lucky lefty
JF-Expert Member
- Feb 16, 2017
- 491
- 454
Habarini wakuu,
Nina msichana wangu mmoja tulianza nae mahusiano toka 2013, katika maisha ya mapenzi baina yetu kuna kipindi cha kati hapo tukagombana, ikabidi kila mmoja akaendelea na ishu zake.
Sasa yeye mwenzangu katika kipindi hicho tulichoachana akatoka na lijamaa huko akapewa kibendi, Mungu akamjaalia akajifungua mtoto wa kiume. Katika kipindi chote toka alipopata ujauzito jamaa aliyempa kibendi alikataa kuhudumia mpaka mtoto alipozaliwa.
Mara baada ya kujifungua huyu msichana akaanzisha tena mahusiano na jamaa aliyemtoa usichana (huyu siye aliyempa kibendi), katika mahusiano yao sijui kilichoendelea lakini niliskia waliachana.
Katika shida shida za utawala huu wa mjomba magu huyu msichana akanitafuta last year and tuka reconcile so akawamsichana wangu tena. Tatizo lilikuja alipotaka nimuoe, mimi sikuwa na tatizo sema kama mtu ninaejielewa ikabidi nifanye uchunguzi (sikutaka kuingia kichwakichwa kwenye ishu za ndoa) kama hana mchepuko huko alipo na ndio hapo nilipojua anatoka na lijamaa lake la zamani.
Ushahidi nilikuwa nao wa kutosha kuanzia messages hadi baadhi ya siku huwa anaenda kulala kwa mchizi, sasa nilipo mconfront kama najua anamchepuko na najua huwa analala kwa mchizi baadhi ya siku msichana alinijia juu kwa maneno mengi akataka tuachane, tatizo sikuwa na nia ya kumuacha ilikuwa tuongee tuyamalize lakini mwenzangu akawa analazimisha tuachane, sasa katika marumbano mimi nikaona isiwe tabu tukapigana chini.
Sasa cha kushangaza jioni yake baada ya kuachana akanitumia message kuniomba msamaha kwa alivyokuwa ananijibu na hataki tuachane kwa hasira, nikamwambia nimemsamehe.
Sasa hapa nipo dilema maana msichana nampenda na yeye ana feelings nasema hivi kwa sababu tunakaa mikoa jirani na kila nikiwa na shida naye nikimpigia aje kesho jua lazima atatia maguu gheto, sijawahi kumwambia aje akazingua au akagoma au akaleta kisingizio cha kutokuja.
Na hata kesho nikimwambia aje huku nilipo atakuja ingawa tumeachana, tatizo hataki kukiri makosa yake na hataki hata kusikia ushahidi niliokuwa nao.
Naombeni ushauri wakuu nimpotezee kimoja au niwe mvumilivu nishee na mchizi?
Nina msichana wangu mmoja tulianza nae mahusiano toka 2013, katika maisha ya mapenzi baina yetu kuna kipindi cha kati hapo tukagombana, ikabidi kila mmoja akaendelea na ishu zake.
Sasa yeye mwenzangu katika kipindi hicho tulichoachana akatoka na lijamaa huko akapewa kibendi, Mungu akamjaalia akajifungua mtoto wa kiume. Katika kipindi chote toka alipopata ujauzito jamaa aliyempa kibendi alikataa kuhudumia mpaka mtoto alipozaliwa.
Mara baada ya kujifungua huyu msichana akaanzisha tena mahusiano na jamaa aliyemtoa usichana (huyu siye aliyempa kibendi), katika mahusiano yao sijui kilichoendelea lakini niliskia waliachana.
Katika shida shida za utawala huu wa mjomba magu huyu msichana akanitafuta last year and tuka reconcile so akawamsichana wangu tena. Tatizo lilikuja alipotaka nimuoe, mimi sikuwa na tatizo sema kama mtu ninaejielewa ikabidi nifanye uchunguzi (sikutaka kuingia kichwakichwa kwenye ishu za ndoa) kama hana mchepuko huko alipo na ndio hapo nilipojua anatoka na lijamaa lake la zamani.
Ushahidi nilikuwa nao wa kutosha kuanzia messages hadi baadhi ya siku huwa anaenda kulala kwa mchizi, sasa nilipo mconfront kama najua anamchepuko na najua huwa analala kwa mchizi baadhi ya siku msichana alinijia juu kwa maneno mengi akataka tuachane, tatizo sikuwa na nia ya kumuacha ilikuwa tuongee tuyamalize lakini mwenzangu akawa analazimisha tuachane, sasa katika marumbano mimi nikaona isiwe tabu tukapigana chini.
Sasa cha kushangaza jioni yake baada ya kuachana akanitumia message kuniomba msamaha kwa alivyokuwa ananijibu na hataki tuachane kwa hasira, nikamwambia nimemsamehe.
Sasa hapa nipo dilema maana msichana nampenda na yeye ana feelings nasema hivi kwa sababu tunakaa mikoa jirani na kila nikiwa na shida naye nikimpigia aje kesho jua lazima atatia maguu gheto, sijawahi kumwambia aje akazingua au akagoma au akaleta kisingizio cha kutokuja.
Na hata kesho nikimwambia aje huku nilipo atakuja ingawa tumeachana, tatizo hataki kukiri makosa yake na hataki hata kusikia ushahidi niliokuwa nao.
Naombeni ushauri wakuu nimpotezee kimoja au niwe mvumilivu nishee na mchizi?