naomba ushauri wenu

Kama hufanyi makosa unawasi wasi gani.

Huyo anaye kuitwa player ungeomba kamchezo naye basi :violin:

fazaaa hapa tu ndio nimekubaliana na wewe"kama hufanyi makosa unawasiwasi gani?" kijana hebu tueleze kwa ufasaha..nyoosha maneno..
 
Usinilaumu kufikiria hayo hasa kwa tunavyosikia jinsi maisha ya huko yalivyo. Tunasikia huko hakuna wakati wa kupoteza kwa ajili ya kazi. Sasa unapotwambia kuwa wake watatu wa watu tayari wanakufuatilia bila shaka ipo nafasi ya kujitanua. Halafu haya mawakati unayokutana kutana na wenzako kiasi cha wanamama kukushobokea yanapatikana wapi, iwapo hakuna mataimu ya kutanua huko?

umeshawahi kusikia msemo tembea uone mambo? basi ndio hayo sio kila unalosikia ni kweli, watu wanapenda kutia chumvi wanapohadithia maisha na mapirika ya walipo, hawasemi yote na huwezi kuyajua yote hadi pale ukienda mwenyewe na kuona kwa macho yako. Mfano ni huo ulosema kuwa hakuna wakati wa kupoteza kwa ajili ya kazi, sio kweli, mimi binafsi kwa mfano, nafanya kazi jumatatu hadi ijumaa saa tatu hadi kumi na moja na nusu, week end niko off, natumia siku hizo kupumzika, kufanya mambo yangu ya binafsi nyumbani, kwenda kuona mechi za mpira, kutembelea rafiki na jamaa pamoja na kuwasiliana na walio nyumbani. Mara chache huenda ofisini kama kuna jambo muhimu au kama niko nyuma katika moja ya kazi zangu. Sasa tu kwa kuwa wako watu wengine kwa sababu zao wenyewe hutafuta kazi za week end kuongezea na kazi ile ya jumatatu hadi ijumaa, hapo ndio tena wanapowaambia kuwa maisha ya nje hakuna kupumzika au kupoteza muda, lakini ukweli ni kuwa huo ni uamuzi wao na sio hali halisi ilivyo kwa kila mtu. Nadhani umenielewa kidogo.
 
Wadada wengi makini hawapendi wanaume wa design yako; mimi mmoja wapo. Simshangai huyo dada aliyekuona player. Maana ni dream za wadada makini kuwa na private husband na si cha wote.

Mimi mume wangu kila mtu wa jinsia ya kike ambaye si ndugu yangu ananilalamikia kuwa anaringa (marafiki na ofisi mates wangu) kisa uwa anawachunia kama hawajuhi wakikutana mitaani. Unajua nawajibu vipi? Jamani mume wangu wala hana maringo. Kimoyo moyo nasema ongeza maringo mume wangu; na wala simwambii eti achangamkie rafiki zangu; wa kazi gani?

Nani anataka mwanaume anayemkenulia kila mtu???? Hata mimi ukinikenulia kenulia kila tunapokutana na kunichangamkia kupitiliza najua unanitaka.

Moja ya mawaidha ninayoyakumbuka kutoka kwa mwalimu mkuu wa skuli tulipokuwa tunaanza primary "tabasamu upate marafiki, utakuwepo hapa shuleni hapa kwa miaka mingi unahitaji kuwa na marafiki, sio kila anaekuchekea anakutaka kimapenzi."
 
Katika mwaka mmoja tu (june 2011 hadi July 2012) wake za watu watatu wamenifata kunitaka kimapenzi. Ninachotaka kujua ni kwa nini? ni kosa gani nifanyalo kiasi kuwa wake za watu wafikiri nawataka?
Wote nimewakwepa, lakini kinachonishangaza ni kwa nini hasa waache waume zao na kunifuata mimi? Wakati huo huo kuna mwanamke ambae yuko single na ananivutia mno lakini ananipiga chenga mwaka na nusu sasa na anasingizia eti ananihisi mimi ni player, jambo ambalo sio kweli kabisa!
Mmoja kati ya hawa wake za watu amefika hadi kudai kuwa anajua hasa kuwa ninamzimia, na ni woga tu ndio unaonizuia mimi kumfuata, na kwa sababu hiyo ndiyo yeye kaamua ku make the first move. Wote wamedai kuwa ucheshi wangu na tabasamu zangu niwaonapo njiani na sehemu za mikusanyiko ni ishara ya kuwa niko interested. Hilo sio kweli kwani hiyo ni hulka yangu kuwa mcheshi kwa kila nimjuae sio kwao wao tu, tabasamu kwangu ni jambo la kawaida. Daima huwa na dakika chache za kusimama kusalimiana na kuzungumza na niwajuao nikutanapo pahali popote pale.
Hivi ndugu zangu kuwa mcheshi na mchangamfu ni kosa? Huku ugenini ukianza kutokusalimia au kutotaka kujuana na watanzania wenzako ni hatari, kwani mbali ya wao kukuona kuwa unajipenda na kuwadharau wenzako pia nao watakutenga, jambo amablo sio jema hasa ukizingatia kuwa tuko mbali na familia zetu, binaadam mzima leo hujui kesho utaamkaje.
Hebu niambieni nifanyaje ili kuepukana na matatizo haya. Imeanza wake wa watu kuhisi nawataka, isije ikaja kufika waume zao kufikiria nawaibia wake zao.


Nashukuru kuwa unajua kama ni wake za watu. Ushauri wangu ni kwamba, Ogopa mke wa mtu, usimchezee hata siku moja. Take it from me, mke wa mtu ni hatari mno.
 
umeshawahi kusikia msemo tembea uone mambo? basi ndio hayo sio kila unalosikia ni kweli, watu wanapenda kutia chumvi wanapohadithia maisha na mapirika ya walipo, hawasemi yote na huwezi kuyajua yote hadi pale ukienda mwenyewe na kuona kwa macho yako. Mfano ni huo ulosema kuwa hakuna wakati wa kupoteza kwa ajili ya kazi, sio kweli, mimi binafsi kwa mfano, nafanya kazi jumatatu hadi ijumaa saa tatu hadi kumi na moja na nusu, week end niko off, natumia siku hizo kupumzika, kufanya mambo yangu ya binafsi nyumbani, kwenda kuona mechi za mpira, kutembelea rafiki na jamaa pamoja na kuwasiliana na walio nyumbani. Mara chache huenda ofisini kama kuna jambo muhimu au kama niko nyuma katika moja ya kazi zangu. Sasa tu kwa kuwa wako watu wengine kwa sababu zao wenyewe hutafuta kazi za week end kuongezea na kazi ile ya jumatatu hadi ijumaa, hapo ndio tena wanapowaambia kuwa maisha ya nje hakuna kupumzika au kupoteza muda, lakini ukweli ni kuwa huo ni uamuzi wao na sio hali halisi ilivyo kwa kila mtu. Nadhani umenielewa kidogo.


Nimekuelewa sana na tukirudi kwenye mada yetu, mambo mawili yanajionyesha hapo. Una wakati wakutembelea jamaa wa kutosha na alhamdullilah una kazi soundly vitu hivi wakati mwengine vinachangia matatizo. Na ndio maana nikasema hapo awali kuwa makini na hizi ulizosema safari za kutembelea jamaa. Hebu jidai kuwa nawe uko bize kidogo ili kupunguza hayo mawasiliano. Wanawake watakutega hao ufikiri kuwa labda wanafatia tabasamu zako kumbe wana hesabu za baadae.
 
Nimekuelewa sana na tukirudi kwenye mada yetu, mambo mawili yanajionyesha hapo. Una wakati wakutembelea jamaa wa kutosha na alhamdullilah una kazi soundly vitu hivi wakati mwengine vinachangia matatizo. Na ndio maana nikasema hapo awali kuwa makini na hizi ulizosema safari za kutembelea jamaa. Hebu jidai kuwa nawe uko bize kidogo ili kupunguza hayo mawasiliano. Wanawake watakutega hao ufikiri kuwa labda wanafatia tabasamu zako kumbe wana hesabu za baadae.

Ahsante, nimekuelewa na nitajaribu kufata ushauri wako
 
Mh,mke wa mtu sumu...nafikiri hii ni hatar zaid ya ile inayoingia kwenye born marrow.
 
Mh,mke wa mtu sumu...nafikiri hii ni hatar zaid ya ile inayoingia kwenye born marrow.
 
Wadada wengi makini hawapendi wanaume wa design yako; mimi mmoja wapo. Simshangai huyo dada aliyekuona player. Maana ni dream za wadada makini kuwa na private husband na si cha wote.

Mimi mume wangu kila mtu wa jinsia ya kike ambaye si ndugu yangu ananilalamikia kuwa anaringa (marafiki na ofisi mates wangu) kisa uwa anawachunia kama hawajuhi wakikutana mitaani. Unajua nawajibu vipi? Jamani mume wangu wala hana maringo. Kimoyo moyo nasema ongeza maringo mume wangu; na wala simwambii eti achangamkie rafiki zangu; wa kazi gani?

Nani anataka mwanaume anayemkenulia kila mtu???? Hata mimi ukinikenulia kenulia kila tunapokutana na kunichangamkia kupitiliza najua unanitaka.

Sitaki kukutia homa ila nakukumbusha tu simba mwenda kimya ndie mlae nyama. Huyo mumue kuwa anawakalia kimya hao marafiki zako sio kuwa hana nyumba ndogo. infact uliza uambiwe, watu wangapi wamesalitiwa na marafiki zao na wakati wote wakiwa wanaamini kuwa waume zao na marafiki zao hawapatani kabisa?

Wataalamu wa nyumba ndogo ni wajanja na janja moja ni kujifanya anaemngegua hampendi anapokuwa mbele ya wanaowajua. Si unafanya kazi wewe? hujawahi kusikia watu maofisini inapotoka siri yao ya kuwa wana affair na kila mtu kushangaa?

Ukimya na kutoongea na marafiki zako sio dalili ya kuwa hana nyumba ndogo, sio dalili kuwa hamnegui mmoja wa marafiki zako na sio dalili kuwa hammezei mate hata rafiki yako mmoja.

Tabasamu kwa upande wake sio dalili ya kumtaka mtu kabisaaaaa!!!!
 
It's important to understand; personality makes you the way you're.
Ucheshi, uchangamfu, upole zote hizo ni attributes tu, as long as ni tabia poa huna haja ya kujishuku.
Elewa tu kuwa hizo tabia umeumbiwa, kwa kuwa out there, there's some girl who is a perfect fit kuja kumerge na tabia zako.
so patient be you buddy!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom