DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amemsifu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi wake uliojengwa katika misingi ya utu, usikivu na maridhiano.
Akizungumza na wananchi wa Jimbo la Mtama wataka Waufungaji Wa kampeni wa Jimbo Hilo Nape amesema Rais Samia ameonesha mfano wa kipekee wa uongozi unaosikiliza wananchi na kuongoza kwa busara, hali iliyowezesha Tanzania kubaki katika amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa.
“Utu wa Mama Samia ndio nguzo ya amani ya Taifa letu. Amejenga Tanzania yenye maridhiano, yenye kusikilizana na kuheshimiana,” amesema Nape.
Ameongeza kuwa, chini ya uongozi wa Rais Samia, Watanzania wameendelea kuona maendeleo yakisukumwa kwa kasi huku umoja na upendo vikipewa kipaumbele kuliko migawanyiko na misuguano ya kisiasa.
Mama Samia amethibitisha kwamba uongozi bora ni ule unaojengwa juu ya utu, si nguvu. Anaongoza kwa hekima, huruma na kusikiliza na matokeo yake ni Taifa lenye utulivu na matumaini mapya,” amehitimisha Nape.
Akizungumza na wananchi wa Jimbo la Mtama wataka Waufungaji Wa kampeni wa Jimbo Hilo Nape amesema Rais Samia ameonesha mfano wa kipekee wa uongozi unaosikiliza wananchi na kuongoza kwa busara, hali iliyowezesha Tanzania kubaki katika amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa.
“Utu wa Mama Samia ndio nguzo ya amani ya Taifa letu. Amejenga Tanzania yenye maridhiano, yenye kusikilizana na kuheshimiana,” amesema Nape.
Ameongeza kuwa, chini ya uongozi wa Rais Samia, Watanzania wameendelea kuona maendeleo yakisukumwa kwa kasi huku umoja na upendo vikipewa kipaumbele kuliko migawanyiko na misuguano ya kisiasa.
Mama Samia amethibitisha kwamba uongozi bora ni ule unaojengwa juu ya utu, si nguvu. Anaongoza kwa hekima, huruma na kusikiliza na matokeo yake ni Taifa lenye utulivu na matumaini mapya,” amehitimisha Nape.