Naombeni ushauri nifanye nini?

NGANYIKA

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2015
Posts
204
Reaction score
161
Mke wangu katoka kuniona hospitali nimelazwa. Nilimpa nauli ya daladala kwenda nyumbani ambapo angetumia saa moja tu. Angetembea kwa miguu angetumia saa mbili.

Lakini pamoja na kumpa nauli ametumia saa nne toka saanane na nusu hadi saa kumi na mbili na nusu. Nikimpigia simu kuuliza alikuwa wapi?Anakata simu.Nikipiga simu tena anabadili mazungumzo nakuegemea kwa watoto. Nikiuliza tu alikuwa wapi anakata simu.

Naomba ushauri wenu
 
Kuna mshikaji kajitolea kukulindia familia yako kuna ubaya gani wakati huu ukiwa unaumwa,wewe angalia kwanza afya yako usije kufa bure kwa presha.
 
unaumwa nn?..uenda tatizo lipo hapo
 
Uwe mpole mkuu. Hapo ulipo u mdhaifu na wahitaji msaada wa mwenzio. Mshukuru Mungu taarifa za maendeleo ya wanao unapata. Muombe MUNGU akuinue hapo kitandani.
 
Mkeo alipitia kwangu,unalalamika nini sasa?
 
hawa wanawake mnaowalea hivi mnawatoa wapi?
ina maana mkeo hana hata kashughuli kadogo ka kumfanya apate hata nauli!!
yaani mtu aje hospital wewe mgonjwa ndio utoe nauli ya yeye kurudia nyumbani!!
una hatari wewe, yawezekana alipitia kutafuta hela za chakula cha kukuletea.
 
kwa hiyo JF umeingia upo wodini?! .......... nakushauri ukitaka kupona haraka uhudhurie na jukwaa la siasa.
 
Simu itakupeleka ICU sasa hivi. Achana nayo hadi upone
 
Inawezekana kajua unachoumwa na inamfanya ashindwe kuongea na wewe,jali afya yako kwanza mengine yatafuata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…