Naomba ushauri wako rafiki....

Naomba ushauri wako rafiki....

hapo kuna mawili kweli au si kweli
fanya uchunguzi coz hujui wangapi wanafurahia
kuona ndoa yenu anadumu!muombe mungu akupe ujasiri pia!
 
Ushauri wenu ni mzuri;
Baadhi ya majibu ya maswali hayo ni kama ifuatavyo:-
Binti nilimuomba namba ya mumewe akasema hana simu.
Nikamuomba namba ya kwake akadai hajaikalili kichwani; akaniomba niongozane naye hadi saloon ili anipe hiyo namba ya kwake - nikamkatalia.
Wife nilimuita hotelini - nikakaa naye - baada ya bia 2/3 hivi nikamuuliza - akadai hajui chochote kuhusiana na hilo.
Kuhusu utulivu wa wife wangu namwamini sana na ni mtu ambaye yuko bize na shughuli zake, ni mcha Mungu, hana makuu; n.k
Ila kulikuwa na tetesi mtaani kwamba kuna kundi la wanawake wanataka kuvuruga ndoa yangu. Kwa kukumbuka tetesi hizo ndo maana nilipoelezwa maneno hayo sikupanick wala kuwa na mawazo.
 
Habari za saa hii. Kila hadithi au kisa kinapande mbili za maelezo huyo dada kasema yake lakini mkeo ujafahamu yake pia.
Kikubwa kama alivyokuambia huyo dada wewe usizidishe wala kupunguza muite wife kwa upole ambao hajawahi ona kwako kisha msimulie najua yeye atakuwa anamengi ya kusema kama uwongo au ukweli hilo anajua yeye ila tu wewe uwe jasiri usipayuke kisha umwachie yeye atatoa jibu

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Naufanyia kazi ushauri wako Mr. Kipanga
 
Tuliza akili unaweza acha mke kwa majungu...cha muhimu fanyia kazi taarifa hizo
 
Usiwe na papara, usimchukie Mkeo, na wala usivuruge amani ya nyumba yako. Mwanaume ameumbwa akawekewa koromeo, Mungu alikuwa na maksudi yake kwamba hicho ni kizibo yaingiayo ndani yasitoke, so weka moyoni na anza uchunguzi wa kina kuhusu nyendo za mkeo. kama ni kweli utabaini na kama si kweli pia utabaini ukishapata majibu yaliyo sahihi halafu Tafakari chukua hatua.
N;B ANGALIA HATUA UTAKAYOCHUKUA HAITAHATHIRI FAMILIA NA WEWE MWENYEWE KWA UJUMLA.

Ushauri wako umetulia sana Lisa! Thank you very much!
 
hakuna mtihani mgumu kama kuwa mwaminifu katika ndoa, both male and female
 
ni kweli kabisa Lisa kwasababu ni taarifa za kuletewa hatakiwi kuchukua maamuzi ya haraka, afanye uchunguzi kwanza ili aweze kubaini ukweli wa taarifa hiyo.
ukitaka kufanikiwa kitu usiwe na papara, lazima uwe na subira, na umuombe sana Mungu akuondoshee maumivu ya Moyo , na akupe hekima ili uweze kulikabili jambo kama hilo. Mimi niliambiwa Mr wangu ana mwanamke na wamezaa, basi sikuwa na papara, nilimtafuta mpk nikampata, nikahakikisha nimemchukua mtoto, Mr anarudi home anamkuta yule mtoto yupo home anacheza nawenzie, kidogo azimie, alishindwa kuuliza wala kusema chochote akaishia kubwaga mizigo na kuondoka, mm sijui alienda wapi aliporudi akataka kuanza kunihadithia nikamkatiza kuwa sitaki maelezo. mpk leo namlea mm na kama atakwenda tena nitaomba talaka. maana ujinga wakati wa kwenda tu kurudi huulizi njia.
 
huyo binti mjanja sana nadhani alikuwa anataka kukutongoza pembeni sasa ulivyojifanya kauzu eti aseme mbele ya rafiki zako kwani hata mkienda pembeni utawaambia ndio kaamua kukukomesha kwa huo uongo ili ujutie uamuzi wako. angekuwa mkweli angekupa vithibitisho vyote ili mtatue tatizo pamoja.
 
Fanya uchunguzi wa kina kwenye hili swali usikurupuke!
 
hiyo ni muhtasai wa khabari...tafuta na fukunyua taraatiiiibu kisha kupata taarifa kamili.........then soma habari kamili!
 
ukitaka kufanikiwa kitu usiwe na papara, lazima uwe na subira, na umuombe sana Mungu akuondoshee maumivu ya Moyo , na akupe hekima ili uweze kulikabili jambo kama hilo. Mimi niliambiwa Mr wangu ana mwanamke na wamezaa, basi sikuwa na papara, nilimtafuta mpk nikampata, nikahakikisha nimemchukua mtoto, Mr anarudi home anamkuta yule mtoto yupo home anacheza nawenzie, kidogo azimie, alishindwa kuuliza wala kusema chochote akaishia kubwaga mizigo na kuondoka, mm sijui alienda wapi aliporudi akataka kuanza kunihadithia nikamkatiza kuwa sitaki maelezo. mpk leo namlea mm na kama atakwenda tena nitaomba talaka. maana ujinga wakati wa kwenda tu kurudi huulizi njia.

dah! Unamoyo waujasiri sana Lisa Mungu akusaidie mumeo asije akatoka nje tena coz i know how it hurts.
 
Hapo kaka kuwa mwangalifu si kila taarifa unayopewa ni kweli, nakushauri uchunguze kwanza kabla ya kuchukua hatua . Uchunguzi wako utabaini kama hiyo message ni ya kweli au la. Pia kwanini haukumuuliza huyo mdada maswali ambayo yangekusaidia kubaini mbivu na mbichi mapema. Kwanini yeye akuambie na kutoweka. Pengine nae huyo mdada ni adui wa ndoa yako , watu bwana wanapenda sana kuingilia ndoa za watu hasa yao yanapokua yamewashinda. Usiliache jambo hili hewani , chunguza na usibadilike tu hapo home kabla hujajua mbivu na mbichi.
 
Piga kimya, fanya uchunguzi kwanza, kama kweli anatemea na mume wa huyo dada.
Ukitoka hapo kapime,hiv, kabla haujafanya uamuzi mwingine
 
Jamani mie sielewi watu, mtukatoka home kwake roho inamuuma anakuja kukupa habari na ulikubali mwenyewe iwe mbele y wenzako.

sasa unadhani yeye kuja kumtaja mumewe na mkeo itamtajirisha?

wengi huwa mnakosea mtu akikutonya hivi sio unaenda eti mnywesha mtu pombe aongee kumbuka mtu mwizi huwa mjanja na hata kama iweje mwizi na mjanja huwa hawakubali labda uwakamate papo hapo katika tendo.

mimi ningekuwa wewe pale pale ningemwita huyo dda/mama aliyechukua muda wake kunitafuta na kuja na kuongea nae kujua why anasema haya ameona nini maana utakuta namba ya mkeo inamsumbulia nyumba yake,

jamani nasema haya maana najua Tanzania wengi wanawake wanaiba nje na uwezi kuamini wana tabia hizo my friends wengine waume zao hata walale waote walie hawatakaa kamwe huhisi wanaiba.

Eti umesikia wanataka kukuvunjia ndoa ili iweje, kwani wanakufata kukutaka wakuvunjie uwe nao? maneno hayo I guess mkeo ndio anakuambia maana anajua utakuja kuanza kusikia maneno anajipanga vilivyo haswa kama sasa hivi unavyodhani anasingiziwa.

sasa ungeongea na dada huyo ungejua uanzie wapi, sasa mke kashajua na njia zao zitabadilika, kuweni wajanja jamani kukimbilia kuuliza kwa pombe eti hotelini ulidhani ndio jibu? mmh

mie ni ushauri tu kwa sie wanawake na wanaume. ulimuomba namba unajua mumewe anaishi nae vipi huko home si angeenda kumtwanga huko hadi basi,

ila nimeshaona wanawake wanaenda kwa wanaume wanasema mkeo analala au amelal ana mume wangu sasa na mimi nataka kulala na wewe ili nilipize, ndio maisha haya.

Good luck
 
Back
Top Bottom