Napendekeza king’amuzi kimoja kwa kampuni zote za ving’amuzi

Napendekeza king’amuzi kimoja kwa kampuni zote za ving’amuzi

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
40,516
Reaction score
46,602
Kwahiyo ukiwasha king’amuzi hicho itakuja menu ya kampuni unayotaka kuangalia, utachagua either Dstv, Startimes, Azam, Zuku, Digitek nk; na pia endapo kampuni nyingine yeyote itataka kujiunga kuongezwa kwenye menu, inafanyika software update ya kuiongeza automatically unapokiwasha king’amuzi.

Kwahiyo mteja ataenda kununua kadi ya kampuni husika kama anavyonunua laini ya simu, ataisajili na kwenda kuichomeka, sasa kwakua masafa ya kila Kampuni hutofautiana, basi ile dish inayofungwa juu itakuwa na kamotor kadogo ambako kako preprogrammed kuelekeza dish kwenye muelekeo wa masafa wa kampuni husika ambayo kadi yake imechomekwa kwenye king’amuzi, yale mambo ya kuita fundi aje kurekebisha dish yamepitwa na wakati.

Mteja anaweza akawa na kadi za ving’amuzi hata 10 ndani ya nyumba, ila king’amuzi kimoja na dish ni moja tu, yaani hadi raha, italeta upinzani ushindani mzuri sana tofauti na sasa ambapo mtu ana uhakika kwamba king’amuzi chake mdio unacho kwahiyo hata ukikuudhi huna ujanja wa kung’oa dish na kufunga cha kampuni nyingine.

Mtu yeyote anaweza akatengeneza mfumo huu na kuuza ving’amuzi vyake kwa wateja, na hao wateja kazi yao itakuwa ni kwenda kununua kadi za ving’amuzi anavyovipemda, kimachotakiwa ni wamiliki wa kampuni za TV kuzi-unlock kadi zao ili ziweze kusoma kwenye hizi universal decoders.

Pia hii itawezesha kuanzishwa kwa kampuni nyingi sana chipukizi za TV za kulipia, maana tunakuwa tumetengenisha kazi ya kusupply na kufunga madish na ving’amuzi na kazi ya kuuza vipindi vya TV, kwahiyo wewe unaaanzisha tu TV yako na kununua masafa kisha unauza kadi zako za decoder kama laini za simu..., raha sana..

Ni hayo tu...
 
Kwahiyo ukiwasha king’amuzi hicho itakuja menu ya kampuni unayotaka kuangalia, utachagua either Dstv, Startimes, Azam, Zuku, Digitek nk; na pia endapo kampuni nyingine yeyote itataka kujiunga kuongezwa kwenye menu, inafanyika software update ya kuiongeza automatically unapokiwasha
Is it possible kwenye dunia hii ya ubepari?
 
Nadhani kila king'amuzi kinakuwa na teknolojia yake. Sidhani kama itakuwa rahisi kwa kampuni kama DSTV wakubali watumie king'amuzi sawa na watu kama Startimes.
... kama nimemwelewa mleta mada anapendekeza TV ziwe kama radio; kwa kutumia redio moja unaweza kupata stations zote as along as mawimbi yanakufikia. Ni wewe kucheza na button kutafuta FM, MW, SW1, SW2, SW3, ... etc.
 
Hata makampuni ya simu waweke vocha moja hiyohiyo inaingia mtandao wowote
Makapuni ya simu tayari yanatoa laini ambayo unaweza kuiweka kwenye simu yeyote unayoitaka, iwe Samsung, iphone, tecno nk., hivyo hivyo na makampuni ya TV yatoe Kadi ambayo mtu unaweza kwenda kuweka kwenye decoder yeyote (universal) unayopenda.
 
Ndio maana tunachombo cha usimamizi (TCRA), kikiunda kanuni basi hauna budi kuifuata, vinginevyo unafutiwa leseni
... tatizo technology zote ziko imported na haziwez kubadilishwa kirahisi na TCRA. Duniani huko wakibadili kama unavyoshauri ndipo TCRA watakuwa na "meno" ya kutunga kanuni ziendane na technology hizo.
 
Makapuni ya simu tayari yanatoa laini ambayo unaweza kuiweka kwenye simu yeyote unayoitaka, iwe Samsung, iphone, tecno nk., hivyo hivyo na makampuni ya TV yatoe Kadi ambayo mtu unaweza kwenda kuweka kwenye decoder yeyote (universal) unayopenda.
Hapa nimekuelewa mkuu, Kwamba makampuni ya hivi Vingamuzi Yauze Kadi na vifurushi,. Kingamuzi kiwe kimoja kinachoruhusu kadi yoyote ya kampuni yoyote ya Kingamuzi.. Au nimeelewa tofauti?
 
... tatizo technology zote ziko imported na haziwez kubadilishwa kirahisi na TCRA. Duniani huko wakibadili kama unavyoshauri ndipo TCRA watakuwa na "meno" ya kutunga kanuni ziendane na technology hizo.
Mbona ving’amuzi universal ndio hivi hivi tu uki-unlock? Hata simu zamani ukinunua ya Tigo, halafu ukataka kuweka laini ya Vodacom unaenda kwa fundi simu anai-flash ili kuondoa ili programme na kurudisha default factory settings (unlock), kwahiyo hakuna cha ajabu, pia tukiweka kanuni zetu, hao wanaotengeneza watabadilisha kulingana na matakwa yetu, maana sisi ndio wateja na watafanya tunachokihitaji.
 
Mchina atalifanyia kazi suala hilo....

Nakumbuka nlikuwaga na moderm ni universal

Unachomeka line yoyote kitu na box

Ova
 
Mchina atalifanyia kazi suala hilo....

Nakumbuka nlikuwaga na moderm ni universal

Unachomeka line yoyote kitu na box

Ova
Hata sasa modem karibu zote ni universal, mwanzoni ndio walikuwa wanazi-lock ili itumike laini moja ya mtandao huo huo waliokuuzia..
 
Kila king'amuzi kina satellite yake wanayotumia kwaajili ya kurusha matangazo,labda kama kampuni zote ziamue kutumia satellite moja hiyo inawezekana,mfano madishi ya azamu yanaelekea 7°E, Dstv wanaelekeza South,startimes etc...
 
Kila king'amuzi kina satellite yake wanayotumia kwaajili ya kurusha matangazo,labda kama kampuni zote ziamue kutumia satellite moja hiyo inawezekana,mfano madishi ya azamu yanaelekea 7°E, Dstv wanaelekeza South,startimes etc...
Mbona nimeeleza solution, nadhani umesoma heading bila kusoma uzi
 
Si kuna kipindi walitaka kuanzisha hii sijui waliishia wapi?

It's possible ila naona ni gharama sana and not practical
 
Back
Top Bottom