Milale
JF-Expert Member
- Aug 29, 2013
- 494
- 189
Habari za majukumu wanaJF.
Naandika uzi huu ikiwa ni saa kumi na robo za usiku, nimewaza na kuwazua ila hili naona limenizidi uwezo na nimeshindwa kulitatua.
Jambo hili sikupenda kuliweka hapa jf ila imebidi niliweke huenda nikapata msaada zaidi na kujua cha kufanya.
Baba na mama walibahatika kupata mtoto mmoja tu wa kiume ambaye ni mimi.
Familia yetu hatukuwa na maisha mazuri tulikuwa maisha duni sana. Baba alikuwa mtu wa pombe na wanawake sana, pia ilikuwa haiwezi kupita wiki bila mama kupigwa.
Basi matatizo ya wazazi kutoelewana katika familia yetu yaliendelea yaliyopelekea kuacha shule nikiwa kidato cha pili mwaka 2008》
Baada ya hapo nilitoka nyumbani na kuja jijini kutafuta maisha.
Ghafla nae mama wakaachana na baba na nilipomuuliza mama sababu ya kuachana alinijibu kuwa asingeweza kuondoka na kuniacha pekee yangu kwa baba nikiwa bado mdogo. Ila kwa vile umri wangu umesogea sogea na nimejitambua tiyari, ana haki ya kuondoka.
Basi mama akawa mkoa mwingine, baba mkoa mwingine pia mimi mkoa mwingine.
Ila wakati niko jijini sikuwa nawasiliana kabisa na baba yangu nikikumbuka mateso yake kwa mama na kwangu pia yaliyopekea mimi kuacha shule licha ya kuwa nilikuwa nashika namba moja kila mtihani na mtihani wa darasa la saba nikishika namba mbili kimkoa enzi nikiwa shule ya msingi, kifupi niliongoza darasa kuanzia darasa la 3 mpaka 7.
Wakati nikisota jijini nikawa nawaza kabsa huenda yule si baba yangu mzazi.
Nifupishe stori
2015 baba maisha yake yalianza kubadilika na kuanza kuwa mazuri ila sikuwa nikijali kabsa japo nilikuwa napigika mtaani sikuwa na habari juu ya maisha yake maana niliona kuwa maisha yangu kuwa magumu yeye ndo chanzo.
Ghafla mwaka 2016 mawasiliano yangu na yake yalianza kurejea na kuanza kuniomba nimuombee msamaha kwa mama arudi nyumbani. Hapo tiyari alikuwa na pesa ya kutosha baada ya kujiingiza katika siasa na kupata cheo fulani akaniahidi kunijengea nyumba DSM au popote pale nitakapotaka endapo nitamshawishi mama arudi home.
Ila sikuwa namuelewa kabsa nilikuwa namsikiliza yanaishia pale nilihisi kuwa hata angenipa dunia nisingeweza, maana pia maisha yangu hapo yalikuwa yameanza kuwa na mwanga japo haikuwa sana.
Ghafla alianza kunitumia pesa mara kwa mara, na pesa yake ya kwanza ilikuwa miliono tano. Kulingana na pesa alizokuwa ananitumia nilijikuta nasahau yote na mawasiliano yakaanza kurejea taratibu na tukawa marafiki mpaka sasa.
Ila kuanzia kipindi hicho amekuwa akinibembeleza sana nimuombee msamaha kwa mama arudi nyumbani ila kati ya mambo ambayo mama hataki hata kusikia ni hilo.
Baba akipata namba ya mama siku hiyo hiyo mama lazima avunje laini.
Mama anasisitiza kuwa hata asikie anamiliki dunia kamwe hatarejea wala hahitaji chochote bora alale njaa kuliko kurudi kwa baba.
Mama nimempangia nyumba anaishi mwenyewe na binti wa kazi, ila kinachoniumiza ni hiki baba nikiongea naye mpaka machozi yanamtoka akiniomba nimuombee msamaha kwa mama ili arudi.
Pia nimeshindwa hata kumjengea nyumba mama yangu kwa kuhofia kuwa baba ataona kuwa mimi ndo chanzo cha mama kutotaka kurudi.
Kwa kifupi nimeshindwa jinsi ya kulitatua hili naombeni mawazo yenu ndugu zangu,
Ili nijue jinsi ya kulitatua maana baba kila siku tunawasiliana na ombi lake kuu ni hili la kuomba nimuombee msamaha maana yeye kashindwa.
Naandika uzi huu ikiwa ni saa kumi na robo za usiku, nimewaza na kuwazua ila hili naona limenizidi uwezo na nimeshindwa kulitatua.
Jambo hili sikupenda kuliweka hapa jf ila imebidi niliweke huenda nikapata msaada zaidi na kujua cha kufanya.
Baba na mama walibahatika kupata mtoto mmoja tu wa kiume ambaye ni mimi.
Familia yetu hatukuwa na maisha mazuri tulikuwa maisha duni sana. Baba alikuwa mtu wa pombe na wanawake sana, pia ilikuwa haiwezi kupita wiki bila mama kupigwa.
Basi matatizo ya wazazi kutoelewana katika familia yetu yaliendelea yaliyopelekea kuacha shule nikiwa kidato cha pili mwaka 2008》
Baada ya hapo nilitoka nyumbani na kuja jijini kutafuta maisha.
Ghafla nae mama wakaachana na baba na nilipomuuliza mama sababu ya kuachana alinijibu kuwa asingeweza kuondoka na kuniacha pekee yangu kwa baba nikiwa bado mdogo. Ila kwa vile umri wangu umesogea sogea na nimejitambua tiyari, ana haki ya kuondoka.
Basi mama akawa mkoa mwingine, baba mkoa mwingine pia mimi mkoa mwingine.
Ila wakati niko jijini sikuwa nawasiliana kabisa na baba yangu nikikumbuka mateso yake kwa mama na kwangu pia yaliyopekea mimi kuacha shule licha ya kuwa nilikuwa nashika namba moja kila mtihani na mtihani wa darasa la saba nikishika namba mbili kimkoa enzi nikiwa shule ya msingi, kifupi niliongoza darasa kuanzia darasa la 3 mpaka 7.
Wakati nikisota jijini nikawa nawaza kabsa huenda yule si baba yangu mzazi.
Nifupishe stori
2015 baba maisha yake yalianza kubadilika na kuanza kuwa mazuri ila sikuwa nikijali kabsa japo nilikuwa napigika mtaani sikuwa na habari juu ya maisha yake maana niliona kuwa maisha yangu kuwa magumu yeye ndo chanzo.
Ghafla mwaka 2016 mawasiliano yangu na yake yalianza kurejea na kuanza kuniomba nimuombee msamaha kwa mama arudi nyumbani. Hapo tiyari alikuwa na pesa ya kutosha baada ya kujiingiza katika siasa na kupata cheo fulani akaniahidi kunijengea nyumba DSM au popote pale nitakapotaka endapo nitamshawishi mama arudi home.
Ila sikuwa namuelewa kabsa nilikuwa namsikiliza yanaishia pale nilihisi kuwa hata angenipa dunia nisingeweza, maana pia maisha yangu hapo yalikuwa yameanza kuwa na mwanga japo haikuwa sana.
Ghafla alianza kunitumia pesa mara kwa mara, na pesa yake ya kwanza ilikuwa miliono tano. Kulingana na pesa alizokuwa ananitumia nilijikuta nasahau yote na mawasiliano yakaanza kurejea taratibu na tukawa marafiki mpaka sasa.
Ila kuanzia kipindi hicho amekuwa akinibembeleza sana nimuombee msamaha kwa mama arudi nyumbani ila kati ya mambo ambayo mama hataki hata kusikia ni hilo.
Baba akipata namba ya mama siku hiyo hiyo mama lazima avunje laini.
Mama anasisitiza kuwa hata asikie anamiliki dunia kamwe hatarejea wala hahitaji chochote bora alale njaa kuliko kurudi kwa baba.
Mama nimempangia nyumba anaishi mwenyewe na binti wa kazi, ila kinachoniumiza ni hiki baba nikiongea naye mpaka machozi yanamtoka akiniomba nimuombee msamaha kwa mama ili arudi.
Pia nimeshindwa hata kumjengea nyumba mama yangu kwa kuhofia kuwa baba ataona kuwa mimi ndo chanzo cha mama kutotaka kurudi.
Kwa kifupi nimeshindwa jinsi ya kulitatua hili naombeni mawazo yenu ndugu zangu,
Ili nijue jinsi ya kulitatua maana baba kila siku tunawasiliana na ombi lake kuu ni hili la kuomba nimuombee msamaha maana yeye kashindwa.