Naombeni msaada haraka, Escrow inaniumiza moyo wangu

Naombeni msaada haraka, Escrow inaniumiza moyo wangu

Mbuzimtu

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2013
Posts
355
Reaction score
178
Ndugu zangu, naumia sana na swala la Escrow kwa kuwa limenipa maswali mengi ya msingi ambayo nashindwa kulala na sijui nifanyeje?. Naomba mwenye majibu ya maswali hapo chini anisaidie haraka sana.
1. Kama pesa za Escrow si mali ya umma, kwa nini watumishi wa umma wawajibishwe kwa kupewa pesa na rafiki yao?.
2. Ni kweli kuwa orodha ya watu waliopoke pesa za Escrow kupitia Stanibic benki hawa julikani?.

3. Ni kweli kwamba benki ya stanibic imegoma kutoa majina ya wanufaika wa Escrow?.
4. Kitendo cha bunge na vyombo vyake kushindwa kuweka full scandal, yaani wanufaika kupitia Mkombozi benk + Stanibic benk, bunge halioni kuwa limefanya kazi ya hovyo na inayotia mashaka mengi juu ya utendaji wake wa kazi?
5. Kuna chombo chochote cha kibishara kilicho juu ya Serikali ya nchi?, kama hakipo, Stanibic wamepata wapi nguvu na misuli ya kugoma kutoa list ya wanyonyaji wa taifa hili?.
6. Je, wananchi tunasababu ya kuendelea kuwaamini wabunge wanaoshindwa kuisimamia na kuishauli serikali kwa ukamilifu?.
7. Kwa nini tuache maswali mengi kuhusu wanaufaika wa Escrow kupitia stanic?.


NITAFURAHI SIKU NIKIONA FULL LIST YA WANUFAIKA WA ESCROW KUPITIA STANIBIC BENK

inafanyaje biashara yake nchini kiasi kwamba hata Serikali na vyombo vyake vinaamliwa na benk hiyohaiwezi kui
 
Hivi kama stanbic bank imegoma kutoa list hivi bunge au chombe chochote cha serikali haiwezi kuichukulia hatua bank hiyo?
Au Hanna sheria inayoruhusu
 
Mimi ninaamini kuwa, hakuna chombo chochote kinachoweza kufanya mambo kinyume na taratibu za nchi alafu kikabaki salama.
 
Hebu tafuta pesa bhana!
Escrow mwachie Slaa na Lipumba walifuatlie!
Utakufa bure ukiwa poor, mambo mengine yaache kama yalivyo!
 
Usijitoe Ufahamu.Waliochukua mgao kupitia Stanbic wanafahamika.kama watu wasiokuwa na influence kubwa kenye hayaa malipo wamepata 400M,800 sijui 1.6B,Unadhani watu wenye influence kubwa wenye malipo haya kama Waziri husika,CAG, Governor wa BOT na Mkulu na Ofisi yake iliyoruhusu malipo watakuwa wamevuna kiasi gani?Kwahiyo hawa watu wanajulikana ila kwa vile ni wakubwa hakuna hata mtu anayejishughulisha kuliongelea wala kuweka nia ya kutaka kuwajua.
 
Usijitoe Ufahamu.Waliochukua mgao kupitia Stanbic wanafahamika.kama watu wasiokuwa na influence kubwa kenye hayaa malipo wamepata 400M,800 sijui 1.6B,Unadhani watu wenye influence kubwa wenye malipo haya kama Waziri husika,CAG, Governor wa BOT na Mkulu na Ofisi yake iliyoruhusu malipo watakuwa wamevuna kiasi gani?Kwahiyo hawa watu wanajulikana ila kwa vile ni wakubwa hakuna hata mtu anayejishughulisha kuliongelea wala kuweka nia ya kutaka kuwajua.

Mkulu wa Kaya aka Sindbad Mpya ndiye kinara cha escrow lakini Wabunge wasio na korodani na matiti halisi wameogopa kumuangamiza wakaamua kuwaonea waliopewa fedha na VIP ambayo ilipata malipo yake halali.
 
tushaliwa, tuwe wapole

Lazima tupiganie ukweli kujulikana ili mwisho wa siku wote narudia wote akiwemo Raisi Kikwete aliyeidhinisha kutolewa kwa fedha hizo wakumbane na mkono mkali wa sheria licha ya kinga yake ya uraisi.
 
Ndugu zangu, naumia sana na swala la Escrow kwa kuwa limenipa maswali mengi ya msingi ambayo nashindwa kulala na sijui nifanyeje?. Naomba mwenye majibu ya maswali hapo chini anisaidie haraka sana.

Ndugu yangu nakupongeza kwa kuanzisha mjadala huu ambao inaelekea wazalendo wengi hawakuupa umuhimu japo ni sawa kabisa na yanayojulikana na yaliyoleta mtikisiko mkubwa kwa siasa za nchi hii. Hapa nimejaribu kutoa maoni yangu kuhusu hoja hii muhimu. Ubarikiwe sana.
[TABLE="class: MsoTableGrid"]
[TR]
[TD][/TD]
[TD="width: 383"] Hoja[/TD]
[TD="width: 362"] Maoni yangu[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 54"] 1.[/TD]
[TD="width: 383"] Kama pesa za Escrow si mali ya umma, kwa nini watumishi wa umma wawajibishwe kwa kupewa pesa na rafiki yao?.

[/TD]
[TD="width: 362"] Kwa kuwa wamefikishwa mahakamani, tuwe wavumilivu tusubiri hukumu. La msingi itakuwa waliowashitaki watatoa msingi ya mashitaka yao. Na wameeleza vifungu walivyovitumia kuwafungulia mashitaka. Ni juu ya washitakiwa kuelezea uhusiano walionao na aliyewapa.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 54"] 2.[/TD]
[TD="width: 383"] Ni kweli kuwa orodha ya watu waliopoke pesa za Escrow kupitia Stanibic benki hawa julikani?.

[/TD]
[TD="width: 362"] Stanibic inawajua, yawezekana haijabanwa vya kutosha kutoa takwimu hiyo. Inawezekana vyombo husika hawataki kuwajua na kuwatangaza hadharani. Lakini vile vile yawezekna kunavifungu vya sheria vinavyowapa kinga ya kutotangaza majina.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 54"] 3.[/TD]
[TD="width: 383"] Ni kweli kwamba benki ya stanibic imegoma kutoa majina ya wanufaika wa Escrow?.

[/TD]
[TD="width: 362"]
Mimi sina uhakika kama wamegoma( Stanibic) kwa maana PAC haikutwambia kilichojili. Sijui kwa nini hawaja ( PAC) haijatumia madaraka waliotumia kuwaweka ndani kama walivyowaweka ndani vigogo wa shirika la umma waliogoma kuleta mikataba kwao? Kwa kuwa baadhi( PAC) na hasa Mheshimiwa Zitto na Mhe. Filikunjombe wapo watusaidie tujue wamekwama wapi.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 54"] 4.[/TD]
[TD="width: 383"] Kitendo cha bunge na vyombo vyake kushindwa kuweka full scandal, yaani wanufaika kupitia Mkombozi benk + Stanibic benk, bunge halioni kuwa limefanya kazi ya hovyo na inayotia mashaka mengi juu ya utendaji wake wa kazi?

[/TD]
[TD="width: 362"]
"Heri moja shika kuliko kenda nenda uje". Tumepata mahali pa kuanzia na tutatakiwa kuibana( PAC) ikamilishe kazi. Sehemu ndogo waliyoifanya imetungua macho. Tuna mahali pa kuanzia, tuna kielelezo( Reference/presidence)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 54"] 5.[/TD]
[TD="width: 383"] Je, wananchi tunasababu ya kuendelea kuwaamini wabunge wanaoshindwa kuisimamia na kuishauli serikali kwa ukamilifu?.

[/TD]
[TD="width: 362"] Kwa kuwa umma unajua kilichotakiwa kufanyika na wao wameshindwa kwa kiwango fulani, tuendelee kuwashinikiza wakamilishe kazi yao. Kwa bahati mbaya kwa mfumo wa bunge letu, hatuna uwezo wa kuwashitaki kwa kushindwa kutimiza wajibu wao. Maana wana kinga ya kutoshitakiwa kwa maamuzi wanayoyafanya kama bunge, kamati au mbumge mmoja mmoja .
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 54"] 6.[/TD]
[TD="width: 383"] Kwa nini tuache maswali mengi kuhusu wanaufaika wa Escrow kupitia stanic?.
[/TD]
[TD="width: 362"]
Hakika hapo ndipo tunapotakiwa kukomaa. Nawaomba akina Kubenea, Jenerali Ulimwengu, Albanus, Dr. Kijo Bisimba na wote wenye uwezo wa kujenga hoja za kisheria wasaidie nchi hii kadri inavyowezekana tuweze kujua ni akina nani hao na wachukuliwe hatua kama wanufaika wa VIP engineering na mkombozi Benki. Lazima haki itendeke na ionekane kutendeka.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 54"][/TD]
[TD="width: 383"][/TD]
[TD="width: 362"][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Ubarikiwe sana, maoni yako ni mazuri tatizo ni kwamba hakuna wa kuratibu kuanza utekelezaji hata walau kuchukua maoni kama haya; wadau toeni mawazo ikitokea tatizo tufanye nini maana wengi tunaishia kutoa maoni humu jamvini na wala hayafiki kokote. la msingi kuliko yote ni kwamba tunaendelea kufunguka upeo wetu kuhusu ''siri kali'' yetu na mambo yanayofanyika.
 
Back
Top Bottom