Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 17,566
- 28,527
Nimeheshimu sana msimamo wa Nape Nnauye, kijana mdogo(kwangu) ambaye amesimamia si tu kauli yake bali hata kwa vitendo kuonyesha udhaifu uliotokea katika eneo lake na kuchukua hatua stahiki kulielezea, kuchunguza na hatimaye kama aivyosema , kukabidhi kwenye mamlaka husika.
Mtu kuwa mkweli, ni mpenzi wa Mungu.
Unafiki, woga wa kutumbuliwa hausaidii sana mbele ya ukweli.
Nape ameonyesha jinsi ambavyo amekuwa consistent katika suala zima linalo mkabili Makonda.
Kama tungekuwa na viongozi kama Nape, kutokubali kuwa waoga hata pale wanaofanya madudu katika maeneo yao ya utawala ni wakubwa, tungekuwa mbali kiuwajibikaji.
Vyeti feki vina eneo lake, wenye eneo hilo wako kimya kama maji ya mtungi, wanajitukanisha kwa kweli.
Hata leo, Nape aidha akiondolewa au kujiuzulu, mfano chanya utakuwa umewekwa katika uongozi wa Taifa.
Watu kama hawa huja kwa nadra.
Big up Nape Nnauye, mwana wa Moses.