nbayoungboy never broken
JF-Expert Member
- Apr 20, 2025
- 383
- 365
Nilijitafuta nikapata mtaji wangu wa takriban milioni 3, nikaona si vibaya nikitumia kukuanzishia biashara.
Nilianza kwa kutafuta fremu, nikaipata, lakini mwenye fremu aliniambia nilipie kodi ya mwaka mzima kwa kuwa eneo lilikuwa katikati ya shughuli. Nikalipa shilingi laki saba kwa mwaka.
Nikaamua kufanya biashara ya nafaka kama mchele, maharage, n.k. Nikanunua mizani na vifaa vyote muhimu.
Biashara ikaanza na mauzo yakawa ya wastani – kuna siku nauza elfu 20, nyingine elfu 50, mara nyingine elfu 70 au hata elfu 10 – yote ilitegemea na wateja waliokuwa wanajitokeza, pengine bahati mtu anaweza kuja kuchukua kilo nyingi.
Mauzo yakaanza kupanda hadi kufikia elfu 150 hadi elfu 180 kwa mwezi, na hata mara tatu ya hapo kulitegemea msimu.
Nikaona ni vizuri nijiongeze, nikaweka ngazi kama ya duka na kuanza kuweka bidhaa za elfu 6 juu ya ngazi hiyo.
Lakini changamoto ilikuja pale mauzo yalipoanza kurudi kule kule kwenye elfu 10 kwa siku. Nikawa najiuliza – je, niendelee kuongeza bidhaa na kujaza duka, au niuze bidhaa zote nilizonazo kwenye ngazi zimalizike kabla ya mwaka kuisha?
Nione faida na hasara zake, halafu nikae chini nihesabu kama baada ya kulipa fremu na matumizi mengine bado hela itaniruhusu kuendelea na biashara au nifunge na nitafute shughuli nyingine?
Nilianza kwa kutafuta fremu, nikaipata, lakini mwenye fremu aliniambia nilipie kodi ya mwaka mzima kwa kuwa eneo lilikuwa katikati ya shughuli. Nikalipa shilingi laki saba kwa mwaka.
Nikaamua kufanya biashara ya nafaka kama mchele, maharage, n.k. Nikanunua mizani na vifaa vyote muhimu.
Biashara ikaanza na mauzo yakawa ya wastani – kuna siku nauza elfu 20, nyingine elfu 50, mara nyingine elfu 70 au hata elfu 10 – yote ilitegemea na wateja waliokuwa wanajitokeza, pengine bahati mtu anaweza kuja kuchukua kilo nyingi.
Mauzo yakaanza kupanda hadi kufikia elfu 150 hadi elfu 180 kwa mwezi, na hata mara tatu ya hapo kulitegemea msimu.
Nikaona ni vizuri nijiongeze, nikaweka ngazi kama ya duka na kuanza kuweka bidhaa za elfu 6 juu ya ngazi hiyo.
Lakini changamoto ilikuja pale mauzo yalipoanza kurudi kule kule kwenye elfu 10 kwa siku. Nikawa najiuliza – je, niendelee kuongeza bidhaa na kujaza duka, au niuze bidhaa zote nilizonazo kwenye ngazi zimalizike kabla ya mwaka kuisha?
Nione faida na hasara zake, halafu nikae chini nihesabu kama baada ya kulipa fremu na matumizi mengine bado hela itaniruhusu kuendelea na biashara au nifunge na nitafute shughuli nyingine?