Eddo Sambai
JF-Expert Member
- Aug 1, 2013
- 2,412
- 1,928
CHADEMA wao wanaku-wangwe!
Hata haitamkiki, Jitu zima aibu
CHADEMA wao wanaku-wangwe!
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye amesifu utaratibu wa CCM unaofuatwa kabla ya kumfukuza mtu uanachama na amesema kwa CCM kuna vikao vingi kabla uamuzi wa kumfukuza mtu uanachama haujafikiwa.
Pia,Nape amedai kinachomponza Zitto ni kuhoji maswala ya ukaguzi wa ruzuku na nia yake ya kugombea uongozi ndani ya chama.
Vile vile Nape amepiga kijembe kwa kusema kama watu hawa wakipewa madaraka makubwa ya kushika dola itakuwaje kama madaraka ya kuongoza chama tu wanayatumia hivyo.
Nape allikuwa akiongea katika mahojiano na mtangazi wa TBC 1 asubuhi hii kwenye kipindi cha Jambo kinachorushwa na TBC1.
MT TAKE:
CCM waliwahi kujaribu kumfukuza nani uanachama katika siku za hivi karibuni?
Ukweli ni kuwa kama Nape aliongea hivyo hajasema uwongo. Katika CCM hakuna utaratibu wa kufukuzana na ndiyo maana nchi yetu inaendeshwa hovyo kwa sababu ya kuongozwa na chama kisichoweza kuwawajibisha viongozi wake. Nape alipopewa nafasi aliyonayo alitoa siku 90 kwa mafisadi kujiuzulu na kwamba wasingefanya hivyo wangeshughulikiwa. Hadi leo hakikufanyika chochote zaidi ule wimbo alianza kuuimba na Ndugu Kinana kuwa kuna mawaziri mizigo.
Kwa kusema kuwa katika CCM kuna process ndefu ya mtu kufukuzwa katika CCM siyo jambo zuri bali ni udhaifu. Udhaifu huo ndio ambao unalipeleka taifa pabaya. Fikiria twiga anasafirishwa nje ya nchi hakuna anayewajibishwa kwa sababu process ni ndefu ya kuwajibishana na mwisho wa siku hakuna kuwajibishana. Kwa sababu ya uzembe wao huo tunashangaa eti tembo wanauawa wengi na wapo hatarini kutoweka, tunataka tumlaumu nani?
Tunakushukuru Nape kwa kauli yako hiyo kwani umekuwa mkweli lakini ujue unatuambia udhaifu wenu na wala hatuna la kuiga hapo.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye amesifu utaratibu wa CCM unaofuatwa kabla ya kumfukuza mtu uanachama na amesema kwa CCM kuna vikao vingi kabla uamuzi wa kumfukuza mtu uanachama haujafikiwa.
Pia,Nape amedai kinachomponza Zitto ni kuhoji maswala ya ukaguzi wa ruzuku na nia yake ya kugombea uongozi ndani ya chama.
Vile vile Nape amepiga kijembe kwa kusema kama watu hawa wakipewa madaraka makubwa ya kushika dola itakuwaje kama madaraka ya kuongoza chama tu wanayatumia hivyo.
Nape allikuwa akiongea katika mahojiano na mtangazi wa TBC 1 asubuhi hii kwenye kipindi cha Jambo kinachorushwa na TBC1.
MT TAKE:
CCM waliwahi kujaribu kumfukuza nani uanachama katika siku za hivi karibuni?
CHADEMA wao wanaku-wangwe!
ccm hafukuzwi mtu bali ukileta zako wana kukolimba fasta
Nape utaangaika sana ndo maana ccm kuna mgawanyiko na ww unajulikana upokundi gani na kuhusu zzk mchukueni aje afanye siasa safi ccm na kwa ushairi jenga chama chako achana na cdmSasa Lowasa ndie atakaegombea uraisi kwa tiketi ya ccm, kamwambie huyo Nape anze mpango wa kutafuta uraiya wa nchi jirani kama alivyo aidi.