Elineema J Mosi
JF-Expert Member
- May 17, 2013
- 808
- 148
Ndugu wana jf
Leo ni siku ya kwanza baada ya kikao cha wenye nchi kumalizika [yaani ccm] walikuwa wanajadili jinsi ya kututawala milele [mada ya kufa kwa ccm haitakaa iwe ajenda milele], najua Ndugu zangu Mh Mwigulu na Mh Nape sasa wanapata kikombe cha chai na mazagazaga ya kutosha huku wakiangalia simu zao aina ya Blackberry na kuperuzi issue tofauti [hivi unafikiri ukiwaambia kuwa yupo Mtanzania leo anakufa kwa njaa unafikiri watakusikiliza wakati wao meza imejaa na hakuna pa kuweka vitu, tena hiyo ni Asabuhi bado mchana na jioni].
Mashabiki wa ccm lazima waje na kejeli za aina yake [hizo mimi sizijali wala hazininyimi usingizi] kwani wanadhani kwao Tanzania hii wana hati miliki na wao ndio wanatakiwa watawale milele[Akili za mwendawazimu ndo huamini haya]. Machungu ya Watanzania yanazidi kupanda kila kukicha maana ccm ni kama UKOO WA PANYA kupata msafi ni hakuna wote ni wale wale tu.
Hebu tizama hizo picha kwa umakini wa hali ya juu, unaweza sema hawa ni watu wa aina mbili yaani mmoja yupo Tanzania mwingine yupo Ulaya, hadi watoto wadogo wamepoteza matumaini kabisa!!. Ukitizama Doctor aliyesoma zaidi ya miaka 7 baada ya kidato cha 6 leo hii posho yake kwa siku ni sh 10,000/= na Mbunge ni zaidi y ash 200,000/= kweli hapa kuna usawa!. Unajua lazima tuwe wakali na haya yanayotokea Tanzania ila tukiwaacha ccm wajifungie wenyewe ndani ya Bunge hakika wataiuza nchi [ kumbuka tu juzi juzi hapa walibaki wenyewe Bungeni na kuamua kuweka kodi ya simu card tena sh 1000 kila mwezi kwa mlala hoi ili tu wapate mahali pa kuchota wakiishiwa mifukoni mwao! [ni tama tu inawaendesha hakuna aliye na nia njema na mlalahoi wote ni wale wale tu!].
Lazima kila mwenye akili timamu awaandame ccm kwani nani mwenye Serikali? Ukiona kiongozi wa ccm awe mbunge, Waziri ama kiongozi wa kichama akikinyooshea kidole chama chochote cha upinzani na kudai ndo chanzo cha hali Fulani mbaya nchi ! hapo wenye akili kubwa tunajua anatafuta jinsi ya kukwepa Aibu hiyo [ hivi ndani ya nyumba Baba akisema no! nani atabisha?]sasa hawa Magamba wanajitetea nini? Wao watafune nchi hadi mifupa leo wanasingizia nini?.
Ndugu yangu mimi na wengi wenu ambao mnasoma hii thread tunahali mbaya[usibishe wakati hata mchana leo hujui ule nini?] na wenye nchi yao juzi juzi walikuwa Dodoma [kwani wewe ulialikwa? Kama haukualikwa jua wewe ni kibaraka tu ndani ya chama huna lolote mkuu (samahani ila natoa msisitizo tu) hivyo wao wakiamua wewe lazima ufuate ukikataa basi ni kipigo tu yaani utapigwa tu]. Hatuna budi kufanya maamuzi ya kujinasua kwenye hili ndimbi la umaskini wa kujitakia maana hakuna saye taka aishi vizuri sasa na uwezo wa kufanya hivyo tunao, hivyo basi sema NO NO NO NO NO kwa hawa wenye nia ya kutawala nchi hii milele. Kumbuka kuzaliwa maskini sio kosa kosa kufa huku ukiwa maskini na fursa zipo [Usilie mdau fanya maamuzi sasa haujachelewa!!!!!!?].
Asante, nawakilisha.
Leo ni siku ya kwanza baada ya kikao cha wenye nchi kumalizika [yaani ccm] walikuwa wanajadili jinsi ya kututawala milele [mada ya kufa kwa ccm haitakaa iwe ajenda milele], najua Ndugu zangu Mh Mwigulu na Mh Nape sasa wanapata kikombe cha chai na mazagazaga ya kutosha huku wakiangalia simu zao aina ya Blackberry na kuperuzi issue tofauti [hivi unafikiri ukiwaambia kuwa yupo Mtanzania leo anakufa kwa njaa unafikiri watakusikiliza wakati wao meza imejaa na hakuna pa kuweka vitu, tena hiyo ni Asabuhi bado mchana na jioni].
Mashabiki wa ccm lazima waje na kejeli za aina yake [hizo mimi sizijali wala hazininyimi usingizi] kwani wanadhani kwao Tanzania hii wana hati miliki na wao ndio wanatakiwa watawale milele[Akili za mwendawazimu ndo huamini haya]. Machungu ya Watanzania yanazidi kupanda kila kukicha maana ccm ni kama UKOO WA PANYA kupata msafi ni hakuna wote ni wale wale tu.
Hebu tizama hizo picha kwa umakini wa hali ya juu, unaweza sema hawa ni watu wa aina mbili yaani mmoja yupo Tanzania mwingine yupo Ulaya, hadi watoto wadogo wamepoteza matumaini kabisa!!. Ukitizama Doctor aliyesoma zaidi ya miaka 7 baada ya kidato cha 6 leo hii posho yake kwa siku ni sh 10,000/= na Mbunge ni zaidi y ash 200,000/= kweli hapa kuna usawa!. Unajua lazima tuwe wakali na haya yanayotokea Tanzania ila tukiwaacha ccm wajifungie wenyewe ndani ya Bunge hakika wataiuza nchi [ kumbuka tu juzi juzi hapa walibaki wenyewe Bungeni na kuamua kuweka kodi ya simu card tena sh 1000 kila mwezi kwa mlala hoi ili tu wapate mahali pa kuchota wakiishiwa mifukoni mwao! [ni tama tu inawaendesha hakuna aliye na nia njema na mlalahoi wote ni wale wale tu!].
Lazima kila mwenye akili timamu awaandame ccm kwani nani mwenye Serikali? Ukiona kiongozi wa ccm awe mbunge, Waziri ama kiongozi wa kichama akikinyooshea kidole chama chochote cha upinzani na kudai ndo chanzo cha hali Fulani mbaya nchi ! hapo wenye akili kubwa tunajua anatafuta jinsi ya kukwepa Aibu hiyo [ hivi ndani ya nyumba Baba akisema no! nani atabisha?]sasa hawa Magamba wanajitetea nini? Wao watafune nchi hadi mifupa leo wanasingizia nini?.
Ndugu yangu mimi na wengi wenu ambao mnasoma hii thread tunahali mbaya[usibishe wakati hata mchana leo hujui ule nini?] na wenye nchi yao juzi juzi walikuwa Dodoma [kwani wewe ulialikwa? Kama haukualikwa jua wewe ni kibaraka tu ndani ya chama huna lolote mkuu (samahani ila natoa msisitizo tu) hivyo wao wakiamua wewe lazima ufuate ukikataa basi ni kipigo tu yaani utapigwa tu]. Hatuna budi kufanya maamuzi ya kujinasua kwenye hili ndimbi la umaskini wa kujitakia maana hakuna saye taka aishi vizuri sasa na uwezo wa kufanya hivyo tunao, hivyo basi sema NO NO NO NO NO kwa hawa wenye nia ya kutawala nchi hii milele. Kumbuka kuzaliwa maskini sio kosa kosa kufa huku ukiwa maskini na fursa zipo [Usilie mdau fanya maamuzi sasa haujachelewa!!!!!!?].
Asante, nawakilisha.