Naombeni ushauri juu ya huyu mchumba

Kama hamna hisia hata kidogo usiolewe nae uyo, mtasumbuana sana, mtaish kwa shida... [HASHTAG]#UtaishiaKujuta[/HASHTAG]
 
Aisee

Komaa akupe muda wa kufahamiana japo kwa miezi 3.


Ingawa mapenzi au ndoa haina kanuni.

Unaweza fahamiana na mkajiona mnapendana lkn msifike mbali.

Enzi za mababu zetu hakukuwa na nafasi ya kupendana lkn ndoa zao zilidumu.

Sikuhizi tunatafuta hisia lkn ndoa nyingi migogoro tu.
 
Kama alifunga ndoa ya kikristo huyo bado ni mume wa mtu, isipokuwa kama mke wake alifariki.. Atakuoaje?

Muombe sana Mungu katika kutimiza hitaji la moyo wako.
 
Dada husife imani kiasi hicho;
Lea mwanao, muombe Mungu mwanaume wako anakuja. .
Utakayempenda, utakayemthamini na mtajenga maisha yenu vizuri tu kwa kidogo mtakachojaliwa

Nina ndugu zangu mmoja kaolewa juzi tu na 36 mwingine aliolewaga name 40. .

Mungu yu Mwema, akupe hitaji la moyo wako na Akutangulie ufanye chaguzi lililo sahihi
 
Dada sijui nianzie wapi..... Labda nianze kwa maswali
1. Hisia zipi unazotaka ziwepo baina yenu huku Mna mwezi mmoja tu?!
2. Jamaa ana haraka na umetoa sababu ya haraka yake kuwa ana watoto. Huoni kuwa haraka yake ni "justifiable"?
3. Kwanini unataka ndoa?
4. Kipi ni bora kwako hisia au kuwa na mtu ambaye ni committed?
5. Kwa umri wako sio muda wa kutafuta hisia, na kuweka vigezo vingi kwa mwanaume. Upo tayari kubeba majukumu ya kuwa mama wa watoto watatu?
6.Kwa sasa hao watoto wanaishi wapi?!
7. Je umeshazungumza na jamaa kuhusu mtaishi wapi baada ya ndoa?!


Mwisho, ndoa nyingi watu wanaishi ili maisha yaende. Ukitafuta hisia kwa kweli mtu anaweza kukupa hizo hisia lakini baada ya miezi kadhaa ukajuta.
 
Miaka 30 umri umeenda ila kama ungekuwa huna mtoto. Kwakuwa una mtoto huna hasra saana chakufanya tuliza akili mwambie asubiri kidogo mjenge urafiki ndipo muoane usikudupuke ndugu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom