Naomba ushauri, mke kanitoroka

Naomba ushauri, mke kanitoroka

Kwanin
Habari wana Jamiiforums

Nilisafiri kwa muda wa siku kama 35 nikaenda Morogoro kufanya kazi, baada ya kukaa siku kama 30 nilirudi nyumban ghafla kwenda kumsuprise mke wangu maana nilikuwa nimemmiss nilipofika nilipigwa na butwaa baada ya kugundua kahamisha nguo zake, viatu, vyombo na kila kitu alichonunua yeye pale ndani na kabakiza vitu vichache sana.
Basi baada ya kumuuliza vitu vyake viko wapi amesema amevipeleka kwa rafiki yake ambae mim simjui.. baada ya kukosa maelezo ya kutosha niliondoka nyumbani na kurudi jioni nikakuta kabeba kila kitu kaondoka.. baada ya kufatilia nikajua ameenda kanisani kwenye semina. Hakurejea kabisa nyumbani na kwa muda wa siku 3 hapatikani kwenye simu na wala sikujua yuko wapi.. hata wazazi wake pia hawajui. Baada ya siku tatu akaanza kupatikana kwenye simu yake ndio akaitwa kwa wazazi akaenda na kusema ameamua tu kuondoka maana ameona hatujafunga ndoa na tumekaa miaka 2 hivyo amechoka kudhini anataka amrudie Mungu wake. Ni kweli ndoa hatujafunga lakin taratibu za kiafrika zimefuatwa. sina shaka sana na kuchepuka kwa kuwa hana tabia kama hiyo. Kiukweli nimepata stress sana.. mpaka sasa sielewi nini cha kufanya. Naombeni ushauri
Kwanini umetumia new id bwana @ Gentamycine?
 
Nmesoma yote,
ila kiukweli mkuu Huu ujinga uloonesha kwenye ayo maelezo yako na uyo mkeo,

Ndo umesababisha umekimbiwa. Wanawake wahuni upenda nice guys Kama nyie, keshakuona dhaifu Sana.

Haya maelezo ukiyaeleza mbele ya wanaume wenye jazba za haraka Sana ,na makofi utapigwa mkuu, jf tunavumiliana sana.

Ulihitaji semina nzito sana ya kiume kabla Ujaoa, ila naamini hujachelewa.

Madini yapo mengi Sana Hapa, ngoja wakongwe waje.

Glenn
Extrovert
Mzee wa kupambania
Mshana Jr
Shimba ya Buyenze
 
Nmesoma yote,
ila kiukweli mkuu Huu ujinga uloonesha kwenye ayo maelezo yako na uyo mkeo,

Ndo umesababisha umekimbiwa. Wanawake wahuni upenda nice guys Kama nyie, kakuona dhaifu Sana.

Haya maelezo ukiyaeleza mbele ya wanaume wenye jazba za haraka Sana ,na makofi utapigwa mkuu, jf tunavumiliana sana.

Ulihitaji semina nzito sana ya kiume kabla Ujaoa, ila naamini hujachelewa.

Madini yapo mengi Sana Hapa, ngoja wakongwe waje.

Glenn
Extrovert
Mzee wa kupambania
Mshana Jr
Shimba ya Buyenze
Asante mkuu lkn sioni cha kushauri
 
Sina shaka sana na kuchepuka kwa kuwa hana tabia kama hiyo. Kiukweli nimepata stress sana.

Mpaka sasa sielewi nini cha kufanya.

Naombeni ushauri
 
Ningekushauri,
1. Acha kabisa kumfatilia uyo mwanamke,
Sababu Ni HAKUPENDI WALA HAKUHITAJI
-Hoja ya kanisa na kutofunga ndoa, haina mashiko Wala haina mahusiano na kubeba vitu vya ndani. HUU NI WIZI, hakuna kanisa linawatuma waumini hivo.

2.kuipeleka hoja/kesi Kama Hii kwa wazazi wako au wa MKE ni kujitangaza wee Ni dhaifu na unahitaji kubembelezewa mwanamke ili akurudie. Unawadhalilisha wazazi wako, hasa baba yako.

3. Kesi za hivi zinahitaji maamuzi magumu, afu mwanamke yeye ndo akaitafute suluhu mwenyewe kwa wazazi wako (sio wazazi wake).
 
Sasa kwanini usiende uko uko kanisani kwake ukamwambie unataka kufunga ndoa? Hili tatizo unaweza kulitatua kabisa! Panga tuu tarehe ya ndoa!

Usitoe mwanya wa watu wa kanisani kwake wakaanza kuzini nae kama wewe kuwa makini……
Hamna Mwanmke pale, Kuna kibaka.
Mnamkaribishia matatizo mwenzenu.
 
Kishapata wa kumuoa, we tafuta mwingine ukae nae miaka miwili, endelea hivyo hivyo miaka miwili miwili, kwani una cha kupoteza? Halafu wanaume nasikia hamkui wala kuzeeka na mna hela kwahiyo tunza kibunda. Na nasikia wanaume mnaweza kupata mwanamke "yeyote" muda wowote 🤣

Kikubwa tu mtumie msg mwambie aache wizi, mlokole gani mwizi? Atachomwa moto.

,😂😂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom