Napata hofu Juu ya hili!

Napata hofu Juu ya hili!

nani alikudanganya mkuu??

Habari zenu wana-MMU!!

Kwanza natanguliza pole zangu kwa wale wote waliofikwa na maafa ya mafuriko na hata wengine kupoteza maisha!! Nasema poleni sana!

Back to the topic,.

Nimekuwa kwenye mahusiano na mpenzi wangu kwa mwaka sasa,. Yeye yupo Dar na mimi nipo nje ya Dar kimasomo, na yeye pia ni mwanafunzi wa chuo!!

Wakati niliporudi likizo nilimwambia huyu mpenzi wangu akapime afya yake kabla hatujashiriki tendo baada ya kuhakikisha mimi sina tatizo,.

Alienda kwenye hospitali moja hapahapa Jijini Dar inaitwa IMTU akaambiwa yupo salama ila arudi baada ya miezi mitatu kupima tena ili kupata uhakika,.

Nilipokutana na huyu mpenzi wangu nikamuuliza majibu vipi?? Akanijibu hawatoi majibu mpaka mtu apime mara 3 ndiyo wanatoa majibu,.

Kwa kuwa nilimuamini huyu mpenzi wangu nilimuelewa tukala tunda la mti wa kati!! Ila baadae nimekuja kujihoji maswali mengi kwamba inawezekana kweli asipewe matokeo ya vipimo vyake? Au alidanganya?? Wakuu nilitumia mpira maana UKIMWI hatari!!
 
wacheni kumlaumu huyu kijana ni wangapi mmepima hapa au mnaongea utapewaje majibu ya vvu kwa kupima mara moja mm mwenye nilienda kupima mara ya kwanza wakanijibu kua nipo salama ila siwezi kupewa majibu cha msingi mumwambie waende wote kuhakikisha sio kila mtu kupima kivyake ila suala la kusema kua hakupewa majibu kwa kupima mara moja ni kweli!
 
Back
Top Bottom