Orketeemi
JF-Expert Member
- Feb 12, 2013
- 4,314
- 10,017
Wakuu hapa nilipo nina miaka 29.
kwa bahati mbaya bado nakaa kwa wazazi lakini ninajitegemea kwa mambo mengi isipokuwa malazi tu.
Nilikuwa nimepanga naishi mwenyewe lakini niliingiliwa na wezi na kuibiwa hivyo niliamua kurudisha mpira kwa kipa ili nijipange upya.Kilichonileta kwenu ni kwamba nimekuwa sina mahusiano ya kimapenzi ya kueleweka yaani naweza kutaka kumuoa msichana fulani lakin baada ya muda nighair na kuona hanifai . Hii ni ile waswahili wanasema ukimchunguza sana bata.
Pamoja n hayo nimekuwa na uhitaji mkubwa wa kuoa maana nahisi nikiwa na mwenzangu ntakuwa makini zaidi na maishaUtata nilionao ni kwamba kuna rafik yangu alinipa namba ya bint fulani ambaye nimewasiliana naye na kuonana naye jana. Huyu binti amenifahamisha ndugu zake ambao naweza kuwauliza ikiwa nitahitaji kumfaham zaidi.
Sasa wazo langu ni kuwa nimeona nifanye juu chini nimuoe huyu binti bila hata kumfaham vizuri , ilimradi nifaham mawili matatu tu kumhusu maana nikisema nisomane naye tabia kwanza naweza jikuta naahirisha kumuoa.Binti amekubali kwa sharti la kupima afya kwanza, ushauri wenu tafadhali.
kwa bahati mbaya bado nakaa kwa wazazi lakini ninajitegemea kwa mambo mengi isipokuwa malazi tu.
Nilikuwa nimepanga naishi mwenyewe lakini niliingiliwa na wezi na kuibiwa hivyo niliamua kurudisha mpira kwa kipa ili nijipange upya.Kilichonileta kwenu ni kwamba nimekuwa sina mahusiano ya kimapenzi ya kueleweka yaani naweza kutaka kumuoa msichana fulani lakin baada ya muda nighair na kuona hanifai . Hii ni ile waswahili wanasema ukimchunguza sana bata.
Pamoja n hayo nimekuwa na uhitaji mkubwa wa kuoa maana nahisi nikiwa na mwenzangu ntakuwa makini zaidi na maishaUtata nilionao ni kwamba kuna rafik yangu alinipa namba ya bint fulani ambaye nimewasiliana naye na kuonana naye jana. Huyu binti amenifahamisha ndugu zake ambao naweza kuwauliza ikiwa nitahitaji kumfaham zaidi.
Sasa wazo langu ni kuwa nimeona nifanye juu chini nimuoe huyu binti bila hata kumfaham vizuri , ilimradi nifaham mawili matatu tu kumhusu maana nikisema nisomane naye tabia kwanza naweza jikuta naahirisha kumuoa.Binti amekubali kwa sharti la kupima afya kwanza, ushauri wenu tafadhali.