Naombeni ushauri kwa hili

Keyzer Soze

Member
Dec 30, 2016
27
22
Habarini wana jamvi? Nina mwaka na nusu sasa tangu nifunge ndoa na sasa tuna mtoto wa kiume ana miezi mitatu,sasa kabla hatujapata mtoto mke wangu alikuwa anabehave kama malaika vile kitu utakachomwelekeza anakuelewa poa sana na sehemu ambayo anaona amekosea atarud chini yanaisha, sasa issue imekuja baada ya kupata mtoto cuz kipindi cha mimba alikuwa na wivu uliopitiliza tofauti na mwanzo,mpaka nkahisi anajifanyisha muda mwingine na ugomvi mkubwa ulikuwa kuhusu simu ambayo mwanzoni alikuwa anaishika lakini anabehave anapokuwa nayo na evidence zote ambazo nlikuwa naona zitamkwaza nafuta mapema tu,lakini sasa hv imefikia mpaka nambadilishia password basi hapo atatuna wiki nzima, nikimwonesha napo inakuwa tabu anaweza kuanzisha chat na mtu akijifanya ni mm saa nyingine hata wale watu wangu wa msingi akimaliza anafuta (hili nilithibitishiwa na watu wanne tofauti like jana mbona sikuelewa unaongelea nn! Nauliza jana tulichat kwan, ndio mtu anakuonesha text zako ambazo katuma wife), na katabia kingine utakuta keshajiweka dp wakati na yeye anasimu yake,na sio kama simuwekagi muda mwingine unakuta anaweka picha like kama za kichokozi na status za kimbea, anabaki anasikilizia kuangalia kwenye cm yake kama ntabadilisha dp yangu,nikibadili mzozo na juzi kilichoniboa kaanzisha chati na kiongozi wangu ofisini ambae namuheshimu sana kwanza kanizidi umri,na hizo chat yeye anaweza anzisha na namba yyte akijisikia yule mother alihisi sio mimi baada ya siku kadhaa akaniita akanambia na kunionesha sms, ikabidi niwe mpole nimwambie hizi kasumba za wife,niliporudi nkamwelezea alichokifanya kwamba hakijanipendeza na nilishawahi kumuonya cha kushangaza basi kajinunisha,huyo mtoto ndio anatumika kama kigezo hapo ntanyimwa hata kumgusa,basi ikabidi niwe mpole,baada ya muda naangalia status yake kaandika "Siui mende kwa nyundo" yani niliona moja kwa moja unanihusu na anajifanyisha makusudi.

Naombeni ushauri wenu ndugu zanguni yani home pamekuwa si sehemu salama ya kuwahi kurud ukitoka kazini.
 
Utoto unakusumbueni, kwa mwanaume rijali aliyekomaa tena baba wa familia hawezi kuruhusu UJINGA wa mke kumuendesha kama gari bovu kiasi cha kufikia hatua ya kuchart na watu kwenye simu ya mumewe. Simu yangu haina password lkn mke wangu hawezi kutuma sms kwa namba za simu zilizomo, sio heshima, hana adabu mkeo na usipoikomesha tabia hiyo mapema itakugharimu kwakuwa unaiweka ndoa yako matatani
 
Duuuh pole sana,,,lakin kwa nn ana wivu?? Kitu gan kinamfanya azidishe wivu baada ya kupata mtoto?tabia yako ipoje mpka anashindwa kukuamin sasa tofauti na mwazo?? Aisee kuna kitu kikubwa sana kinaweza kutokea,,kukuharibia kaz,kukuharibia mahusiano yako na watu na mbaya zaid bila wewe kutarajia... Hebu rename jina la baba yako au baba yake au mama yake andika neno la demu halaf aanzishe chat zake baadae ndio inakua ushahidi mzur kwako,
 
Wanawake huwa wko ivo kwenye ndoa changa sasa ni juu yako kuwa na msimamo nina hutaki na nini unataka ni kipindi kigumu cha kuweza kujuana Tabiazenu kiuhalisia kuwa makini ndoa changa hufa sana kipindi hiki maana mwanamke hamuanini kabisa Mume ni kwa sababu analea anajua unaweza kuchepuka
 
Habarini wana jamvi? Nina mwaka na nusu sasa tangu nifunge ndoa na sasa tuna mtoto wa kiume ana miezi mitatu,sasa kabla hatujapata mtoto mke wangu alikuwa anabehave kama malaika vile kitu utakachomwelekeza anakuelewa poa sana na sehemu ambayo anaona amekosea atarud chini yanaisha, sasa issue imekuja baada ya kupata mtoto cuz kipindi cha mimba alikuwa na wivu uliopitiliza tofauti na mwanzo,mpaka nkahisi anajifanyisha muda mwingine na ugomvi mkubwa ulikuwa kuhusu simu ambayo mwanzoni alikuwa anaishika lakini anabehave anapokuwa nayo na evidence zote ambazo nlikuwa naona zitamkwaza nafuta mapema tu,lakini sasa hv imefikia mpaka nambadilishia password basi hapo atatuna wiki nzima, nikimwonesha napo inakuwa tabu anaweza kuanzisha chat na mtu akijifanya ni mm saa nyingine hata wale watu wangu wa msingi akimaliza anafuta (hili nilithibitishiwa na watu wanne tofauti like jana mbona sikuelewa unaongelea nn! Nauliza jana tulichat kwan, ndio mtu anakuonesha text zako ambazo katuma wife), na katabia kingine utakuta keshajiweka dp wakati na yeye anasimu yake,na sio kama simuwekagi muda mwingine unakuta anaweka picha like kama za kichokozi na status za kimbea, anabaki anasikilizia kuangalia kwenye cm yake kama ntabadilisha dp yangu,nikibadili mzozo na juzi kilichoniboa kaanzisha chati na kiongozi wangu ofisini ambae namuheshimu sana kwanza kanizidi umri,na hizo chat yeye anaweza anzisha na namba yyte akijisikia yule mother alihisi sio mimi baada ya siku kadhaa akaniita akanambia na kunionesha sms, ikabidi niwe mpole nimwambie hizi kasumba za wife,niliporudi nkamwelezea alichokifanya kwamba hakijanipendeza na nilishawahi kumuonya cha kushangaza basi kajinunisha,huyo mtoto ndio anatumika kama kigezo hapo ntanyimwa hata kumgusa,basi ikabidi niwe mpole,baada ya muda naangalia status yake kaandika "Siui mende kwa nyundo" yani niliona moja kwa moja unanihusu na anajifanyisha makusudi.

Naombeni ushauri wenu ndugu zanguni yani home pamekuwa si sehemu salama ya kuwahi kurud ukitoka kazini.
Mkuu huyo kwanza kabisa ni mpitaji sio mke wako huyo na kama ni mke wako mwambie live bila chenga hiyo tabia aiache mara moja si nzuri hata kidogo.
 
Utoto unakusumbueni, kwa mwanaume rijali aliyekomaa tena baba wa familia hawezi kuruhusu UJINGA wa mke kumuendesha kama gari bovu kiasi cha kufikia hatua ya kuchart na watu kwenye simu ya mumewe. Simu yangu haina password lkn mke wangu hawezi kutuma sms kwa namba za simu zilizomo, sio heshima, hana adabu mkeo na usipoikomesha tabia hiyo mapema itakugharimu kwakuwa unaiweka ndoa yako matatani
Tulishakuwa kwenye uhusiano miaka miwili na kitu na alikuwa mtu mmoja understanding sana,na nilishawafata hadi kaka zangu kiimani lakin wengi kwenye ushauri wao wanasema ni kipindi cha mpito,kila mimba huja na mambo yake nakuwa mpole nisimpe tabu yeye na kijana wangu,
 
Tulishakuwa kwenye uhusiano miaka miwili na kitu na alikuwa mtu mmoja understanding sana,na nilishawafata hadi kaka zangu kiimani lakin wengi kwenye ushauri wao wanasema ni kipindi cha mpito,kila mimba huja na mambo yake nakuwa mpole nisimpe tabu yeye na kijana wangu,
Kwa nilivosoma nikaelewa ni kwamba ameshajifungua mtoto, kumbe ana mimba?
 
Kwa nilivosoma nikaelewa ni kwamba ameshajifungua mtoto, kumbe ana mimba?
Ameshajifungua lakin katika kutaka ushauri wanasema kila mimba huja mambo yake ndio maana wananiambia ni kipindi cha mpito cuz ana mtoto as long as amejifungua na bado mtoto ni mdogo ndio ana miezi yaenda mitatu now,lile zengwe la mimba linakuwa linamtoka.
 
Ameshajifungua lakin katika kutaka ushauri wanasema kila mimba huja mambo yake ndio maana wananiambia ni kipindi cha mpito cuz ana mtoto as long as amejifungua na bado mtoto ni mdogo ndio ana miezi yaenda mitatu now,lile zengwe la mimba linakuwa linamtoka.
Wanakufundisha mambo ya kipuuzi mkuu. Komesha tabia mbaya hiyo kabla haijakuharibia ndoa yako. Haiingii akili ni mkeo kuwatumia watu wako sms hadi mabosi wako inaingiliana vp na kujifungua kwake? Anyway ni ndoa yako ww na mkeo na ww ndiye baba wa familia
 
Mkuu kwanza pole sana kwa hilo.
Ni kweli yawezekana labda ni kipindi cha mpito kilichoanzia kwenye ujauzito hadi kujifungua kwake.
Inawezekana ikawa ni tabia ambayo imejijenga kutokana na mazoe na mambo anayoyasikia kutoka kwa wenzake kuwa mke akiwa katika kipindi kama hicho mume huchepuka.
Lakini pia anafanya hayo makusudi ili yeye awe ndie mwenye mamlaka na kauli ya mwisho hapo nyumbani.
Wengi wa wanawake kwa sasa wanatabia ya kupenda kuwatawala waume zao. Mwanzo asingeweza kufanya hivyo kwa kuwa hakuwa na kitu cha kumkinga ila kwasasa kipo ambacho ni mtoto wako, hata wewe umekili hapa kuwa unahofia kumpa tabu mwanao.
Umesema kuna nyakati anakukatalia hata kumgusa mtoto.
Hiyo inamaana kuwa ngao yake katika hayo yote ni huyo mtoto.

Sasa basi
Kemea kwa nguvu zako zote Tabia hiyo bila ya kuogopa chochote kwa sababu kila unavozidi kukaa kimya ndivyo tabia inavozidi kukua.
Kuwa mkali naye kwa tabia yake hiyo yaani onyesha ule baba wako wewe kama baba wa familia, atakaponuna kwasababu ya kumkemea usijisumbue kumbembeleza nikimaanisha kuwa uwe na msimamo mkali juu ya kile unachotaka akiache.
Hata kama akiamua kuondoka nyumbani bado usiogope kwasababu suala litakapo fika kwa wazazi au wazee wenu, utakapoliweka wazi kama kweli ni mke mwenye nia na uchungu wa ndoa yake basi ataelewa na atarudi tena na heshima itakuwepo.
Lengo hapa si kuvunja bali kuwepo kwa heshima kwa kila upande.
Chukua hatua mapema.

Note; wewe sio malaika hivyo basi usijihesabie haki kwa 100% Bali jaribu pia kuacha na kujiepusha kufanya yale ambayo hayapendi.
Jitahidi kuepuka viashiria vinavosababisha mkeo awe na wivu kwako.
Nikukumbushe tu kuwa hata maandiko yamesema;
Enyi waume ishini na wake zenu kwa akili.

Ahsante mkuu.

Mungu nisaidie nikija kuoa haya yasinikute.
 
Vyovyote vile USIMPIGE. Ila ninaungana na wengine kusema unapaswa kusimama kama mwanaume wacha kulalalamika mkuu!!!
 
Natoa wazo ingawa wewe hujajielezea kasoro zako. Mimi hua naamini mwanamke katika ndoa atabaki kua mwanamke tu no matter what!, sasa mimi kwa nilivosoma maelezo yako uyo bi dada kashaanza kujitoa ufahamu wa kua yeye ni mwanamke inatakiwa ajiheshimu kipivi na piah amuheshimu mumewe kivipi!,
 
Umeshapewa ushauri wa kutosha, cha msingi badilisha passworld, akinuna mpotezee. ukifika nyumbani msemeshe kama kawaida asipokujibu kauka. utajirudi mwenyewe.
 
Jana kuna mkuu kaleta uzi kua ametoka kuoa ndoa ina siku tatu ni tamu sana.

Leo nakuta huu uzi.

Hapo kuna posts kibao za wanaume kuvunja amri ya sita na wake za watu na kinyume chake.

Hili lishakua tatizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom