NAOMBENI MSAADA WENU WANA JF.

Faru Jenny

Senior Member
Dec 29, 2016
101
71
Habarini za jumapili ndugu zangu? Natumaini mko salama na mnaendelea vizuri na maisha ya kila siku. Tafadhali naomba nichukue muda wenu kidogo kuwaeleza shida niliyonayo kama mtanzania mwenzenu mtakaowiwa muone namna ya kunisaidia.

Mimi ni mtanzania mwenzenu mzaliwa wa pili kwenye familia ya watoto sita. Kwenye familia yetu kwa sasa tuna mzazi mmoja baada ya baba kufariki mwaka 2009. Na la mwisho kwenye utambulisho mm ni mtoto pekee wa kiume katika familia yetu.

Sasa naomba niingie kwenye kilichonifanya kuna hapa kwenu wana JF kuwalilia. Mwaka 2008, dada yangu alichaguliwa kujiunga kidato cha tano katika moja ya shule za sekondari za serikali zilizopo kaskazini mwa nchi yetu. Baada ya kusoma kwa miezi kama mitatu akawa ameanza shida ya kuchanganyikiwa..( psychiatric) kama inavyotajwa kitaalam mm sina uelewa sana. Shule ilichukua jukumu kumfikisha katika hospitali ya mawenzi mkoani Kilimanjaro na baadae familia ilichukua jukumu la kumsafirisha Dar kwa kuwa kipindi hicho baba alikuwa hai na alikuwa anafanya vishughuli vyake huko Dar es salaam. Dada alitibiwa katika kitengo cha magonjwa ya akili cha hospitali ya taifa ya muhimbili kwa kipindi chote cha ule mwaka 2OO8. Alirudi shuleni kuanza kidato cha tano upya mwaka 2OO9, mwaka ambao pia mzee alifariki.

Tokea hapo tatizo limekuwa likimrudia mara na akawa anaahirisha masomo kila wakati hadi akafanikiwa kuhitimu chuo kikuu mwaka 2O15. Katika kipindi chote hicho tulikuwa tunajitahidi kama ndugu kujichangiana kumtibu. Kwa miaka kumi hiyo hadi sasa tulitumia resources nyingi kumtibu kwa kweli ukizingatia hata kwa waganga tulienda kutokana na ushawishi na shuhuda za watu . Aisee ukiwa na shida kubwa unaweza kulishwa hata mavi na binadamu.

Kinachotuumiza zaidi ni kuwa tangu alipo hitimu chuo kikuu mwaka 2O15 ameugua mfululizo hadi sasa. Tangu shida hiyo ilivyomuanza hajawahi kuugua kwa kipindi kirefu mfululizo kama hiki. Tumejitahidi kadiri ya uwezo wetu katika kila jambo lakini haki yake ndio ikazidi kuwa mbaya yani anakuwa kichaa zaidi kila kukicha. Kwa kweli imefika mahali hadi ndugu wa karibu wakajitoa kwa kuchoka kuhangaika. Nikabaki mm Na mama kama Mtoto wa kiume nikawa napambana hivyohivyo. Mm nipo mbali na nyumbani nakofanyia shughuli zangu so nikiwa napata madeni makubwa kwa akili ya kumfuatilia na kumuuguza.

Sikukata tamaa. Ilivyofika mahali usalama wake ukawa hatarini kutokana na kutoroka nyumbani usiku mara kwa mara na kwenda kusiko julikana. Baada ya kufikia hatua hiyo nikafahamishwa kuwa kuna hospitali inaitwa Lutindi ipo korogwe Tanga, pale usalama wake unaweza kuwa wa uhakika maana ni kwa ajili ya watu kama hao. Wanakaa hostel za hospital wanakula wanatibiwa kwa dawa na ushauri wa kisaikolojia.

Jamani nilijitahidi nikamchukua nikaenda nae huko na ndiko aliko sasa TATIZO NIMEZIDIWA MALIPO NDUGU ZANGU. KULE NATAKIWA KUTOA ELFU 6O, kila wiki kitu ambacho kwa kubangaiza kwangu note sijaona nikifaulu. Mambo yananiendea mrama sana nimejitahidi kulipa wiki 2. Kwa sasa nimezidiwa na hakuna tena msaada mwingine nilionao.

Ninawaomba mnisaidie chochote. Anatakiwa kukaa hospital kwa miezi mitatu . Sitaweza tena mwenyewe nipigeni tafu mlionacho kidogo nitawashukuru sana. Hata ukitaka kutuma chochote cha msaada hospitali moja kwa moja nita shukuru karibu DM nitatoa mawasiliano ndugu zangu.

Asante kwako wewe uliyechukua muda kusoma ingawa naweza kuwa sijaweza sana kujielezea naamini mtajitahidi kunielewa. Wasaalam.
 
Pole kwa yote kaka. Naomba tu kufahamu kwamba baada ya hiyo miezi mitatu ya kukaa hospitali atapona?

Je?, aliwahi kufanyiwa maombi ikashindikana?
Habarini za jumapili ndugu zangu? Natumaini mko salama na mnaendelea vizuri na maisha ya kila siku. Tafadhali naomba nichukue muda wenu kidogo kuwaeleza shida niliyonayo kama mtanzania mwenzenu mtakaowiwa muone namna ya kunisaidia.

Mimi ni mtanzania mwenzenu mzaliwa wa pili kwenye familia ya watoto sita. Kwenye familia yetu kwa sasa tuna mzazi mmoja baada ya baba kufariki mwaka 2009. Na la mwisho kwenye utambulisho mm ni mtoto pekee wa kiume katika familia yetu.

Sasa naomba niingie kwenye kilichonifanya kuna hapa kwenu wana JF kuwalilia. Mwaka 2008, dada yangu alichaguliwa kujiunga kidato cha tano katika moja ya shule za sekondari za serikali zilizopo kaskazini mwa nchi yetu. Baada ya kusoma kwa miezi kama mitatu akawa ameanza shida ya kuchanganyikiwa..( psychiatric) kama inavyotajwa kitaalam mm sina uelewa sana. Shule ilichukua jukumu kumfikisha katika hospitali ya mawenzi mkoani Kilimanjaro na baadae familia ilichukua jukumu la kumsafirisha Dar kwa kuwa kipindi hicho baba alikuwa hai na alikuwa anafanya vishughuli vyake huko Dar es salaam. Dada alitibiwa katika kitengo cha magonjwa ya akili cha hospitali ya taifa ya muhimbili kwa kipindi chote cha ule mwaka 2OO8. Alirudi shuleni kuanza kidato cha tano upya mwaka 2OO9, mwaka ambao pia mzee alifariki.

Tokea hapo tatizo limekuwa likimrudia mara na akawa anaahirisha masomo kila wakati hadi akafanikiwa kuhitimu chuo kikuu mwaka 2O15. Katika kipindi chote hicho tulikuwa tunajitahidi kama ndugu kujichangiana kumtibu. Kwa miaka kumi hiyo hadi sasa tulitumia resources nyingi kumtibu kwa kweli ukizingatia hata kwa waganga tulienda kutokana na ushawishi na shuhuda za watu . Aisee ukiwa na shida kubwa unaweza kulishwa hata mavi na binadamu.

Kinachotuumiza zaidi ni kuwa tangu alipo hitimu chuo kikuu mwaka 2O15 ameugua mfululizo hadi sasa. Tangu shida hiyo ilivyomuanza hajawahi kuugua kwa kipindi kirefu mfululizo kama hiki. Tumejitahidi kadiri ya uwezo wetu katika kila jambo lakini haki yake ndio ikazidi kuwa mbaya yani anakuwa kichaa zaidi kila kukicha. Kwa kweli imefika mahali hadi ndugu wa karibu wakajitoa kwa kuchoka kuhangaika. Nikabaki mm Na mama kama Mtoto wa kiume nikawa napambana hivyohivyo. Mm nipo mbali na nyumbani nakofanyia shughuli zangu so nikiwa napata madeni makubwa kwa akili ya kumfuatilia na kumuuguza.

Sikukata tamaa. Ilivyofika mahali usalama wake ukawa hatarini kutokana na kutoroka nyumbani usiku mara kwa mara na kwenda kusiko julikana. Baada ya kufikia hatua hiyo nikafahamishwa kuwa kuna hospitali inaitwa Lutindi ipo korogwe Tanga, pale usalama wake unaweza kuwa wa uhakika maana ni kwa ajili ya watu kama hao. Wanakaa hostel za hospital wanakula wanatibiwa kwa dawa na ushauri wa kisaikolojia.

Jamani nilijitahidi nikamchukua nikaenda nae huko na ndiko aliko sasa TATIZO NIMEZIDIWA MALIPO NDUGU ZANGU. KULE NATAKIWA KUTOA ELFU 6O, kila wiki kitu ambacho kwa kubangaiza kwangu note sijaona nikifaulu. Mambo yananiendea mrama sana nimejitahidi kulipa wiki 2. Kwa sasa nimezidiwa na hakuna tena msaada mwingine nilionao.

Ninawaomba mnisaidie chochote. Anatakiwa kukaa hospital kwa miezi mitatu . Sitaweza tena mwenyewe nipigeni tafu mlionacho kidogo nitawashukuru sana. Hata ukitaka kutuma chochote cha msaada hospitali moja kwa moja nita shukuru karibu DM nitatoa mawasiliano ndugu zangu.

Asante kwako wewe uliyechukua muda kusoma ingawa naweza kuwa sijaweza sana kujielezea naamini mtajitahidi kunielewa. Wasaalam.
 
Pole kwa maswahibu hayo ndugu, tatizo la dada yako halihitaji matibabu ya hosptali utahangaika na hosptali zote hatapona. Hata wana JF leo wakijitolea kukusaidia matibabu kwa mwaka mzima hosptalini hatapona!
Kwa kadri ya uelewa wangu wa maswala hayo tatizo la dada yako chanzo chake sio mwilini, ni rohoni. Sasa mgonjwa wa rohoni ukimpeleka hosptali za mwilini hutaambulia chochote zaidi ya kufilisiwa hata vijisenti vichache ulivyo navyo. Sehemu kubwa zaidi mlipokosea ni kesi ya nyani kumpelekea ngedere yaani kumpeleka kwa waganga wa kienyeji.


Kuna njia moja tu ya kumponya dada yako hata wewe mwenyewe kama ukitaka nayoifahamu mimi nayo haina gharama na ni nzuri sana kupitia hiyo kama mtaamua kuifuata ki kweli kweli mtafanikiwa sana kiroho na kimwili.
Nayo ni kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yenu yaani "kuokoka".
Akiamua kuokoka atafunguliwa vifungo vyote vya rohoni na atakuwa mtu huru hilo tatizo hatalipata tena. Tafuta kanisa lolote la kiroho lililopo karibu yenu mkafunguliwe.
Amua sasa maamuzi yapo juu yenu.


Ficus
 
Pole kwa maswahibu hayo ndugu, tatizo la dada yako halihitaji matibabu ya hosptali utahangaika na hosptali zote hatapona. Hata wana JF leo wakijitolea kukusaidia matibabu kwa mwaka mzima hosptalini hatapona!
Kwa kadri ya uelewa wangu wa maswala hayo tatizo la dada yako chanzo chake sio mwilini, ni rohoni. Sasa mgonjwa wa rohoni ukimpeleka hosptali za mwilini hutaambulia chochote zaidi ya kufilisiwa hata vijisenti vichache ulivyo navyo. Sehemu kubwa zaidi mlipokosea ni kesi ya nyani kumpelekea ngedere yaani kumpeleka kwa waganga wa kienyeji.


Kuna njia moja tu ya kumponya dada yako hata wewe mwenyewe kama ukitaka nayoifahamu mimi nayo haina gharama na ni nzuri sana kupitia hiyo kama mtaamua kuifuata ki kweli kweli mtafanikiwa sana kiroho na kimwili.
Nayo ni kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yenu yaani "kuokoka".
Akiamua kuokoka atafunguliwa vifungo vyote vya rohoni na atakuwa mtu huru hilo tatizo hatalipata tena. Tafuta kanisa lolote la kiroho lililopo karibu yenu mkafunguliwe.
Amua sasa maamuzi yapo juu yenu.


Ficus
Yah upo sahihi Mkuu, ni kweli Bwana yetu Yesu Kristo wa nazareti anaweza kumponya huyo dada, kikubwa ni imani kwa tu.

Lakini umeniacha na swali Mkuu, nawaza tu..."ni kivipi mtu aliyechanganyikiwa na akili, akaweza kuokoka?!!.
 
Gharama zinahusu nini mkuu, matibabu ya magonjwa ya Akili hutolewa bure
 
Pole kwa maswahibu hayo ndugu, tatizo la dada yako halihitaji matibabu ya hosptali utahangaika na hosptali zote hatapona. Hata wana JF leo wakijitolea kukusaidia matibabu kwa mwaka mzima hosptalini hatapona!
Kwa kadri ya uelewa wangu wa maswala hayo tatizo la dada yako chanzo chake sio mwilini, ni rohoni. Sasa mgonjwa wa rohoni ukimpeleka hosptali za mwilini hutaambulia chochote zaidi ya kufilisiwa hata vijisenti vichache ulivyo navyo. Sehemu kubwa zaidi mlipokosea ni kesi ya nyani kumpelekea ngedere yaani kumpeleka kwa waganga wa kienyeji.


Kuna njia moja tu ya kumponya dada yako hata wewe mwenyewe kama ukitaka nayoifahamu mimi nayo haina gharama na ni nzuri sana kupitia hiyo kama mtaamua kuifuata ki kweli kweli mtafanikiwa sana kiroho na kimwili.
Nayo ni kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yenu yaani "kuokoka".
Akiamua kuokoka atafunguliwa vifungo vyote vya rohoni na atakuwa mtu huru hilo tatizo hatalipata tena. Tafuta kanisa lolote la kiroho lililopo karibu yenu mkafunguliwe.
Amua sasa maamuzi yapo juu yenu.


Ficus
Amina baba. Tumejitahidi kwa miaka kumi sasa. Maombi nayo tumeenda sana. Labda kuna mahali tulikosea ... Hatujachoka kupokea ushauri. Lakini hospital nao wanasema tatizo lake ni ugonjwa wa akili unaotibika sasa hapo ndio tukaona tujitahidi kumtibu hospital maana kuna shuhuda nyingi waliofanikiwa kwa njia ya matibabu ya hospital. Ingawa kumwomba Mungu katika yote hayo sio jambo la kupuuzia hata kidogo.
 
Gharama zinahusu nini mkuu, matibabu ya magonjwa ya Akili hutolewa bure
Lutindi tunatoa gharama kila wiki kaka. Wale wagonjwa wanakula na kulala huko kwa miezi mitatu yote wanayohudumiwa kimatibabu. Taasisi ile pia sio ya serikali ingawaje hata matibabu ya Serikili tumekuwa tukigharamia kwa wakati wote. Kuanzia muhimbili na kwingine hatijawahi kuhudumiwa Burr.
 
Yah upo sahihi Mkuu, ni kweli Bwana yetu Yesu Kristo wa nazareti anaweza kumponya huyo dada, kikubwa ni imani kwa tu.

Lakini umeniacha na swali Mkuu, nawaza tu..."ni kivipi mtu aliyechanganyikiwa na akili, akaweza kuokoka?!!.
Ni vipi mtu aliyechanganyikiwa na akili ameweza kuhitimu chuo kikuu!? Tafadhali rejea upya uzi.
 
Pole kwa yote kaka. Naomba tu kufahamu kwamba baada ya hiyo miezi mitatu ya kukaa hospitali atapona?

Je?, aliwahi kufanyiwa maombi ikashindikana?
Ndio kipindi kinachodhaniwa kuwa sahihi kwa wao kumhudumia wakaona mabadiliko, sasa kama kweli atapona au la tunamwachia Mungu maana imekuwa hivyo kwa miaka kumi kama nilivyoeleza.
 
pole sana kwa mtiani huo ndugu,huyo dada yetu atakuwa na mapepo ,katika hii dunia mtu kuchanganyikiwa akiri kwa namna hiyo na hasa kama hakuzaliwa na tatzo hilo huwa si rahisi sana, ila endapo tu atakuwa na vitu visivyo vizuri katka mwili wake anaweza kupatwa na hali kama hiyo aliyo nayo dada yetu.Ni nguvu kubwa ya uponaji inahitajika.
 
Ni vipi mtu aliyechanganyikiwa na akili ameweza kuhitimu chuo kikuu!? Tafadhali rejea upya uzi.
Mleta uzi anadai, "...baada ya kumaliza tu chuo 2015, ndipo ukichaa ukapanda kupita maelezo...akaanza hata kutoroka nyumbani usiku......"

Nadhani wewe, ndio urudie kusoma vizuri Mkuu.
 
Ni vipi mtu aliyechanganyikiwa na akili ameweza kuhitimu chuo kikuu!? Tafadhali rejea upya uzi.
Kama utakuwa umeelewa vizuri nimeeleza kuwa miaka ya nyuma alikuwa akiahirisha miaka sana ya masomo maana alikuwa akiugua na kupona ameahirisha mara kadhaa chuo kikuu na alivyokuwa advance pia. Alimaliza vizuri degree yake ndugu. Kuanzia wakati huo ndio ameshikwa mfululizo hadi leo
 
pole sana kwa mtiani huo ndugu,huyo dada yetu atakuwa na mapepo ,katika hii dunia mtu kuchanganyikiwa akiri kwa namna hiyo na hasa kama hakuzaliwa na tatzo hilo huwa si rahisi sana, ila endapo tu atakuwa na vitu visivyo vizuri katka mwili wake anaweza kupatwa na hali kama hiyo aliyo nayo dada yetu.Ni nguvu kubwa ya uponaji inahitajika.
Asante kwa ushauri
 
Amina baba. Tumejitahidi kwa miaka kumi sasa. Maombi nayo tumeenda sana. Labda kuna mahali tulikosea ... Hatujachoka kupokea ushauri. Lakini hospital nao wanasema tatizo lake ni ugonjwa wa akili unaotibika sasa hapo ndio tukaona tujitahidi kumtibu hospital maana kuna shuhuda nyingi waliofanikiwa kwa njia ya matibabu ya hospital. Ingawa kumwomba Mungu katika yote hayo sio jambo la kupuuzia hata kidogo.
Rudini tena kwenye maombi na mfuate procedures nilizowaandikia hapo juu. Watu wengi huenda kwenye maombi baada ya kupatwa na matatizo, punde wakishaponywa hurudia "life style" ile ile. Na tatizo hurudi na kuwa kubwa zaidi. Hii ni sawa na mgonjwa wa malaria anapokwenda hosptali akatibiwa na kupona akasahau kusafisha/kufyeka vichaka na mazingira yanayomkaribisha mbu akasahau pia kulala bila kuweka chandarua. Mtu wa namna hii unafikiri ugonjwa hautamrudi?!
 
Kama utakuwa umeelewa vizuri nimeeleza kuwa miaka ya nyuma alikuwa akiahirisha miaka sana ya masomo maana alikuwa akiugua na kupona ameahirisha mara kadhaa chuo kikuu na alivyokuwa advance pia. Alimaliza vizuri degree yake ndugu. Kuanzia wakati huo ndio ameshikwa mfululizo hadi leo
Kama utakuwa umeelewa vizuri nimeeleza kuwa miaka ya nyuma alikuwa akiahirisha miaka sana ya masomo maana alikuwa akiugua na kupona ameahirisha mara kadhaa chuo kikuu na alivyokuwa advance pia. Alimaliza vizuri degree yake ndugu. Kuanzia wakati huo ndio ameshikwa mfululizo hadi leo
Haijalishi wewe unaweza kusimama badala yake na akaponywa na kuokoka.
Prisoner of hope
 
Back
Top Bottom