Naombeni jibu tafadhali..inauma sana!!

Naombeni jibu tafadhali..inauma sana!!

Joined
Apr 29, 2013
Posts
49
Reaction score
14
Hivi inawezekanaje mtu uzae mtoto umlee mpaka miezi minne halafu umtupe kweli? hata ile huruma tu kwamba mtoto huyu amenizoea, nitamkumbuka, cjui nani atamuokota, kweli mtu unakuwa hauna? nimeamini kweli tumeumbwa tofauti...mtoto huyu mzuri unayemuona ametupwa maeneo ya bamaga mwenge, kwa nini tuzae ikiwa kulea ni shida? mbona njia za uzazi jamani zimejaa...omg..!!! picha ya mtot.jpg picha ya mtot.jpg mtoto.JPG mtoto.JPG
 
Kweli tumeumbwa tofauti wengine wanatafuta wtt kwa udi na uvumba wengine ndo hao wanawatupa. Yaraab stara. Tustiri umma wako.
 
Huyo aliembeba ni prospective first lady mrs joyce kileo?
 
Hivi inawezekanaje mtu uzae mtoto umlee mpaka miezi minne halafu umtupe kweli? hata ile huruma tu kwamba mtoto huyu amenizoea, nitamkumbuka, cjui nani atamuokota, kweli mtu unakuwa hauna? nimeamini kweli tumeumbwa tofauti...mtoto huyu mzuri unayemuona ametupwa maeneo ya bamaga mwenge, kwa nini tuzae ikiwa kulea ni shida? mbona njia za uzazi jamani zimejaa...omg..!!!View attachment 100707View attachment 100707View attachment 100708View attachment 100708

Hii inakupa picha halisi kwanini wachawi wengi ni wanawake! Wana roho ngumu kweli kweli!
 
Mi nina wasiwasi kama kweli mama yake amemtupa. Inawezekana huyo mtoto aliibwa kwao mwizi mambo yakamshinda akamtupa. It is possible pia huyo mtu alitaka kumkomoa mama yake. Nashindwa kuwa mwepesi kuhukumu.
 
Wanawake wakatili sana jamani.
 
Du kweli kila mtu ana experience yake na leba, labda huyo alifika hospital na ndani ya dakika moja akafyatua copy.Lakini angekuwa ni yule aliehangaika na uchungu na kuwekewa dripi za uchungu kama chupa sita wala asingefanya hivo,angekomaa nae mpaka mwisho
 
huyo dada aliyetupa mtoto MUNGU amrahani asipate mtoto tena ktk maisha yake yote yaliyobakia hapa duniani na hata mbinguni kama lipo.
 
Kweli tumeumbwa tofauti wengine wanatafuta wtt kwa udi na uvumba wengine ndo hao wanawatupa. Yaraab stara. Tustiri umma wako.
Laah inasikitisha sana kama huyo aliefanya kitendo cha kumtupa huyu mtoto alikua na dhamira gani!!! Maana hata myama ana akili za kuangalia mwanae na kumficha mahala ambapo anajua hapa ni mahala pana usalama wa mtoto wake na hata mtoto wake akilia tu anajua mwanagu ananjaa analala na kumpa mwanawe ziwa anyonyee mpaka akishashiba anajua ametosheka, swali la kujiuliza huyu aliemtupa huyu mtoto inamaana anazidiwa akili na myama? au alikua anataka kuua hiki kiumbe? Pumbavuuuu kabisa huyu inatakiwa tufuate usemi wa Mhishimiwa ni kupiga tuu mtu wa aina hii
 
Hivi inawezekanaje mtu uzae mtoto umlee mpaka miezi minne halafu umtupe kweli? hata ile huruma tu kwamba mtoto huyu amenizoea, nitamkumbuka, cjui nani atamuokota, kweli mtu unakuwa hauna? nimeamini kweli tumeumbwa tofauti...mtoto huyu mzuri unayemuona ametupwa maeneo ya bamaga mwenge, kwa nini tuzae ikiwa kulea ni shida? mbona njia za uzazi jamani zimejaa...omg..!!!View attachment 100707View attachment 100707View attachment 100708View attachment 100708

Juu ya kitendo alichofanya nampa pongezi kwa kuhakikisha kuwa amelifanya wakati muafaka kwani mtoto ana afya yake. Bila shaka aqlikuwa na sababu ambayo yy amehisi itajibika kwa kutowa nafasi kwa wengine kumpokea.
 
Wanawake wakatili sana jamani.
Na baba wa mtoto asiyetaka kujua mtoto wake naye aitwaje? Mkuu ni muhimu kujiuliza mambo mengi hapo kwanini asingetoa mimba, kwanini amefanya hivyo baada ya kukaaa naye kwa muda fulani na asimtupe tu baada ya kumzaa, je baba wa mtoto yuko wapi? na amechukua hatua gani za kutaka kujua habari za mwanae ukizingatia bado ni mdogo kiasi hicho
 
Juu ya kitendo alichofanya nampa pongezi kwa kuhakikisha kuwa amelifanya wakati muafaka kwani mtoto ana afya yake. Bila shaka aqlikuwa na sababu ambayo yy amehisi itajibika kwa kutowa nafasi kwa wengine kumpokea.

eh unampa pongezi kwa kutupa mtoto?hata kama awe na matatizo kiasi gani suluhisho c kutupa mtoto alikuana uhakika gani kama mtoto huyo ataokotwa na mtu ..je angeliwa na wanyama? ni bora angeweka wazi shida zake wasamaria wamsaidie...
 
Back
Top Bottom