Naombeni ushauri kuhusu tabia ya dada yangu

Naombeni ushauri kuhusu tabia ya dada yangu

Xian

Senior Member
Joined
Mar 24, 2014
Posts
127
Reaction score
42
Wapendwa samahani sana kwa usumbufu,

Nina kitu ambacho kwa kweli kinaniumiza moyo wangu sana, sisi kwetu tumezaliwa wawili na wote ni wasichana, dada yangu ni mkubwa kwangu kwa miaka saba hajaolewa na kwa kweli sijawahi kuona yuko na mwanaume ambaye wanadumu kwa muda hata kwa wiki mbili.

Akiwa na mtu yeye ni mtu wa kumfokea mwanaume na kumtukana hivyo ni dada mwenye kazi nuzri msomi kiasi ila tatizo lake ni hilo.

Shida yangu kubwa iliyonifanya niilete hapa kila nikipata mchumba akija nyumbani kujitambulisha dada yangu anadai ni mpenzi wake wa zamani na maneno hayo anawaeleza wazazi hivyo yule mwanaume hawezi kukubaliwa kuendelea na mimi.

Mara ya kwanza nilijua kweli huyo kaka hakulalamika akaondoka zake ni muda mrefu sana, nikapata mwingine dada akadai hivyo nina amini kwa kuwa tanzania kubwa.

Cha kushangaza nikapata mwanaume wa nchi nyingine nimemleta Tanzania kwa ajili ya kujitambulisha dada yangu baada ya muda akadai yule baba atembea nae kipindi hiki nilichokuja nae Tanzania.Kiukweli niliumia sana.

Yule Mjapan akatuona sisi washenzi akaondoka zake yamebaki mawasiliano ya kawaida tuu. Mungu kanikumbuka tena nimepata jamaa mwingine, baba akashauri tupange tarehe ambayo dada hayupo, na kweli kila kitu kilienda sawa.

Harusi yangu inakaribia sana na mpaka sasa dada yangu hawajawahi kuonana na mchumba wangu huyu mpya na hajapata uhakika kama kweli nina mchumba kwani hata pete ya uchumba sivai kwa kumuogopa yeye.

Naomba ushauri je! nimweleze ukweli dada kuwa nina mchumba ila tamuona siku ya harusi?

Au nimweleze mchumba tabia za dada ili hata likitokea awe anajua?

Baba zangu wadogo wanashauri asiambiwe kitu na siku ya harusi astukizwe tuu kwani hakutakuwa na sherehe kubwa ni lunch tuu na vinywaji.

Asanteni nina imani mmenielewa.

Nisaidieni
 
duh!pole sana!mi nahisi umfahamishe huyo mchumba hali halisi kwa mazingira ya nyumbani anaweza akajua anytime,nawatakieni maandalizi mema na mwisho maisha mema ya ndoa!
 
asante sana, tena ukimuona yeye ni mzuri sana wa sura na umbo kuliko mimi ila ndiyo hivyo tuu
 
duh dunia ina mambo ..............loh dada mtu kaaa kimya kama boy wako ni mwelewa just mwadisie tu tabia ya dada yako lakini kidogo san usiingie deep
 
Mbwa unayemjua sauti yake kwa nini akusumbue akibweka...

Kama mshajua tabia za huyo bi dada wala hakuna haja ya kumficha isipokuwa inabidi wazee wamkalishe chini na aelezwe na kukanywa tabia yake hiyo mbaya...

asante sana
 
duh dunia ina mambo ..............loh dada mtu kaaa kimya kama boy wako ni mwelewa just mwadisie tu tabia ya dada yako lakini kidogo san usiingie deep

kiukweli ni mwelewa sana na mara nyingi ananiuliza mbona dada sijawahi kumuona hata siku moja, namwambia tuu yuko busy sana na kazi, kwa kweli moyo umejawa ganzi naogopa
 
Kama ndoa yako ni ya kikristo nina wasiwasi ndoa ikitangazwa atakuwekea pingamizi kanisani.
 
Dadako ana tatizo la kutojiamini,anadhani yeye anastahili kuolewa kwanza kabla yako,wazazi wana nafasi kubwa kumweka sawa....pole sana.

tena ukimuona ni mzuri kweli kwa surana umbo lakini ndiyo hivyo tena, ninamsomea mama yangu post zenu anasema kwa kweli ni bora kumuweka chini
 
Kama ndoa yako ni ya kikristo nina wasiwasi ndoa ikitangazwa atakuwekea pingamizi kanisani.

ndoa ni ya kikristu itafungiwa kanisani, ila yeye si mwendaji kanisani kama mimi yeye anaenda mwaka mpya tuu
 
Nadhani msimwambie, fanyeni mambo kimya kimya kama mlivykubaliana na wazazi laki pia mwambie mume mtarajiwa tabia za dadako, ili hata siku wakionana mkaka awe anajua nakutana na mtu wa aina gani

All da best
 
....umwambie usimwambie ipo siku ataharibu tu kama hujui namna ya kudeal naye. nashauri umuelimishe mume mtarajiwa ukichaa wa dadio na jiandae kupambana naye huku ukikaa naye mbali maana hujui kesho atakuja vipi period...!!
 
duh!pole sana!mi nahisi umfahamishe huyo mchumba hali halisi kwa mazingira ya nyumbani anaweza akajua anytime,nawatakieni maandalizi mema na mwisho maisha mema ya ndoa!

asante sana kwa ushauri
 
Back
Top Bottom