajua kwa kuchukia maamuzi ya wananchi nawe ni mmoja wao
hahaha umekosea sana mkuu, kuna sehem nimecomment kumhusu huyo raisi, hafai kwa vile anahisi nchi ni ya kwake binafsi, the likes of African leaders wanajiona wao ndo wao kama vile wataishi milele
 
Kufuatia Rais wa zamani wa Gambia Bwana Jammeh kung'ang'ania madaraka baada ya kushindwa kwenye Uchaguzi,MKUU WA majeshi Gambia ameonesha au amefanya jambo la kuigwa sana Afrika na Duniani baada ya kukataa kumpa suport Bwana jameh ili ni jambo la kuigwa sana kwani viongozi wengi wa Afrika wanategemea majeshi yao yawaunge mkono katika kubaki madarakani,nampongeza sana Kamanda uyu wa GAMBIA NA ANASTAHILI APEWE TUZO YA NOBEL kwa kuheshimu maamuzi ya Wananchi kwani Viongozi wengi wa Afrika wanatumia vyombo vya usalama ku deploy au kukandamiza Demokrasia
Haswa wa A. Mashariki ni aibu, angalia Uganda, Burundi, Rwanda, znz, Kongo sijui s. Sudan, Kenya na tz itakuwaje post election. Wengine wanaanda mazingira feki ya uchaguzi, time feki, ili kupata matokeo feki na uhalali feki wa kubakia madarakani. Mfano Znz. Mungu ambari sana Mkuu wa majeshi Gambia. Hajawa kama hawa wachumia tumbo wanaotumika kugandamiza haki na binadamu kwa tamaa ya madaraka. Mungu nao wape stahili yao.
 
Haswa wa A. Mashariki ni aibu, angalia Uganda, Burundi, Rwanda, znz, Kongo sijui s. Sudan, Kenya na tz itakuwaje post election. Wengine wanaanda mazingira feki ya uchaguzi, time feki, ili kupata matokeo feki na uhalali feki wa kubakia madarakani. Mfano Znz. Mungu ambari sana Mkuu wa majeshi Gambia. Hajawa kama hawa wachumia tumbo wanaotumika kugandamiza haki na binadamu kwa tamaa ya madaraka. Mungu nao wape stahili yao.
Ipo siku tutafika tu!
 
hahaha umekosea sana mkuu, kuna sehem nimecomment kumhusu huyo raisi, hafai kwa vile anahisi nchi ni ya kwake binafsi, the likes of African leaders wanajiona wao ndo wao kama vile wataishi milele
Samahani mkuu, katiba zetu zimekuwa makaratasi sana na Marais wa kiafrika wamegeuka ma Miungu watu kiasi katiba hazina maana mbele yao.

Wanawafanya wananchi kama kuku wa kizungu
 
Njia sahihi na pekee ya kujihakikishia kuishi kwa amani ni kutenda mema na kutomtegemea binadamu mwenzio.
Nawacheka sana wanaowanyanyasa binadamu wenzao kwa kigezo kwamba 'tuna serikali na jeshi' hadi kuwatenganisha watu na wapendwa wao kwa kuwaweka jela bila sababu!
Mliofuatilia na kuendelea kufuatilia suala la Gambia nadhani tumejifunza mengi juu ya 'cheo ni dhamana'. Mwalimu Nyerere aliyaona hayo miaka mingi sana na kujitahidi kuutenganisha urais (cheo) na maisha yake binafsi.
Yahya Jammeh alidhani watu wote ni wajinga kama yeye akasahau kuwa kukaa kimya sio kigezo cha kutokujua. Na hata baada ya kumchagua mpinzani yeye aliamua kutumia ujinga wa watawala kuitumia mahakama kuzuia eti asiapishwe pia kuliamuru bunge limuongezee muda akijua 'ataisimamia kesi' husika.
 
Kwa hili nawapongeza ECOWAS


Huyu mkuu wa majeshi hakutaka makuu baada ya kuona jamaa wana mshikamano.
Yaani kwa jeshi dogo namna hiyo sidhani kama hata wanahitaji kuwa na bajeti ya ulinzi.
Tumeanza kujielewa sasa, binafsi sipendelei vita bali suluhisho na amani vitawale.

Tumeshuhidia wananchi wa Gambia walivyohaha na kuikimbia nchi.
Lakini nchi zingine wameingilia na kuonyesha msimamo wao.
 
tatizo wanapogombea uraisi wanatupa matumaini mno lkn cha ajabu wakishapata wanatugeuka kwa kujifanya MUNGU WATU!, KUWEKA SHERIA ZA KIKATILI, KUNYANYASA WENGINE na kila aina ya ubaya.
 
Huyu jama nae amesoma alama za nyakati kwani nae hakuwa salama, awali alishatangaza kumuunga mkono huyu dikteta kwa njia yoyote. Ameona majeshi ya ECOWAS yako kila pembe na wengine wapo ndani ya Gambia akaona bora amtose mwenzie.
Mkuu! Ungekua wewe ndo upo kwenye nafasi ya Mkuu wa Majeshi wa Gambia,ungesema nini?
 
Back
Top Bottom