Mbona nilishaleta mada ndefu sana ikahadiliwa na jamaa wengi kama wewe ambao wanajikuta wanachoka hata hawajamfikia wanemtongoza walinipa asante ,maana walifanikiwa ,angali labda nikumegee tu kidogo,tabia za wanawake huwaga hawaendi mbali sana katika mihangaiko yao na hiyo itakusaidia wewe kwa yule uliemdondokea kwanza kusoma tabia yake,hapa sizungumzii wale ambao utakuna nao kwenye vilabu vya mbege ,apana nazungumzia wale ambao pengine amekupitia na ukahitaji kuwa nae ,muhimuni kuanza mazoea na hapa panataka au panahitaji ueledi mzuri sana ,pia jaribu utakavyoweza ili upate kuangaliana nae uso kwa uso na ufanikishe eye contact ,macho yakiangaliana huwa yanazungumza ,utaweza kutafsiri kivyako ,urahisi ni kujifanya umepotea njia ,na kama ulishamfatilia safari zake kama nilivyo andika hapo mwanzo ,utamuambia unatafuta njia au duka fulani ,ukweli ni kule aendako na kama anaweza kukufikisha ,bila ya shaka atakusaidia kukufikisha.
Katika muongozano jaribu kusifia kitu ,au kushangaa kitu ,yani hata ukiona paka ,au kuku au nyumba basi unaweza kuanza hapohapo ,kwa mfano nilikuwa na paka wangu kama yule akagongwa na gari akafa ,nililia kwani nikimpenda sana sana,..utasikiliza kama atakujibu au atabakia kimya ,kama ni kimya ,muulize wewe unapenda paka ,,yote hayo ni kutafuta maingiliano na wanawake wanapenda story sana ,usirefushe sana mazungumzo yako,na ikiwa na yeye atakuuliza jaribu kufupisha jawabu.