Nape Nnauye auvuruga upinzani SAUT tawi la Mwanza na kuwaambia UKAWA hakuna juisi ya bure Ikulu

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Mar 22, 2013
5,536
2,264
[video=youtube_share;6oejkH1DCz4]http://youtu.be/6oejkH1DCz4[/video]

Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amepeleKa ‘msiba' Kwenye vyama vya upinzani, baada ya kusomba wanachama wa vyama hivyo ambao wanaosoma katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (Saut), tawi la Mwanza, wakiongozwa na Rais wa Serikali ya Wanafunzi (Sautso), Philbert Saimon.


Wanachama hao ambao wengi ni wanachama wa CHADEMA waliamua kuhama chama hicho jana, katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Nyamalango, nje kidogo ya Chuo cha Saut, ambapo Nape alikuwa mgeni rasmi.

Akieleza sababu zilizomfanya ahame CHADEMA, Philbert Saimon alisema, "Tumepoteza muda mrefu kuwatumikia watu wasio na mwelekeo, watu ambao wamejaa uongo na ubabaishaji mwingi, wakati sisi tunahangaika, tunaacha masomo kwa ajili yao, watoto wao wanasoma vizuri, tumechoka kutumiwa, CCM ndio mpango mzima."

Vijana wengine walipohojiwa kwa nyakati tofauti walisema kwa muda sasa CCM imeanza kwa kasi kubwa kurekebisha upungufu uliokuwa ukikabili chama hicho na hivyo kuvutia wengi kuiamini na hili linayochangia kuua kabisa vyama vya upinzani nchini.

Nape kwa upande wake alisema: "Wenzangu walikuja hapa na talalila nyingi sana, leo nitajibu hoja moja baada ya nyingine na nitaanza na la changamoto za elimu."

Alisema mchakato wa ujenzi wa shule za sekondari za kata ulipoanza, wapinzani wengi walikejeli na kuzipa majina mbalimbali, lakini walioanza shule za sekondari za kata mwaka ule leo ndio wanamaliza vyuo vikuu nchini na wengine wako nje ya nchi.

Alieleza jinsi Serikali kwa kushirikiana na wananchi, inavyojenga maabara kwenye sekondari za kata na kupeleka walimu kwa mamia kila wilaya, ili kuboresha elimu nchini na kuwataka wananchi kupuuza wote wanabeza mafanikio hayo.

Kuhusu Kikundi kinachojiita UKAWA. Nape aliendelea kusisitiza msimamo wa CCM wa kutowabembeleza wajumbe hao kurudi katika Bunge Maalumu la Katiba, akidai ni kupoteza muda kwa watu wasiokuwa na nia njema ya kuhakikisha Katiba mpya inapatikana.

"Hawa wenzetu wamegeuza huu mchakato kama mchezo, kila wakigoma wanabembelezwa, wanapewa juisi Ikulu wanarudi bungeni, sasa wamegeuza mchezo, safari hii habembelezwi mtu, kama noma na iwe noma.

"Sheria ya mchakato Katiba mpya wameshiriki tukatunga wote, na sheria imeeleza wazi kuwa tutakuwa na awamu tatu kuu za kukamilisha mchakato wa Katiba mpya nchini.

"Awamu ya kwanza ni ya kukusanya maoni, awamu ya pili ni ya kujadili na kuyachambua maoni na awamu ya tatu ni ya kuipitisha kwa kupiga kura za maoni kwa wananchi. Asiyetaka kufuata utaratibu tuliojiwekea, hana nia njema na upatikanaji wa Katiba mpya," alisema Nape.

Nape alisisitiza kuwa hoja ya kuwa CCM haitaki Katiba mpya ni hoja mfu kwani aliyetangaza na kuanzisha mchakato ni Mwenyekiti wa Taifa wa CCM na Serikali ndiyo inayotoa fedha za kugharamia mchakato huo na kama CCM isingetaka Katiba mpya, isingefanya hayo yote.

"Hata mjadala wenyewe na utoaji wa maoni kwenye rasimu hakuna taasisi iliuchukulia kwa umuhimu mkubwa mchakato huo kuliko CCM, mpaka tumetoa maoni yetu kwa maandishi na machapisho kadhaa.

"Sasa wenzetu wanaounda genge la UKAWA wakati hata mmoja wao hana chapisho lolote zaidi ya ubabaishaji na kelele nyingi. Ndio maana wanafikia mahali wanadai muundo wa serikali tatu utadhibiti ufisadi nchini, nataka kujua serikali tatu inadhibiti vipi ufisadi? Si lazima kuwa na serikali tatu ndio udhibiti ufisadi," alisema Nape.

Nape alisisitiza kuwa UKAWA itasambaratika bila mkono wa CCM, na kuwa CCM hawana muda wa kuhangaika kusambaratisha upinzani kwani upinzani utajisambaratisha wenyewe kwa mbegu mbaya walizopanda na wanaendelea kuzipanda.

"Huwezi kupanda mahindi ukavuna uwele, kile unachopanda ndicho utakachovuna," alisema.

============================== =================
BAADHI YA PICHA ZA MKUTANO.


1.jpg

Wanachama wa Tawi la CCM SAUT wakiburudisha kwa kucheza na kuimba nyimbo mbali mbali.
3.jpg

Wanachama wa CCM SAUT wakionyesha ujumbe kutoka kwenye mabango
2.jpg

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wanachama wa Tawi la CCM SAUT Kambarage na wananchi wa Nyamalango wilaya ya Nyamagana, Mwanza ambapo aliwaambia kuwa CCM itaendelea kuongoza kwani ndio chama pekee nchini chenye sera na mipango inayoeleweka kwa wananchi huku ahadi zake zinatekelezwa kila kona ya nchi.
7.jpg

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akipokea kadi ya CHADEMA kutoka kwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha Mtakatifu Agustine Ndugu Simon Philbert Macheyeki ambaye amejiunga rasmi na CCM,katika mkutano huo zaidi ya wanafunzi 86 wa chuo hiko wamejiunga na CCM.
3.jpg

Kadi za wanachama wapya waliojiunga na CCM kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustine Mwanza.
8.jpg

Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha Mtakatifu Agustine, Ndugu Simon Philbert Macheyeki akiwa na wanachama wengine wapya wakila kiapo cha kujiunga na CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Nyamalango wilayani Nyamagana.
4.jpg

Wanachama wapya zaidi ya 420 wajiunga na CCM kutoka Chuo Kikuu cha SAUT.
1.jpg

Ujumbe kutoka kwa Tawi la CCM SAUT
10.jpg

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akisalimiana na baadhi ya wananchi na wanachama wa Tawi la CCM SAUT Kambarage Mwanza.
 
Kweli kipigo walichotoa green guards kitakuwa kimewavuruga kabisa wanafunzi wa SAUT!
 
Mkapa aliacha deni la taifa shilingi tril 7.kikwete kakopa tril 22 ambazo zingeweza kujenga barabara za kiwango cha daraja la kwanza km 22000.kikwete kajenga km 11000 za drj la 5 ambazo zitakufa zote baada ya miaka 5.hapo nape anasemaje?je tutakopa tena ili tukarabati hizi?au tutaanza kukusanya kodi ili tulipe deni? je malori yetu yatasitisha kazi au?na je kwa ukubwa wa ccm kuwa na watetezi wasiozidi 10 katika jukwaa makini kama jf ni afya kwa chama?
 
Aisee JF kiboko!!! Ni yuleyule Simon Philbert aliyetajwa mapema saa 24 kabla, na picha yake kuanikwa katika uzi wa Nicholaus Kilunga. Heeeee!!!!! CCM chama kikubwa, vipi kinaokota MAKOMBO??????
 
Njaaa tu.hivi hicho chuo wanafundisha nini? Na watu hapo naona kama mataira vile au macho yangu
 
Chuo cha SAUT ni aibu kwa vijana..ila mambo haya hawezi kufanya vyuo vya watu wanaojitambua..
 
"Hakuna juice ya bure Ikulu"ni kauli kweli inapaswa kutolewa na kiongozi wa kitaifa wa chama kikongwe kuliko vyote Africa CCM? MwanaDiwani hii ni kauli ya hovyo hovyo sana haipaswi kutamkwa na Nape
 
Last edited by a moderator:
Mkapa aliacha deni la taifa shilingi tril 7.kikwete kakopa tril 22 ambazo zingeweza kujenga barabara za kiwango cha daraja la kwanza km 22000.kikwete kajenga km 11000 za drj la 5 ambazo zitakufa zote baada ya miaka 5.hapo nape anasemaje?je tutakopa tena ili tukarabati hizi?au tutaanza kukusanya kodi ili tulipe deni? je malori yetu yatasitisha kazi au?na je kwa ukubwa wa ccm kuwa na watetezi wasiozidi 10 katika jukwaa makini kama jf ni afya kwa chama?
Big point.
 
Nape hawezi kuongea maswala ya msingi na mzito ya nchi hii..kaongea maswala ya juisi.. yaani mtu kama mbowe na lisu..wanaumaskini wa kukosa hela ya juisi mpaka wafuate ikulu...lisu au mbowe wakiacha siasa wana kazi za kwenda kufanya na kuishi popote pale duniani...nape akiacha siasa atafanya kazi gani km si atakufa njaa ana cv ya kuajiriwa popote au ana biashara yoyote iliyosimama kwa idea zake..mtu mwenye mawazo ya kimaskini ndo anaongelea juisi na vitu ka hizi..na mitoto ya saut inamsikiliza tu...nchi haiwezi kuendelea kwa watu kuongea siasa nyepesi kama za juisi za ikulu na misiba kuziweka ndo ajenda za kitaifa...kinana anajaribu kuwatoa huko kuongelea maendeleo na matatizo ya wananchi.. Lakini nape and cos wanarudi huko..
 
Ni Wenye akili finyu tu Mkuu TANGANYIKA KWANZA ambao ni buku 7 division 5 ambao wanaweza kusimama na kukipigia debe chama cha wahuni, mafisadi, magaidi na majangili. Mtu mwenye kujitambua kamwe hawezi kujihusisha chama kilichojaa walaghai wa hali ya juu kama hawa.

Mkapa aliacha deni la taifa shilingi tril 7.kikwete kakopa tril 22 ambazo zingeweza kujenga barabara za kiwango cha daraja la kwanza km 22000.kikwete kajenga km 11000 za drj la 5 ambazo zitakufa zote baada ya miaka 5.hapo nape anasemaje?je tutakopa tena ili tukarabati hizi?au tutaanza kukusanya kodi ili tulipe deni? je malori yetu yatasitisha kazi au?na je kwa ukubwa wa ccm kuwa na watetezi wasiozidi 10 katika jukwaa makini kama jf ni afya kwa chama?
 
Last edited by a moderator:
Mkapa aliacha deni la taifa shilingi tril 7.kikwete kakopa tril 22 ambazo zingeweza kujenga barabara za kiwango cha daraja la kwanza km 22000.kikwete kajenga km 11000 za drj la 5 ambazo zitakufa zote baada ya miaka 5.hapo nape anasemaje?je tutakopa tena ili tukarabati hizi?au tutaanza kukusanya kodi ili tulipe deni? je malori yetu yatasitisha kazi au?na je kwa ukubwa wa ccm kuwa na watetezi wasiozidi 10 katika jukwaa makini kama jf ni afya kwa chama?
Ndugu, Nani alikuambia kuwa na deni la taifa katika uchumi wa sasa ulimwenguni ni dhambi na haikubaliki?.

Kama unataka kuelewa mantiki ya hoja yangu, soma hii article ya BBC News (Business) kutoka UK.
Taken out of context, the numbers are staggering. The US has a total debt pile of almost $17 trillion (£10.6 trillion), which is expected to rise to almost $23tn in the next five years.

But how does that compare with other major economies?

Japan is not far behind, with current debts totalling $11.5tn. By any standards, these are big, big numbers.

And these countries are not alone - almost every major global economy has debts of more than a trillion dollars, according to the International Monetary Fund (IMF).

BBC News - How bad are US debt levels?
Fanya research kwanza kabla hujaweka vidole vyako kwenye keyboard na kuanza kulalamika.
 
Wewe jamaa ni -------- wa hali ya juu. Deni la Taifa linaongezeka wakati hatuoni faida yoyote ile kutokana na kuongezeka kwa deni hilo. Kila sekta nchini hali ni mbaya sana halafu unathubutu kuandika hapa eti kuongezeka kwa deni si dhambi!!!!! Sasa hili deni nini linasababisha kuongezeka ikiwa kila kitu nchini ni hovyo hovyo!!! Si elimu, matibabu, usafiri, huduma za maji/umeme, ajira, mishahara ya wafanyakazi duni. Jitambue badala ya kuandika pumba kila kukicha.

Ndugu, Nani alikuambia kuwa na deni la taifa katika uchumi wa sasa ulimwenguni ni dhambi na haikubaliki?.

Kama unataka kuelewa mantiki ya hoja yangu, soma hii article ya BBC News (Business) kutoka UK.

Fanya research kwanza kabla hujaweka vidole vyako kwenye keyboard na kuanza kulalamika.
 
Wanafunzi wamepotea njia tuu coz of giza, mwanga ukirejea watarudi njia kuu na hawatapotea tena.
 
Ndugu, Nani alikuambia kuwa na deni la taifa katika uchumi wa sasa ulimwenguni ni dhambi na haikubaliki?.

Kama unataka kuelewa mantiki ya hoja yangu, soma hii article ya BBC News (Business) kutoka UK.

Fanya research kwanza kabla hujaweka vidole vyako kwenye keyboard na kuanza kulalamika.
Acha ujinga wewe..inalinganisha na us..us inakopa maendeleo unayaona..serekali ya ccm inakopa maendeleo huyaoni acha kulinganisha linganisha tu
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Aisee JF kiboko!!! Ni yuleyule Simon Philbert aliyetajwa mapema saa 24 kabla, na picha yake kuanikwa katika uzi wa Nicholaus Kilunga. Heeeee!!!!! CCM chama kikubwa, vipi kinaokota MAKOMBO??????
Ninyi vijana wa BAVICHA kwa vile kwenu baadhi ya wananchi wanabaguliwa kifikra, kidini, kikanda na mnawaona kama POLITICAL TOOLS, basi mnadhani kuwa hata CCM ina fikra na mawazo kama yenu.

CCM hatuweki lebels kwenye nyuso za wanachama wake zilizoandikwa MAKOMBO. Hizo lebels endeleeni kuwa nazo kwa sababu katika chapa hizo, ubaguzi unawatafuna kwa sasa mpaka mmekimbilia kujificha kwenye mwanvuli wa kikundi cha UKAWA.
 
Mwambie huyu asiyejitambua!!! Anataka kufananisha kukopa kwa US na kukopa kwa Tanzania. US wanabana matumizi ya Serikali ili kupunguza budget deficit, Serikali hii dhalimu ya Tanzania lini ilichukua hatua zozote ili kupambana na budget deficit na hivyo kupunguza matumizi mbali mbali ya kifisadi yanayofanywa kila kukicha kama vile safari za nchi za nje zisizo na tija na kununua magari ya kifahari kila mwaka na ufisadi wa kutisha ambao hauchukuliwi hatua zozote!?

Acha ujinga wewe..inalinganisha na us..us inakopa maendeleo unayaona..serekali ya ccm inakopa maendeleo huyaoni acha kulinganisha linganisha tu
 
"Hakuna juice ya bure Ikulu"ni kauli kweli inapaswa kutolewa na kiongozi wa kitaifa wa chama kikongwe kuliko vyote Africa CCM? MwanaDiwani hii ni kauli ya hovyo hovyo sana haipaswi kutamkwa na Nape
Ndugu, hii ina maana kuwa, zama za kubembelezwa kwa sasa zimepita. Hata mtotot ana muda wa kubembelezwa.

Kuna mambo mengine ya maana na muhimu yanayohitaji kupatiwa ufumbuzi badala kuwabembeleza watu wazima ambao kwa msukumo na mapenzi yao waliamua kuondoka kwenye Bunge la Katiba na kwa msukumo na mapenzi hayo hayo watarudi wao wenyewe.

Bahati mbaya pia kwa sasa hakuna bajeti ya juisi na kawaha kwa kikundi cha watu wanaojiita UKAWA. Kama wanataka juisi na kawaha, haina budi walipie kutoka kwenye posho zao za vikao vya bunge Maalum.
 
Back
Top Bottom