Jt jr
Senior Member
- Feb 3, 2012
- 181
- 57
Jamani kuna msichana nilimtongoza nikiwa shule ya msingi lakini hatukufika mwafaka kwa kuwa tulivyomaliza shule kila mtu aliendelea na secondary na hatukuwa na mawasiliano kila mtu akawa na issue zake. Baadae alitafuta namba yangu ya cm nikiwa form5 nikawa naye kwa mda lakini baadae tuliachana kwa kile alichodai kuwa simjali, ila ni kwa sababu ya shule. Alirudia kunitafuta nilipomaliza form6 tukaka tukaongea mengi akaniweka wazi kuwa ana mtoto teyari na aliyezaa nae mtu mwenye mke, anadai ilitokea bahati mbaya na mtoto alichukuliwa na babake, nikiwa chuoni amenitafuta tena tukawa tunachart akanielezea stori zake zote na wanaume aliokuwa nao yeye akadai ilikuwa ni harakati ya kumtafuta anayemfaa maishani. kaniambia ananipenda, na Akaahidi hatarudia ujinga wake wa nyuma nikambadilishia na laini ya cm, mpaka sasa tunapanga tuje kuoana. Ila najiuliza itakuwaje?na huku teyari ana mtoto ingawa alichukuliwa na baba yake, kitu kingine nalingana naye umri. Naombeni ushauri wenu wanajamii km ni busara kuwa nae.