Naombeni mnielekeze nahisi wanataka kunitapeli

Naombeni mnielekeze nahisi wanataka kunitapeli

vnn

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2015
Posts
3,030
Reaction score
7,497
Nimeona tangazo kwenye group flani la watsapp la fani tuliyosomea.

kuna jamaa alikua anatangaza kua anaunga bando la GB 6 kwa week halotel na unamlipa baada ya kuungwa.

sasa bwana nikamtumia namba yangu akaniambia kuna code zitakuja kwenye simu yako uzitume chap kwangu nikuunge.

Code zenyewe zilizokuja ndo zikanifanya nishtuke au jamaa anataka kunitapeli.

IMG_20211103_115144.jpg



wataalam wa mambo naomba mnijuze hii namba yangu ya OTP niliyotumiwa je, anaweza akaitumia ku hack lsimcard yangu?

au anaweza hata kuingia halopesa yangu?

nijuzeni kabla sijqmtumia bas wadau
 
Umeliwa jamaa. Maana yake anatumia simu yako kama yeye ndo anamiliki.

OTP =one time password.

Maana yake amefanya changes huko sasa hiyo ndo password ya mwisho kuthibitisha kama niwewe ndo unafanya changes
 
Huo ujumbe umeingia kutoka kwenye jina gani au namba ipi?
 
😂😅 njoo tubeti tu achana na mambo hayo ya GB kuungwa nenda dukani nunua vocha yako safiii tu hiyo, ame install halopesa kwenye simu yake, so ungetuma code hiyo tu ungeisha,
 
Nimekunywa chai ya maziwa ila angekuwa mtu mwingine ashatangaza.
 
Hikiwalichofanya Makampuni ya simu kupunguza bundle, kitawafanya matapeli kutumia huu upenyo kutapeli watu
 
Umeliwa jamaa. Maana yake anatumia simu yako kama yeye ndo anamiliki.

OTP =one time password.

Maana yake amefanya changes huko sasa hiyo ndo password ya mwisho kuthibitisha kama niwewe ndo unafanya changes
duh bora nimeshtuka mapema sijamtumia
 
😂😅 njoo tubeti tu achana na mambo hayo ya GB kuungwa nenda dukani nunua vocha yako safiii tu hiyo, ame install halopesa kwenye simu yake, so ungetuma code hiyo tu ungeisha,
duh kumbe jamaa ms*nge
 
Huyo anayetaka kukutapeli anatumia Halopesa App na atapita na pesa yako yote.

!

!

Inaonekana umeshamtumia mpaka password za akaunti yako.?
 
Huyo anayetaka kukutapeli anatumia Halopesa App na atapita na pesa yako yote.

!

!

Inaonekana umeshamtumia mpaka password za akaunti yako.?
siijamtumia chochote zaidi ya namba ya simu tu
 
siijamtumia chochote zaidi ya namba ya simu tu
Kunawengine wanasema wanaunga vifurushi vya mwezi au miez kadhaa mpka mwaka, nliwauliza Nan ana access ya kuniunga?? Hyo mtu akanijuib mtu wa mtandao husika, Bei zao si haba, ila nilista tu kukubali nikajua naweza kupigwa,

Nlimwambia aniunge kabla ya kulipia akagoma nikaacha,
 
Back
Top Bottom