Habari zenu, mwenzenu na shida tarehe 1 juz niliamka asubui nikawa naskia maumivu ya tumbo ghafla nikaanza kuharisha nakutapika baada ya kwenda hospital wakanipima nikaambiwa na typhoid na vidonda vya tumbo wakanichoma sindano ya kuzuia kutapika na nikawekewa drip 3 za maji ila cha kushangaza mpaka Leo bado naharisha na kutapita na kula pia siwezi hapa nilipo nmejikatia tamaa maana mwili unachoka sana kizunguzungu na kuishiwa nguvu, je hii ni hali ya kawaida au kuna Dawa naweza kutumia kutatua hili tatizo naombeni msaada wenu niweze kupona nateseka