Kijiti cha uyole.....majani..
Alisema, baraka hizo za Mbowe kwa mwaka zinasababisha Taifa kupata hasara ya Sh. milioni 25 na kwa kuwa watendaji wengine wa Chadema pia wanalipwa posho badala ya mishahara, kwa ujumla wanaliingizia Taifa hasara ya Sh. milioni 487.
Alifafanua kuwa, fedha hizo ambazo ni hasara hiyo inayosababishwa na Chadema kugeuza mshahara kuwa posho ili isilipwe kodi wakati wafanyakazi wengine wote wanatozwa kodi, zingeweza kununua vitabu vya Sayansi 48,000 kwa sekondari nchini na madawati mengi.
...
HALI ILIVYO NDANI YA CCM KIUCHUMI NI KIOO AU TASHWIRA YA YALIOMO SERIKALINI.Really?
Najilazimisha kuamini kuwa mdogo wangu huyu ana uchungu kweli na upotevu wa fedha za umma na kuwa kipimo hiki anchokitumia ataanza kukitumia kwenye PPF, ATCL, n.k na atatoa pendekezo kuwa posho na mishara ya Wabunge ipunguzwe kwa asilimia angalau 30 halafu tuone ni kiasi gani cha fedha tutaokoa halafu tukiziokoa tutafanya nazo nini.
Huyu dogo ana matatizo gani? Ameambiwa akitaka kukoga nyoyo za watanzania aeleze ni jinsi gani serikali ya CCM inatekeleza ilani ya uchaguzi. Hii ya kuiimba Chadema as if CCM ndio chama cha upinzani haina mshiko hata robo na wala haitasaidia kurudisha mapenzi yaliyopotea kwa CCM. Just wasting his time for nothing!!!!
Tiba
Mkuu kumuita mjinga pia unampa cheo huyu jamaa ni zaidi ya mjinga!Nape anafikiri kuwa WaTZ ni karunguyeye kama wale wazee wa ccm ! Eti pinda anaishi maisha rahisi , yapi ? Mshahara zaidi ya 15 m. ! Mjinga huyu kijana.
Mkuu umeongea ukweli mtupu, nakugongea thanx kabisa! Hawa watu cku yao inakaribia!Hivi huyu Nape kaishia vidudu nini? Ni vitabu vipi 48,000 vya sayansi vinavyoweza kununuliwa kwa sh 487,000,000 (kwa wastan wa kila kitabu sh 10,145.83) na hela ikabaki kwa ajili ya madawati? Vitabu tu vya mitaala vya shule ya msing kimoja kinauzwa sh 10,000 mpaka 15,000 (aende bookshop za Mtaa wa Samora aulizie). Vitabu vya sayansi kwa O-Level kama Lambert, Abort, Nelcon, etc vinauzwa zaidi ya sh 50,000.
Au kwa sababu watoto wake wanasoma international schools/au nje ambako kila mtoto anapata vitabu hapohapo shuleni?
Au kwa sababu anapata mishahara mitatu (DC, Katibu Mwenezi, na kutoka kwa Mafisadi) na hivyo ye akinunua kitabu kwa sh 100,000 anaona kama ametoa sh 10,000 tu?
Au kwa sababu anajua anaongea na watu ambao serikali yake imewanyima elimu na hivyo hawaelewi hata akisema vitabu vya sayansi ni nini na viauzwa bei gani (angejaribu kutumia idadi ya madawati akaona jinsi atakavyopingwa kwa sababu hata mwananchi wa kawaida anaijua hesabu yake)?
Mwacheni aendelee kuudanganya uma, anasahau kwamba sasa watu wameelevuka na watatumia hesabu hiyo hiyo kuthaminisha ni vitabu vingapi vya sayansi vingeweza kununuliwa na fedha ya Epa (zaidi ya sh 130,000,000,000), Kagoda (Zaidi ya sh 40,000,000,000), Dowans (Zaidi ya sh 94,000,000,000), Kiwira (sikumbuki ni bil ngapi), Na hizi za kunyanyua makampuni ya pamba yaliyoathirika na mtikisiko wa uchumi duniani (sh 48,000,000,000) na zingine nyingi wanazoiba kwa kushirikiana na Barick na migodi mingine?
Tutaikomboa nchi yetu kutoka mikononi mwa madhalimu, walanguzi, wala rushwa na wanyanyasaji wa haki za kibinadamu (walioko tayari kuona damu ya binadamu wenzao ikimwagika na wao wanaendelea kuinjoi madaraka, wanatufanya sadaka na kafara za utajiri wao).
Na siku tukijikomboa, wachimbe makaburi yao wenyewe wajizike kabla sisi hatujawafikia.
Alifafanua kuwa, fedha hizo ambazo ni hasara hiyo inayosababishwa na Chadema kugeuza mshahara kuwa posho ili isilipwe kodi wakati wafanyakazi wengine wote wanatozwa kodi, zingeweza kununua vitabu vya Sayansi 48,000 kwa sekondari nchini na madawati mengi.
Alisema mambo ya CCM ni ya kimungu, ndiyo maana Watanzania wameendelea kukiamini na kukipa ridhaa ya kuongoza nchi kwa amani na utulivu.
Source: Habari Leo
Nape ni bogusi sana ingawa nilikuwa na matumaini naye wakati akigombea madaraka ndani ya CCM. Baada ya kupata madaraka hayo ameonyesha rangi zake halisi kuwa hakuna mwana-CCM mwenye akili. Vile vile kila ninapoona picha zake naona kama vile anazeeka kimaumbile kwa kasi ya haraka sana, inawezekana na akili zake pia zinazeeka haraka sana.
Njia anayotumia ya kujenga chama chake ni kuwa (a) anakubali kuwa chama chake hakifai kama ambavyo CDM wanavyosema, (b) anashambulia CDM kuwa nao hawafai zaidi kuliko CCM. Hiyo siyo njia nzuri ya kujenga chama cha kisisasa, kwani kama atafanikiwa basi wananchi wanaweza wakahamia chama kingine zaidi ya CCM na CDM. Ninamtegemea aje na hoja za kuonyesha kwa nini watu waipende CCM siyo atuambie kwa nini watu wasiipende CDM.