Naombeni njia jamani nifanyeje

Naombeni njia jamani nifanyeje

Pendaelli

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2014
Posts
12,105
Reaction score
35,140
Heri na baraka ziwe nanyi.

Ushauri, mawazo, michango yenu itanisaidia sana.

Ni binti aliyenipenda sana nakumbuka alivyoniambia kwavile alivyonipenda hakuwa tayari kuniona mimi natangulia kufa bora aanze yeye.

Kwa jinsi tulivyopendana haielezeki, ilianza hivi, baada ya migogoro kwao alitakiwa arudi kijijini akaniomba nimtafutie kazi, kuhangaika huku na huku akapata, shida ikazidi kwao kwani alikua anakaa na mama wa kambo na baba yake hana kauli.

Akaniomba tena nimtafutie pakukaa, nikahangaika tena akapata, nako shida tena ikawa kubwa, akaniomba nimpangie chumba.

Kwavile nilivyompenda nikaamua tukakae wote kwangu na mimi ndio nilianza maisha baada ya muda, taarifa zikafika kwa baba yake alipinga sana lakini akatoa masharti yaliyokua yananigharimu hela nyingi mno, nikajipa moyo nitafanikisha, binti ninae ndani matatizo yakawa yanapishana binti ni kuumwa tu, miaka ikaenda mpaka wa 3.

Sikufanikisha, mpaka binti mwenyewe akaamua kuniacha kwa kudanganywa na vijana wajanja wakati mimi nampenda.

Mwaka sasa tangu aniache, ninateseka sana.

Ushauri wenu jamani.
 
Sikilizia moyo wako binti,unajua umuhimu na udhaifu wake kuliko sisi
 
Jarbu kuchangamana sna na marafki zako ili uachane na hali ya kumkumbuka,, pia na ww tafuta wako wakukupumzisha
 
pole..., siko naandika thread mara kwa mara lakin ndugu jitahidi kuweka aya sawa
 
mi hapo kwenye matatizo tu ndo nmechoka.....yaani tangu umemjua ni matatizo tu mwanzo mwisho?
 
naomba kuendelea kuelezea shida ninayoipata baada ya kuondoka.nimekuwa nikimuwazia sana kila siku na kutaman kurudiana nae ila sijui nianzie wapi,niliwai kukutana nae mara moja tu tena kanisani sikupana nafasi ya kuongea nae na sikujamuona tena.na watu wananiambia wanakutanaga nae.picha alioiacha inaniumiza sana,nikikumbuka jinsi tulivyoanza maisha kwa shida natokwa na machozi,,nikijitahidi kumsahau siwezi na kuna nyimbo tulizokuwa tunaziangalia sana na ninazipenda sana na kuna dada mmoja muimbaji amefanana nae sana yaani nina mkumbuka sana,na maneno aliokua ananiambia jinsi alivokua ananipa moyo juu ya maisha ninaumia sana.ushauri wenu hapa nifanyeje ndugu zangu,nampenda sana.lakini chanzo ni hitilafu za ndugu zangu na baba yake. kwao hawakunipenda na hata kwetu hawakumpenda,lakini alinipa moyo na ndio tukakaa miaka hio 3 na furaha isio ya kifani na mfukoni hata mia sina.lakin ndio alishawishika akatumia kigezo cha ndugu zangu hawakumpenda ndio akaondoka. nipeni mawazo wandugu nifanyeje?
 
naomba kuendelea kuelezea shida ninayoipata baada ya kuondoka.nimekuwa nikimuwazia sana kila siku na kutaman kurudiana nae ila sijui nianzie wapi,niliwai kukutana nae mara moja tu tena kanisani sikupana nafasi ya kuongea nae na sikujamuona tena.na watu wananiambia wanakutanaga nae.picha alioiacha inaniumiza sana,nikikumbuka jinsi tulivyoanza maisha kwa shida natokwa na machozi,,nikijitahidi kumsahau siwezi na kuna nyimbo tulizokuwa tunaziangalia sana na ninazipenda sana na kuna dada mmoja muimbaji amefanana nae sana yaani nina mkumbuka sana,na maneno aliokua ananiambia jinsi alivokua ananipa moyo juu ya maisha ninaumia sana.ushauri wenu hapa nifanyeje ndugu zangu,nampenda sana.lakini chanzo ni hitilafu za ndugu zangu na baba yake. kwao hawakunipenda na hata kwetu hawakumpenda,lakini alinipa moyo na ndio tukakaa miaka hio 3 na furaha isio ya kifani na mfukoni hata mia sina.lakin ndio alishawishika akatumia kigezo cha ndugu zangu hawakumpenda ndio akaondoka. nipeni mawazo wandugu nifanyeje?

Ameshaondoka,
Wewe endelea na maisha yako...
 
achana nae, kisicho ridhiki hakiliki, ni wakati wako sasa wa kunuomba MUNGU akupe mke mwema......
 
heri na baraka ziwe
nanyi. ushauri, mawazo,michango yenu itanisaidia sana. ni bint
alienipenda sana nakumbuka alivyoniambia kwavile alivyonipenda hakuwa
tayari kuniona mi natangulia kufa bora aanze yeye.kwa jinsi
tulivyopendana haielezeki,ilianza hivi, baada ya migogoro kwao alitakiwa
arudi kijiji akaniomba nimfutia kazi,kuangaika huku na huku
akapata,shida ikazidi kwao kwani alikua anakaa na mama wa kambo na baba
yake hana kauli.akaniomba tena nimtafutie pakukaa,nikahangaika tena
akapata,nako shida tena ikawa kubwa,akaniomba nimpangie chumba.kwavile
nilivyompenda nikaamua tukakae wote kwangu na mi ndio nilianza maisha si
muda.taarifa zikafika kwa baba yake alipinga sana lakin akatoa mashart
yaliokua yananigarim ela nying mno,nikajpa moyo nitafanikisha,bint ninae
ndan matazizo yakawa yanapishana bint ni kuumwa tu,miaka ikaenda mpaka
wa 3,sikufanikisha,mpaka binti mwenyewe akaamua kuniacha kwa kudanganywa
na vijana wajanja wakati mi na mpena,mwaka ss tangu aniache,ninateseka
sana,ushauri wenu jamani.

mkuu pole. hapa shetani tumuhurumie sizan kama kahusika
 
Mkuu mwaka ni mwingi aisee... usiniambie haujaendelea na maisha yako..??!!,.... ushauri ni wewe kuendelea na maisha achana na huyo mwanamke maana mwenye kosa sio hao vijana wajanja ni huyo mwanamke ameshindwa kujua upendo hupimwa na nini...
 
Wanawake walivyojaa wewe unavyolialia duh majanga.
 
Muombe MUNGU akupe ujasiri, uvumilivu na amani moyoni. Then kaa ktk mpango wa Mungu naye atakupa cha kufanya.

Pamoja na yote jitahidi kuandika kwa kufuata kanuni za uandishi bora. Unatupa tabu kusoma!!

POLE SANA.
 
Yani mwaka mzima bado unajitesa wakati mwenzako anakula raha?
 
Tatizo ulijitwisha majukumu ambayo si yako...

Chukulia hilo kama somo na usirudie tena kwa utayempata mwingine...
 
Back
Top Bottom