Naombeni ushauri

Mie huwa naamini matatizo katika ndoa 98% yanachangiwa na wanawake-hii story ni ya upande mmoja but mie naamini wewe ndio tatizo.
Wanaume bhn
mnajionaga malaika we ushaambiwa MTU anakunywa pombe analewa na matusi toka akiwa na miaka 9 afu useme shida ni mwanamke isitoshe mwanamke anakaa ukweni Hadi mama mkwe anajua tabia ya Mwanae huyo dada kachangiaje matatizo ya huyo mwanaum
 
MTU hawezi kutoka tu huko kwenye mapombe amwage sufuria la mboga,itakiwa kuna kitu umemkosea au umemjibu vibaya au umepika mboga hivyo lazima kuna sababu
Hujawahi kuishi na walevi nini
Hana sababu ya kufanya kitu akijiskia anafanya chochote anaweza hata kukupiga mpk akuue akachanganya na wanae tuulize Sisi Baba zetu walikua wanatupiga wakishalewa hata kosa hujui umefanya nn
 
Nawatoto wawili
, hebu tumpe ushauri mujarabu laasivyo atakujafanywa mdangaji. Kwauchumi huu, utakubali uletewe watoto wawili au mama awaache wanae
kweli.
 
Wanaume wa hivyo ukiondoka anadata. Jipe likizo ili ajitafakari. Ila uwe tayari kwa lolote anaweza asishtuke ukiondoka.
Na ukweli ni kwamba hatabadilika so akili kichwani mwako.
Huu ushauri naukubali ila kumwambia mtu straight kuwa aondoke waachane huku anataka akiondoka awabebe wote wawili baafae simtaanza kumuita majina ya ajabu mnayoyadhihaki kila siku humu. Tutengeneze kwanza ikishindikana ndio usepe. Watoto wawili
, mnaona uchumi wa babu zetu uu
 
Huoni kalichangia tatizo lake mwenyewe
, yaani unajua mtu ni mlevi chronic tangu anamiaka 9 na still anaishi kwao sasa kilichokupeleka uzae na kuishi naye nini.
mama yangu mzazi angekuzaba kofi balaa na mzee angekufukuza kabisa. Yaani yote hayo uliyajua na still ukajipiga kifua kuwa unaweza
, unaona kweli ni haki yako kutafuta huruma kabisa
 
Still haiprove kwamba mwanamke ndo mwenye makosa hakuna wa kumlaumu mwenzie
 
Still haiprove kwamba mwanamke ndo mwenye makosa hakuna wa kumlaumu mwenzie
Yaani atalaumiwa mpaka kesho maana ulionywa ukaziba masikio. Asiyesikia la mkuu huvunjika guu. Kuna wale ambao ulevi huuanza katikati uko mimi huyo mwanamke sitamlaumu ila wewe uliyejua picha yote, 😂😂 my sister that's on you. Ulipewa akili zitumie, sio utumie hisia. Yaani mimi nioe binti aliye malaya aliyekubuhu leo, kesho akichepuka nisilaumiwe😂😂😂 that's illogical. Hatupo kwenye telenovela au fantasies humu bali ni reality. Mmewezeshwa hadi na elimu yote ila bado ubebewe makosa ya kujitakia, nope. Grow up and take accountability.
 
Mzee wao ni wao kuna la kujifunza hapa
 
Aondoke wajipe muda, why kubembeleza? Kuna watu wanafanya makosa kwa makusudi kabisa sio kwamba hawatambui nini wanafanya.
Halafu hata hawajaoana rasmi...why kubeba mzigo wa mtu asiyekuthamini.?
Na asipoangalia huyo dada atakuja
kuachwa mchana kweupee.

Aondoke kama anaweza kujitegemea maana wadada wengi wanavumilia shida kwasababu ya pesa za mume na sio kingine.
 
Kabla alikuwa na tabia hizo au zimejitokeza tu.
Kabla ya kuondoka tafuta tiba hakuna kisichoshindikana
 
Yanajengeka yeye sio wa kwanza utakimbia wangapi,kila mmoja ana matatizo,labda usiolewe
 
Yanajengeka yeye sio wa kwanza utakimbia wangapi,kila mmoja ana matatizo,labda usiolewe
Huo ndo ushauri wangu mimi akifata ushauri wako ni sahihi pia. Kupanga ni kuchagua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…