Viongozi wengi wa CCM wanaiangalia jamii kwa hadhira ya udini, ukabila na ukanda, kwa hiyo kila chombo, kikundi, chama au hata ajira huwa wanaangalia kwa mtazamo huo. Mfano mzuri hata makundi yao ya urais yamejengwa kwa hadhira hiyo hiyo kama sio kundi la dini yetu basi litakuwa kundi la ukanda wetu. Sote tuliwasikia Uvccm wakisema rais ajaye hawezi toka Kaskazini.
Kwa stage waliyofikia viongozi wa CCM ukitembelewa na mtu wa kabila fulani lazima itajengwa hoja ya ukabila, Nape alipoona viongozi wa UKAWA Mbowe, Slaa na Mbatia wamekutana basi kwa vile mtazamo wake umejengwa kwa hadhira ya ukabila moja kwa moja ubongo wake uka conclude huo ni ubaguzi wa kikanda au kikabila bila kuangalia kilichopelekea kukutana bila wenzao.
Bila kujali kama anafanya haya kwa makusudi au kutojua huu ni upuuzi mkubwa anapanda mbegu mbaya sana na naweza kabisa kusema Nape ni mpuuzi kama wapuuzi wengine na anastahili kupuuzwa.