bad spenko
Senior Member
- Jun 22, 2020
- 125
- 137
Niende moja kwa moja kwenye point kama heading inavyojieleza.
Lengo la hii thread ni kuomba wajuzi wa hii biashara tushauriane. Nimeanzisha biashara ya kuuza kitimoto Dar maeneo ya Kibamba njia ya kwenda Muhimbili MUHAS.
Wakati naanzisha nilikua na kijana ambaye ni mzoefu wa hii kazi ya kuitengeneza lakini cha ajabu kijana niliekua nae baada ya wiki moja akaanza kulewa ovyo na kucheza betting nilipopata taarifa nikamkalisha chini abadilike lakini baada ya siku mbili alimwachia mtu funguo ili aendelee yeye simu akawa hapokei wala nini.
Nikaamua nimwache nibaki na huyu alieniletea lakini changamoto za huyu ni mchafu wa mavazi ila kazi anaiweza lakini sasa baadhi ya wateja wangu wananishauri kua huyu jamaa hakufai mazingira yake na huduma anayotoa atakupotezea wateja.
Sasa kuna dada nimempata na kazi anaiweza ila sasa nashindwa nitamsimamisha vipi ili nimwingize huyu dada napata wakati mgumu na mimi binafsi nafanya shughuli nyingine ya kuajiriwa kwa hiyo mda mwingi nakua sipo kwenye biashara yangu zaidi ni kwamba naenda jioni kwa jioni napiga hesabu zangu naondoka mda ninaokaa hapo ni mchache kama masaa 3 ivi.
Naomba kujuzwa au ushauri juu ya maelezo hapo juu wajuzi tafadhali. Nina hasira sana na maisha ya kujikwamua kwenye hali niliyonayo kwa sasa ina kama mwezi 1.
Msaada kwenu wakuu bado mi dogo janja nina 23 years. Nashindwa kuchukua maamuzi sahihi ya yupi nimweke hapo.
NAWASILISHA.
Lengo la hii thread ni kuomba wajuzi wa hii biashara tushauriane. Nimeanzisha biashara ya kuuza kitimoto Dar maeneo ya Kibamba njia ya kwenda Muhimbili MUHAS.
Wakati naanzisha nilikua na kijana ambaye ni mzoefu wa hii kazi ya kuitengeneza lakini cha ajabu kijana niliekua nae baada ya wiki moja akaanza kulewa ovyo na kucheza betting nilipopata taarifa nikamkalisha chini abadilike lakini baada ya siku mbili alimwachia mtu funguo ili aendelee yeye simu akawa hapokei wala nini.
Nikaamua nimwache nibaki na huyu alieniletea lakini changamoto za huyu ni mchafu wa mavazi ila kazi anaiweza lakini sasa baadhi ya wateja wangu wananishauri kua huyu jamaa hakufai mazingira yake na huduma anayotoa atakupotezea wateja.
Sasa kuna dada nimempata na kazi anaiweza ila sasa nashindwa nitamsimamisha vipi ili nimwingize huyu dada napata wakati mgumu na mimi binafsi nafanya shughuli nyingine ya kuajiriwa kwa hiyo mda mwingi nakua sipo kwenye biashara yangu zaidi ni kwamba naenda jioni kwa jioni napiga hesabu zangu naondoka mda ninaokaa hapo ni mchache kama masaa 3 ivi.
Naomba kujuzwa au ushauri juu ya maelezo hapo juu wajuzi tafadhali. Nina hasira sana na maisha ya kujikwamua kwenye hali niliyonayo kwa sasa ina kama mwezi 1.
Msaada kwenu wakuu bado mi dogo janja nina 23 years. Nashindwa kuchukua maamuzi sahihi ya yupi nimweke hapo.
NAWASILISHA.