Nape Nnauye: Process ya kumfukuza mtu CCM ni ndefu

Nape Nnauye: Process ya kumfukuza mtu CCM ni ndefu

Kumbe ndiyo maana MAFISADI hawafukuziki.
 
Nape zile siku 90 ulizompa Laigwanan Lowassa na Mtemi Chenge zinaisha lini? Au zilikua siku 900 magazeti yalikunukuu vibaya?
 
Tulishamzoea Nape, ni mzee wa hoja za matukio, hua hana cha kuisema CDM sasa atakipata! Wafanye utaratibu wa kumfukuza Lowasa na Chenge basi! Mbona Mansoor walimtimua au kisa ha nguvu ya kisiasa?
 
Huyo nyepesi mwenyewe nasikia anaugua ule ugonja wa basket ya m,bakaji kwa hiyo anatafuta pakufia tu
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye amesifu utaratibu wa CCM unaofuatwa kabla ya kumfukuza mtu uanachama na amesema kwa CCM kuna vikao vingi kabla uamuzi wa kumfukuza mtu uanachama haujafikiwa.

Pia,Nape amedai kinachomponza Zitto ni kuhoji maswala ya ukaguzi wa ruzuku na nia yake ya kugombea uongozi ndani ya chama.

Vile vile Nape amepiga kijembe kwa kusema kama watu hawa wakipewa madaraka makubwa ya kushika dola itakuwaje kama madaraka ya kuongoza chama tu wanayatumia hivyo.

Nape allikuwa akiongea katika mahojiano na mtangazi wa TBC 1 asubuhi hii kwenye kipindi cha Jambo kinachorushwa na TBC1.

MT TAKE:
CCM waliwahi kujaribu kumfukuza nani uanachama katika siku za hivi karibuni?

Stupid Nape! Yaani kuwa na njia ndefu nayo ni sifa!
Kumbe siyo ajabu kwao kuwa na watu makapi kwa kipindi kirefu kiasi hicho?

Tatizo la CCM ni mkusanyiko wa watu wasiyo na sifa ya ajira nyingine, na wamefanya 'chama' ndo ajira. Hawawezi kutoka, hawawezi kujiuzuru maana nani hataki ajira? Sasa tena mtu anapayuka kwamba hata kufukuzwa ni vigumu. Hicho ni chama gani sasa!
 
Kwa sababu ya hii process ndefu ya kumwajibisha mwenye makosa ndani ya ccm ndiyo maana chama hiki na serikali yake kimejaa mafisadi na wala rushwa.
 
Nepi huwa hawazi anachoongea zaidi ya kuropoka,mfano majuzi juzi tu mwishoni mwa mwaka jana amesikika akisema mikutanoni sehemu walizozungukia na mwenzie Adui wa NDOVU wetu Kinana kuwa mawaziri wa ccm mizigo akiwemo MGIMWA,cha ajabu amekufa mzee wa watu wanaanza kuropoka eti alikuwa kiongozi wa kuigwa. CCM hawa wadata,ni kuwachukulia vichaa hivi hivi.
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye amesifu utaratibu wa CCM unaofuatwa kabla ya kumfukuza mtu uanachama na amesema kwa CCM kuna vikao vingi kabla uamuzi wa kumfukuza mtu uanachama haujafikiwa.

Pia,Nape amedai kinachomponza Zitto ni kuhoji maswala ya ukaguzi wa ruzuku na nia yake ya kugombea uongozi ndani ya chama.

Vile vile Nape amepiga kijembe kwa kusema kama watu hawa wakipewa madaraka makubwa ya kushika dola itakuwaje kama madaraka ya kuongoza chama tu wanayatumia hivyo.

Nape allikuwa akiongea katika mahojiano na mtangazi wa TBC 1 asubuhi hii kwenye kipindi cha Jambo kinachorushwa na TBC1.

MT TAKE:
CCM waliwahi kujaribu kumfukuza nani uanachama katika siku za hivi karibuni?

Hata kama hakuna mwanachama mwenye makosa wakufuzane tu?
 
Ni rahisi Polisi kumwangalia usoni mshitakiwa wakati polisi huyo akiwa amavaa magwanda polisi counter, ni vigumu polisi huyo huyo kuwangalia usoni mshitakiwa huyo wakikutana nae peponi maana kila mtu hana cheo chochote. CCM kama chama tawala ni vigumu kuwafukuza wanachama wao wanaoshindwa kutekeleza madaraka waliyopewa kama mawaziri makatibu wakuu wanachofanya ni kuwafukuza tu kwenye hizo nyazifa walizowapa.

Ila itakapofikia CCM ni chama cha upinzani watawafukuza sana tu wanachama wao na itakuwa rahisi mno fikiria wanachama wa CCM anakisaliti chama chama chake kwa chama tawala kama CHADEMA kweli CCM watamwacha? Wakimwacha tu aendelee na usaliti basi kitakuwa chama cha ajabu sana.

My take Nape tafakari tena kauri yako kuhusu CCM kufuza wanachama wake uanachama baada ya waraka huu.
 
I bet, hata iweje hamuwezi kumpatia kila mtz maji safi na salama mita 400 ifikapo 2015 kwa muda uliobakia- mlituhadaa tuwape kura na kula huku mkijua uwezo hamna. Viwanja vya ndege, meli na reli ni hadithi za alnacha. Maisha bora hayaji kwa kasi, nguvu na ari zaidi. Tangazeni kuwa mmetudanganya vyakutosha, kutuhadaa vya kutosha na kutubumbaisha vya kutosha. Umbumbu wetu mlio tuwekamo ndio umetufikisha hapo. Sasa tangazeni kushindwa kwenu.
 
Back
Top Bottom