Nape Nnauye: Process ya kumfukuza mtu CCM ni ndefu

Nape Nnauye: Process ya kumfukuza mtu CCM ni ndefu

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,212
Reaction score
162,791
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye amesifu utaratibu wa CCM unaofuatwa kabla ya kumfukuza mtu uanachama na amesema kwa CCM kuna vikao vingi kabla uamuzi wa kumfukuza mtu uanachama haujafikiwa.

Pia,Nape amedai kinachomponza Zitto ni kuhoji maswala ya ukaguzi wa ruzuku na nia yake ya kugombea uongozi ndani ya chama.

Vile vile Nape amepiga kijembe kwa kusema kama watu hawa wakipewa madaraka makubwa ya kushika dola itakuwaje kama madaraka ya kuongoza chama tu wanayatumia hivyo.

Nape allikuwa akiongea katika mahojiano na mtangazi wa TBC 1 asubuhi hii kwenye kipindi cha Jambo kinachorushwa na TBC1.

MT TAKE:
CCM waliwahi kujaribu kumfukuza nani uanachama katika siku za hivi karibuni?
 
Katibu wa Itikadi na
Uenezi wa CCM,Nape Nnauye amesifu utaratibu wa CCM unaofuatwa kabla ya
kumfukuza mtu uanachama na amesema kwa CCM kuna vikao vingi kabla uamuzi
wa kumfukuza mtu uanachama haujafikiwa.

Pia,Nape amedai kinachomponza Zitto ni kuhoji maswala ya ukaguzi wa
ruzuku na nia yake ya kugombea uongozi ndani ya chama.

Vile vile Nape amepiga kijembe kwa kusema kama watu hawa wakipewa
madaraka makubwa ya kushika dola itakuwaje kama madaraka ya kuongoza
chama tu wanayatumia hivyo.

Nape allikuwa akiongea katika mahojiano na mtangazi wa TBC 1 asubuhi hii
kwenye kipindi cha Jambo kinachorushwa na TBC1.

MT TAKE:
CCM waliwahi kujaribu kumfukuza nani uanachama katika siku za hivi
karibuni?

mansour wa zanzibar
 
Ukweli ni kuwa kama Nape aliongea hivyo hajasema uwongo. Katika CCM hakuna utaratibu wa kufukuzana na ndiyo maana nchi yetu inaendeshwa hovyo kwa sababu ya kuongozwa na chama kisichoweza kuwawajibisha viongozi wake. Nape alipopewa nafasi aliyonayo alitoa siku 90 kwa mafisadi kujiuzulu na kwamba wasingefanya hivyo wangeshughulikiwa. Hadi leo hakikufanyika chochote zaidi ule wimbo alianza kuuimba na Ndugu Kinana kuwa kuna mawaziri mizigo.

Kwa kusema kuwa katika CCM kuna process ndefu ya mtu kufukuzwa katika CCM siyo jambo zuri bali ni udhaifu. Udhaifu huo ndio ambao unalipeleka taifa pabaya. Fikiria twiga anasafirishwa nje ya nchi hakuna anayewajibishwa kwa sababu process ni ndefu ya kuwajibishana na mwisho wa siku hakuna kuwajibishana. Kwa sababu ya uzembe wao huo tunashangaa eti tembo wanauawa wengi na wapo hatarini kutoweka, tunataka tumlaumu nani?

Tunakushukuru Nape kwa kauli yako hiyo kwani umekuwa mkweli lakini ujue unatuambia udhaifu wenu na wala hatuna la kuiga hapo.
 
Kama tafsiri ya maendeleo ya nchi ni pye pye za chama cha siasa basi Tanzania ingekuwa juu kuliko USA! Nape asema hivi na vile...Mwigulu asema hivi na vile...Mbunge aliyeingia Bungeni kwa mbeleko afanya mkutano mkubwa sana....na mengine na mengine! Hii itawasaidia nini wananchi wa kawaida ambao hawana hata uhakika na kesho yao?
 
Jamaniyeeeeeee!! Mangula alitoa miezi 6 waliopata nafasi kwa rushwa wajiondoe vinginevyo wataondolewa,,, MBONA KIMYA MPAKA LEO?
Au alidhani haitaisha? Honey moon yake bado!!
 
Vipi alisikika akizungumzia na kutoa ufafanuzi wa kwanini umeme umepanda hivi wakati vipato viko palepale? Nimempa ndani ya wiki moja aje azungumzie kwa kina kupanda huku kwa umeme na atueleze wana nia njema na kupanda kwa uchumi wetu? Tumechoka na siasa za maji taka tunataka atupe hatima za maisha yetu kwa wao kutupa maelezo sahihi. Watu wote tusikae kimya mpaka watupe maelezo ya kina.
 
Sio lazima kila uamuzi uwe sahihi. Lakini UTHUBUTU una maana sana katika maisha ya uongozi wa watu.
Nyerere asingethubutu - tusingepata uhuru, Afrika ingekuwa bado kwenye mikono ya ukoloni na ubeberu!!!
Karume asingethubutu - Zanzibar ingeendelea kuwa chni ya Sultani
Ndani ya uthubutu wao wamefanya makosa kadha wa kadha, tunachokiangalia ni dhamira yao na wala sio makosa yao kwani makosa ni sehemu ya mchakato wa utekelezaji wa dhamira fulani!!

Kwa mtazamo wangu CHADEMA wanajaribu kuthubutu ili kubadilisha mitazamo ya watu ambayo imekuwa mgando kiasi cha kushindwa kufikiri kwa usahihi na kufanya maamuzi yenye manufaa. Katika kufanya hivyo inawezekana wakafanya makosa lakini dhamira ndiyo itawaongoza. CHADEMA waachwe waendelee KUTHUBUTU!
 
Hapo amedanganya,ccm wanayo victimisation sometimes na ndo hii tabia ambayo chadema wanataka kuianza that's why tuikemee kwa nguvu
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye amesifu utaratibu wa CCM unaofuatwa kabla ya kumfukuza mtu uanachama na amesema kwa CCM kuna vikao vingi kabla uamuzi wa kumfukuza mtu uanachama haujafikiwa.

Pia,Nape amedai kinachomponza Zitto ni kuhoji maswala ya ukaguzi wa ruzuku na nia yake ya kugombea uongozi ndani ya chama.

Vile vile Nape amepiga kijembe kwa kusema kama watu hawa wakipewa madaraka makubwa ya kushika dola itakuwaje kama madaraka ya kuongoza chama tu wanayatumia hivyo.

Nape allikuwa akiongea katika mahojiano na mtangazi wa TBC 1 asubuhi hii kwenye kipindi cha Jambo kinachorushwa na TBC1.

MT TAKE:
CCM waliwahi kujaribu kumfukuza nani uanachama katika siku za hivi karibuni?

ccm hafukuzwi mtu bali ukileta zako wana kukolimba fasta
 
mbona nape hamtaji tena lowasa majukwaani.au ndio vikao virefu vya kufukuzana? Au kasoma ishara za nyakati?
 
CCM kumfukuza Mwanachama ni process ndefu kwa kufupisha mchakato huo ni KumKolimba tu Mwanachama msaliti; Je ni ipi Nzuri kati ya taratibu hizo kwa Wasaiti.
 
Pumba.. Yule mbuge wa pemba aliyetoa maoni ya serikali tatu mlimfanyaje? Akili zenu hazina kumbukumbu eh?
 
Jamaniyeeeeeee!! Mangula alitoa miezi 6 waliopata nafasi kwa rushwa wajiondoe vinginevyo wataondolewa,,, MBONA KIMYA MPAKA LEO?
Au alidhani haitaisha? Honey moon yake bado!!

Nape ajibu hapa...
Gamba EL katimuliwa? Nini dhumuni la ziara yake ya Kumnanga EL na wale wenye Tuhuma za ufisadi ndani ya CCM?
 
Hapo amedanganya,ccm wanayo victimisation sometimes na ndo hii tabia ambayo chadema wanataka kuianza that's why tuikemee kwa nguvu

Mmmh ni tabia nzuri tu, tumeshindwa kuvikitimaizi mafisadi papa ila tunavikitimaizi watz kwa kuwajengea maisha magumu.
 
Jamaniyeeeeeee!! Mangula alitoa miezi 6 waliopata nafasi kwa rushwa wajiondoe vinginevyo wataondolewa,,, MBONA KIMYA MPAKA LEO?
Au alidhani haitaisha? Honey moon yake bado!!

Mkuu KakaJambazi kuwa mvumilivu si tumeambiwa utaratibu ni mreeeeeeeeefu....kwa hiyo CCM kwa sasa staili ni kula tu usiulize mpaka wa shamba kwani Utaratibu wa kujua mpaka ni mreefu kweli kweli
 
Jamaniyeeeeeee!! Mangula alitoa miezi 6 waliopata nafasi kwa rushwa wajiondoe vinginevyo wataondolewa,,, MBONA KIMYA MPAKA LEO?
Au alidhani haitaisha? Honey moon yake bado!!

Usisahau pia ile marufuku ya kuitwa "waheshimiwa" imeenda wapi?
 
Back
Top Bottom